Tunamkumbuka Edward Sokoine - Mtu wa Watu

Kyomo

Weka mambo; Hawa vibaka iko siku watafagiliwa na tutawaweka ukonga huwezi kuhujumu nchi namna hii halafu unakaa na kuwabeza wale unaofuja pesa zao.
 
Kyoma; its good to know that you are back and in one piece. Ukiona umesema jambo likazua mtafaruku ujue umegusa mahali yake kama waswahili wanavyosema. Hawa manyang'au wamekuwa waroho hata wamesahau kuwa hizo fedha wanazopewa na kuzitumia kwa manufaa yao zinakuwa documented for the whole world to see. wanafahamu fika kuwa sio rahisi mwananchi wa kawaida kujua ni nini kinaendelea ndio maana kuweka kwako data hapa kumewa-provoke; they thought it is a secret....ama kweli ulafi ni ugonjwa.
Najaribu kufikiri kama ni hivi ndani ya mwaka mmoja wa uongozi wa jeikei tumekopa kuliko tulivowahi kukopa for the past 45 years of independence basi come five years atakuwa ametuacha mahali pa kuwa salvaged kama Titanic!

Kwanza naona kumlinganisha lowassa na Sokoine ni kumpandisha sana chart..huyu jambazi la mchana utamfananisha na sokione jamani huyo marehemu si atageuka huko kaburini..nadhani hapo walipo Nyerere na Sokoine wanatafakari namna ya kumshawishi Mungu awape sabbatical leave waje kuinusuru nchi hii mikononi mwa hawa majambazi!

Na waendelee kutishia tu lakini ukweli si unauma.!
 
Mheshimiwa Kyoma,

Hizi hoja zako ni nzito mno na ndio faida ya kuwa na forum kama hii maana vinginevyo isingelikuwa rahisi kwa hoja kama hizo kutolewa. Hongera sana mzee kwa kutufundisha.

JF itanemeeka kwa watu wenye data na hoja za nguvu kuzimwaga.

Kuna watu wengi sana wanajua ukweli juu ya hawa majangiri wanaotuibia na wana data pia lakini wanakaa kimya. Hawa ni wasaliti wa umma sawa tu na hao majangiri wenyewe.

Wakati umefika wa watu mbalimbali kutumia kila njia kuhakikisha baadhi ya siri za hawa majangiri zinatolewa nje ili wananchi tuelewe.

Humu ndani kuna civil servants wengi tu na wanajua mambo mengi ambayo ni mabaya kwa taifa lakini wanakaa kimya.

Mzee Kyoma hizi jumbe zako zimenigusa sana maana sisi ni vijana wa Sokoine ambao wakati anakufa tulikuwa mashuleni, na tulitaka tubebe jeneza lake mpaka kule Arusha. Sitaweza kumsahau Sokoine na Watanzania tunafanya kosa kubwa sana kutomkumbuka huyu mzee.
 
Yebo Yebo;
Its good to share with us what you experienced but mind you, if you beleive in maintaining your anonymity thats the easiest way of exposing yourself..the people who were with you will have no problem in identifying you if they read this episode..that is, free advice
 
Mnajua kama huyu Kyoma kanifanya nikae mpaka usiku wa manane nasoma makala zake ...sasa kama mlikuwa na ushauri pelekeni kwenye thread ya ushauri

Kyoma rudi tena bwana maana kuna maswali mengi nataka nikuulize na
 
Hey

Wajameni tusikilize ushauri ya DrWHO hii makala ni ya kumkumbuka Marehemu Sokoine...makala na maoni pelekeni kuleeee.
 
sawa sawa Bob Mkandara,

kwa kifupi ni kuna mada chache ambazo binafsi niliona nakosa mchango wako ikiwemo hii ya Sokoine. hata hivyo endelea kuchemsha kweli kweli hayo maisha hata kama nimachungu kama chloroquine, utapata ahueni lakini bado utawashwa tu
 
Kyoma:

Nashukuru kwa michango yako mizuri. Nashauri uihariri itoke kama makala kwenye magezeti ya nyumbani ili watanzania wengi zaidi waisome. hata kama utatumia pen name. Mazenge kwa mfuga mbwa kumeanza kubadilika. Kutabadilika zaidi kama utakuwa wakala wa mabadiliko unayotaka kuyaona. Najua unanielewa nikizungumza hii lugha ya kiubungo ubungo.

