Jamani habari zenu? Kwa muda mrefu nimekua nikila chakula maeneo ya cafeteria iliyoko ndani ya mabibo hostel. Lakini niliamua kuacha kabisa kula cafeteria baada ya siku moja kuona paka wakilambalamba sahani za chakula mezani.
Baada ya hapo nikahamia nje pale kwa wapemba. Kinachonipa shida ni kwamba nikila hapo kwa wapemba tumbo hua linajaa gesi kwa muda mrefu. Ndipo siku moja nikaambiwa na mtu mmoja kua kuna uwezekano hawa jamaa hua wanatia hamira ktk chakula.
Sasa kama hali ndo hii mimi nawashauri wananchi wenzangu tuwakemee hawa jamaa waache kutuwekea hamira kwenye chakula wanatuumiza kiafya.
Kwa sasa natafuta sehemu nyingine ya kula ila tatizo mitaa ya huku mabibo hostel hakuna mkahawa wenye kujali afya za walaji japo kwa kiwango cha mamantilie, yaani uchafu, vyakula ni kama unakula mataputapu, kauli zao mbovu, nk.
Kwa hiyo nawaombeni sana wateja tunaojazana kwa wapemba kila siku tujali afya zetu kwa kushirikiana kuwakemea.
Baada ya hapo nikahamia nje pale kwa wapemba. Kinachonipa shida ni kwamba nikila hapo kwa wapemba tumbo hua linajaa gesi kwa muda mrefu. Ndipo siku moja nikaambiwa na mtu mmoja kua kuna uwezekano hawa jamaa hua wanatia hamira ktk chakula.
Sasa kama hali ndo hii mimi nawashauri wananchi wenzangu tuwakemee hawa jamaa waache kutuwekea hamira kwenye chakula wanatuumiza kiafya.
Kwa sasa natafuta sehemu nyingine ya kula ila tatizo mitaa ya huku mabibo hostel hakuna mkahawa wenye kujali afya za walaji japo kwa kiwango cha mamantilie, yaani uchafu, vyakula ni kama unakula mataputapu, kauli zao mbovu, nk.
Kwa hiyo nawaombeni sana wateja tunaojazana kwa wapemba kila siku tujali afya zetu kwa kushirikiana kuwakemea.