JJ
 
Kyoma:
Nashukuru kwa michango yako mizuri. Nashauri uihariri itoke kama makala kwenye magezeti ya nyumbani ili watanzania wengi zaidi waisome. hata kama utatumia pen name. Mazenge kwa mfuga mbwa kumeanza kubadilika. Kutabadilika zaidi kama utakuwa wakala wa mabadiliko unayotaka kuyaona. Najua unanielewa nikizungumza hii lugha ya kiubungo ubungo.
JJ

Mnyika, heshima yako mkuu,

Sijamalizia huu mjadala wa Sokoine. Mzee Jokakuu alinishauri kuwa mapande yangu ni marefu mno, hivyo, nimetoa muda wa kuyameza na kuruhusu maswali pamoja na uchangiaji kutoka kwa wanabodi. Ni kweli, kuna umuhimu wa kuwa na idadi kubwa ya wanabodi ambao watajitolea kuchukua kurasa katika magazeti ya nyumbani na kuandika makala ili kuwashirikisha watanzania wengi katika kuchanga bongo. Huu utakuwa mkakati mmojawapo wa Jambo Forums katika harakati za kuwafikia walengwa, ambao ni watanzania wote.

Nilijaribu kuwasiliana na baadhi ya vyombo vya habari ili nipate fursa ya kuchangia makala kila wiki. Hata hivyo, juhudi zangu hazijafanikiwa mpaka sasa. Manyika, umekwisha ona michango yangu sehemu nyingine nikitumia jina langu, hivyo sioni tatizo kutumia jina langu katika makala zote. Ningefurahi, kuzihariri makala zangu zote nilizozituma Jambo Forums ili ziandikwe kwenye magazeti. Pia naweza kuchangia makala kila wiki bila malipo. Masharti yangu ni kuwa, makala zangu zote, pamoja na kuwa zitachapishwa magazetini, iwe ni haki yangu, kwa maana kuwa, hata siku za usoni nikitaka kuzikusanya na kuziweka katika mfumo wa kijarida au kitabu, isiwepo songombingo ya nani anamiliki hizo makala.

Pili, natambua kuwa magazeti yana wahariri, na wengine wangependa kuzichapisha makala kwa mtindo unaoshabihiana na misimamo ya vyombo vyao. Nisingependa kuona kuwa hoja zilizobeba msingi wa makala zinatolewa, au kuongezwa hoja nyingine kwa kisingizio cha uhariri. Ningependelea uhariri kwa maana ya kusaihisha lugha na uumbaji wa sentensi, au kuiandika upya makala kwa kutumia lugha wanayoipenda bila kubadilisha maana ya ujumbe wangu.

Bado natafuta, na nikifanikiwa kupata chombo cha maana, nitatekeleza wajibu huu. Kama unaweza kusadia upatikanaji wake, unakaribishwa kwa moyo mkunjufu.
 
Ogah,

Shukran mzee mwenzangu, hiki kijiwe kimefika mahala ambapo sina uwezxo tena wa kuchangia mengi ila nitabakia nyuma hadi hapo nitakapo rudi mjini!... bado nafukuzana na kuku wa kuchinja. Internet cafe wizi mtupu, simu wizi mtupu na mengine mengi yasiyosemekana.

Nimekutana na bwana mmoja ambaye anaitwa Chobuyaga, huyu jamaa ana data kama vile katia wazimu. Nimemuomba ajiunge na kijiwe hiki naye kisha itikia wito. Huyu naweza sema Mzee ES....mtoto (samahani uncle).

Nitakacho sema ktk issue ya Sokoine ni kwamba hata Mussa baada ya kuwaopkoa Wayahudi alikuja kanwa na wayahudi wenyewe. Na kama unaijua historia ya baadhi ya dini fulani toka huko Asia ya mbali imetokana na upinzani wa maajabu ya Mussa. Leo mwambie Baniani kuwa Mussa ni nani hawana kabisa habari nae isipokuwa Krishna!... nadhani umenipata.

Hivyo basi kubishana sana juu ya Sokoine na kuanza kumfananisha na sijui nani ni sawa na kutafuta mfano wa Yesu na Mungu ukiwasimulia waislaam. Mtakesha...pamoja na kwamba daraja la Yesu halina mfano wa sisi binadamu walala hoi kulijadili wakati sisi hata hiyo pepo hakuna kati yetu atakaye ikaribia acha mbali kuingia.

Muhimu, jamani tuzungumzie issue zinazotugusa leo hii. Usafiri wa dala dala (Vipanya) ni adhabu kubwa sana kwa nchi yetu yaani aibu kubwa!..

Tanzania leo hii ni mwendawazimu anayetembea uchi kama mbwa na ajabu watu wanahesabu idadi ya mijibwa inayokuja kujisuuza kisha tunafikiri wingi huo kama ni sababu ya ubora na uzuri wa jibwa hili Tanzania...

Kumbuka vizuri ile hadithi ya maisha ya mama yetu Tanzania... ukisha ichambua na kuelewa nini maana ya maelezo yale, hakika utakuwa umeelewa zaidi tofauti ya Viongozi wa leo hii na wale waliotangulia...

Jamani eeeeh! Tumekwishaaaa! Mwacheni Sokoine jamani jitazameni wenyewe tunavyo bashiwa Kiuchumi!.. au sababu ni kuwa usenge wa kiuchumi ni ustaaarabu mpya? Kumradhini na hii lugha ya mtaani.

Tumekwisha toka enzi ya Mwinyi tena vibaya vibaya. nakupeni swali moja tu - Ni nani mmliki wa majumba ya Sofia house hapa mjini Dar? na yapo mangapi? nani mmliki wa kituo cha mabasi Ubungo? Majumba yote ya MHC na Msajili yanaposhushwa na kujengwa jumba jipya akina nani wana share zao ndani. Hupewi wewe mlalahoi uliyeputa kwa mguu tokakila kona ya mji kuja fanya kazi mjini. Akina nani wamerudi na kuyachukua majumba hayo karibu yote na hizo fedha zao za ununuzi zinakwenda wapi. Mfuko waserikali inapata nini toka majumba haya!... Utaambiwa serikali haifanyi biashara... Huu si wendawazimu!

Na imekuwaje nyumba za MHC na Msajili ambazo zilitaifishwa leo hii ziuzwe na wapangaji kwa watu kwa millioni 50 ama kupangishwa chumba kwa dollar 300 kwa mwezi hali hao wapangaji hawakuchangia hata tofali?..Na hao wanaopangisha majumba kweli wanalipa kodi ya upangishaji?..maanake tukumbuke upangishaji ni biashara.. acha mbali uharamu wa kupangisha nyumba ya serikali.

Hakuna hata kiongozi mmoja ndani ya CCM leo hii ambaye ana maisha ya kawaida yaani sawa na mfanyakazi yeyote yule.. NO ONE!... wote matajiri bila mtaji elimu wala ujuzi.

Mwacheni Sokoine, hakuna kitakacho tusaidia... tuendelee kufukuzana na kuku wa kienyeji...
 
Mkandara: Muhimu, jamani tuzungumzie issue zinazotugusa leo hii. Usafiri wa dala dala (Vipanya) ni adhabu kubwa sana kwa nchi yetu yaani aibu kubwa!..
Tanzania leo hii ni mwendawazimu anayetembea uchi kama mbwa na ajabu watu wanahesabu idadi ya mijibwa inayokuja kujisuuza kisha tunafikiri wingi huo kama ni sababu ya ubora na uzuri wa jibwa hili Tanzania...
Kumbuka vizuri ile hadithi ya maisha ya mama yetu Tanzania... ukisha ichambua na kuelewa nini maana ya maelezo yale, hakika utakuwa umeelewa zaidi tofauti ya Viongozi wa leo hii na wale waliotangulia...

Shukran kwa kupata muda angalau kuandika kidogo - Miaka 45 ya uhuru bado nchi inatumia vyoo vya shimo ambavyo ukienda chooni inabidi uruke kama chura hususan kariakoo, je hawa viongozi tulionao wanajali kweli maisha ya WTZ? EL kipindupindu kitaisha vipi Dar wakati bado tunatumia vyoo vya enzi za Abunuwasi?
 
Ogah,
Shukran mzee mwenzangu, hiki kijiwe kimefika mahala ambapo sina uwezxo tena wa kuchangia mengi ila nitabakia nyuma hadi hapo nitakapo rudi mjini!... bado nafukuzana na kuku wa kuchinja. Internet cafe wizi mtupu, simu wizi mtupu na mengine mengi yasiyosemekana...

Mkandara
ni afadhali umeyaona mwenyewe. Maana wengine tukisema hapa makuwadi wa soko huria wanaanza kuorodhesha ati uwingi wa makampuni ya simu bongo ndio faida zenyewe za ugenishaji? Hivyo vibanda vya internet ndio balaa kubwa maana pesa yako inaenda hivi hivi unaiona. danganyika yetu ni kiza kitupu huko mbeleni.
 
Wanabodi,

Hakika nimesoma mengi hapa Bongo na sidhani kama kutakuja kuwepo na kiongozi ama msomi hata hata mmoja atakaye simama na kusema MAENDELEO hua hivi!...Dua kama ulikuwepo... leo hii hakuna umeme mji mzima, magenereta tu yanapuyanga. Mikoa mingi taa za barabarani haziwashwi, umeme ni majumbani mwa watu. Hapa Dar unahesabu kirahisi taa zinazowashwa hususan pale kwenye (transformer). Kisima cha maji kuchimbiwa ni millioni mbili!, kisha biashara ni kuuza maji kwa jirani. Barabara zetu zinajengwa na makampuni ya ndani (Wahindi) wasiokuwa na vifaa vya ujenzi ila huenda ku-lease ktk makampuni. Wamiliki halisi ni akina nani?...hesabu kwenu.

Tabasamu hizo simu nimekoma mwenyewe yaani card ya dollar 5 utaongea chini ya dakika 10 kwa cell hapa hapa mjini. tusije wasemea ovyo wabongo kwa kutuma message tu. Wapi duniani kuna bei kama hii ya Bongo? hiyo TV cable ni kitu kama dollar 65 kwa mwezi na hakuna vipindi muhimu zaidi ya mpira ama ligi ya Ulaya kisha utawasikia wenyewe wakidai kuwa haya ndoo maendeleo. Sinema za hapa ni michezo ya kuigiza ( iwe comedy ama tamthilia). Majumba yanajegwa hovyo hovyo mitaani bila kufikiria miaka 20 ijayo traffic itakuwaje ktk mtaa huo!..Hivi kweli tuna wasomi nchini ama? Miti mikubwa imepandwa kila mtaa hadi ktk milango ya maduka na miti hiyo ina asili ya mizizi mikubwa ikisha kuwa. Sijaona barabara hata moja yenye mitende mjini. Kisha miti hiyo hiyo imegeuzwa kuwa vijiwe vya watu... hakuna ajira mjini, wafanye nini?

Kisha nimalizie kwa habari za mtaani.. Ndugu zangu hakuna wakereketwa kabisandani ya lingo la Siasa!.. ni zero tunawasikia akina Zito na J.J humu ndani huko nje jamani,hawa jamaa wenyewe wanapwaya sana. Kuna ukiritimba na mafia kali sana ambayo hakuna mwanasiasa yeyote toka CCM na upinzani haiogopi. In reality wote wanajua kuwa matokeo. Yaani ndoo Tatanic imeshagonga mwamba na inazama taratibu huku mkionyeshwa urefu wa deck lake linavyopanda juu kama ishara ya uchumi bora.

Hiyo 10% ni kila ofisi ya serikali na mashirika utakayo tembelea na wala haiombwi toka chini. Je, mnaweza kuamini kuwa hata Mtikila kuna issue anaziogopa pamoja na kwamba zina ukweli?..Bongo jamani Bongo hii ya leo kiboko!..

Jasusi,
Hizo nyumba ndugu yangu ni za mke wa rais mstaafu ( utajaza mwenyewe) akitumia wahindi. Na habari inayofunga kazi ni kwamba hata Manji sii tajiri utajiri wake anatumiwa na vigogo kuficha makucha yao.

Brother nyumba za serikali leo hii ni biashara kubwa sana nchini yaani zinamegwa vibaya vibaya kwa kutumia wawekeshaji bandia ikifuatiwa na mchanga wa dhahabu toka machimbo yetu na yale ya Congo.

Naomba tu mtu kama mimi niwekwe kwenye hiyo Taasisi mpya ya rushwa maanake nafahamu mbinu zote zinazotumika..

Hata hivyo Nafasi bado zipo kwa walemavu sisi ikiwa unaweza kuyakoga. Nje ya hapo tutakuwa tunadanganyana kabisa JK hawezi kubadilisha kitu...Nasema hawezi kwa sababu nyingi sana ikiwa kweli anayathamini maisha yake kwani huwezi kuokoa jahazi baharini ikiwa limekwisha ingia maji. Anachoweza kufanya ni kujiokoa yeye mwenyewe na wachache ambao anaweza kuwabeba mgongoni sii taifa zima...Nchi ni corrupt kupita kiasi kwa hiyo jamani join the club. Huo muswada mpya ni hadithi ya Alinacha!...ndoto za mchana kama ile isemayo Anayepanda juu msubiri chini!....bila kuzingatia kuwa huyo aliyepanda ni mwewe na kesha kachukua kifaranga, Atashuka lini? kama sii kurudia kifaranga kingine.

Imetosha, narudi mtaani kumfukuza kuku wa kienyeji....
 
Mkandara,

Nani atakuweka kwenye hicho kitengo cha rushwa? Kinachotakiwa sasa
ni kuficha makucha mpaka siku ikifika unayatoa makucha makubwa kuliko ya chui. Nafikiri njia pekee ni kutumia mtindo wa De Clerk au Goberchev.

Tusikate tamaa kuna siku huo umafia wao utakwama tu.
 
Back
Top Bottom