Tunalaani kitendo hiki, hakivumiliki!


Mimi nadhani si kazi kubwa sana kubaini ni nani au akina nani behind this act – na hasa iwapo vyombo vya usalama havitaweza kuwakamata. Ni watu ambao hawakamatiki katika nchi hii – maana wako juu ya sheria – hufanya jinai yoyote watakayo na serikali ya Muungwana inabakia kuwa impotent.

Kwanza kabisa – ile kesi ya Kubenea kumwagiwa tindikali imefikia wapi? Hakuna chochote kinachoendelea na nimesikia mashahidi wanatishwa kwenda kutoa ushahidi – na waliokwenda wamepotea (disappeared) bila kunekana.

Pili kesi moja ya kubwa ya EPA (ile ya Kagoda) bado haijatinga mahakamani, pamoja na kuwepo ushahidi tosha – wa kutoka CRDB – wa nani (au akina nani) walilipwa yale mabilioni in cash – over the counter. Takukuru wameshindwa kupata ushahidi huo wa wazi kwa sababu walipwaji hao wako above the law kuliko Watanzania wengine. (Linganisha na watuhumiwa hawa wa wizi wa TTCL/TRA – kwa kuwa ni wale walio chini ya sheria.)

Tatu hivi karibuni gazeti hilo la Kubenea limemuanika waziwazi EL kuhusu suala la Richmond baada ya kuandika tuhuma mpya kabisa dhidi yake za kampuni ya CDC ya Canada ya kuzalisha umeme, kampuni ambayo EL alifuta tenda yake na badala yake kuiingiza Richmond!

Tuhuma hizi mpya bila shaka zimemuumiza sana EL ambaye siku chache tu zilizopita ‘alijitetea' katika TBC1 akimtumia swahiba wake Tido kuhusu kashfa ya Richmond inayojulikana. Kuja kwa hii mpya ya CDC ambay ilikuwa bado haijulikani bila shaka kumemuumiza sana EL – tena sana – maana alifikiri alikuwa amelimaliza suala zima la Richmond.

Kwa hivyo wana-JF mtajua ni akina nani wako behind this latest attempt on the life of Kubenea. Nadhani mwenyezi Mungu anamuweka ili amalize kile alichomtuma kuikomboa nchi hii kutoka kwa makucha ya mafisadi.
 
MIMI NAWALAANI HAWA MUNGIKI KWA KITENDO HIKI BILA KUJALI KWANINI WAMEFANYA HILI.....MAANA SO FAR HATUJUI SABABU YA HAYA KUTOKEA KWA SAID KUBENEA....INAWEZEKANA KUNA DIMENSIONS NYINGI KATIKA TUKIO HILI......

Ila msisahau jamani hawa watu wanaovamiwa ni binadamu wa kawaida wanaweza kuwa na mambo mengine mengi tusiyoyajua yakasababisha kuvamiwa si lazima iwe tasnia yao tu......kwani watu wote wanaovamiwa mitaani ni wana habari? na wanataka kunyamazishwa? wengine wanavamiwa kwa chuki za kifamilia....wizi wa wake au waume...different reasons.

KAMA KWELI WALIMVAMIA KWA SABABU YA KUMYAMAZISHA HAKIKA NI WACHAWI WA DEMOKRASIA

MIX WITH YOURS
 
Huamini nini wakati ulimsikia kiranja mkuu wa viranja akisema kuwa atawashughulikia wote wanaomsema vibaya na wengine ameshawashughulikia?
Mchukia Fisadi, this is too serious issue ila nashauri,kulinda heshima ya JF, lets not point fingers ila one thing for sure, siyo kiranja mkuu, wala sio SS, hawa ni wahuni fulani tuu ambao Kube amekwaruzana nao katika haya na yale.

Kiranja mkuu ni omni present, vijana wake hawawezi kupatafuta kwa Kubenea kwa sababu jicho lao, linamonitor every move he make, wanasikia everything he says na naamini anacop nao vizuri tuu, if not working for them, hivyo they have 101 ways to deal with him, clean, soft and natural way like smooth oparator, wale ni holigans tuu.

Naunga mkono hoja ya kulaani, na kuhamasisha tuchague mabadiliko, vinginevyo, things will always be the same again.
 
Mchukia Fisadi, this is too serious issue ila nashauri,kulinda heshima ya JF, lets not point fingers ila one thing for sure, siyo kiranja mkuu, wala sio SS, hawa ni wahuni fulani tuu ambao Kube amekwaruzana nao katika haya na yale.

Kiranja mkuu ni omni present, vijana wake hawawezi kupatafuta kwa Kubenea kwa sababu jicho lao, linamonitor every move he make, wanasikia everything he says na naamini anacop nao vizuri tuu, if not working for them, hivyo they have 101 ways to deal with him, clean, soft and natural way like smooth oparator, wale ni holigans tuu.

Naunga mkono hoja ya kulaani, na kuhamasisha tuchague mabadiliko, vinginevyo, things will always be the same again.


Yaaa lazima tubadilike .....'multi dimensions.....miaka ya 1990 kuna profu mmoja wa SUA aliua na jamaa wakachukua gari na kulitelekeza somewhere...sasa kwa sababu yule prof alikuwa anapenda wake za watu...basi alipouawa tu tetesi zikasambaaaa kuwa ameua kwa sababu ya WIZI WA WAKE ZA WATU....mmmmh hakukuwa na namna ya kuwa convisi watu vinginevyo....nasikitika hata mimi wakati huo niliamini hilo lakini kua uwezekano kuwa wala wale watu hawakumuua kwa sababi hiyo ila 'tabia yake iliyoozoeleka ilikuwa hiyo basi hata kifo chake kilikhusishwa hivyo.....hii ina maana angekuwa mkosoaji wa serikali basi pia ingeelezwa ni sababu za kuikosoa serikali..
mix with yours
 
Invisible,

i) Asante kwa Taarifa hii japo ya huzuni hasa ikizingatiwa si mara ya kwanza kwa Kubenea, na sote tunafahamu jinsi kesi iliyoko mahakamani inavyoenda. Inasikitisha lakini ndiyo hali tuliyonayo.
ii) Naungana nawe kulaani kwa nguvu zote matendo ya aina hii. Hakuna asiyeweza kuunganisha kwa ulaani kabisa kwanini Kubenea amekuwa Target ya mara kwa mara ya vituko hivi. Ningependa kumshauri Kubenea, pamoja na kuwa Jeshi letu halichukui kwa kuuzito matukio haya, kwa sababu yeyote ile, kama ilivyotokea kwangu wakati nilipowekewa kifaa cha kunasia Sauti chini ya kitanda pale Dodoma, na Polisi siyo tu wamekaa kimya bali pia kutangaza kisingizio cha kuwa ni binti yake Slaa ndiye aliyeingia chumbani, atoe maelekezo ya kina polisi ikiwa ni pamoja na namba za simu anazohisi ni za vitisho, kumtukana baada ya matoleo ya Gazeti la Mwanahalisi analolimiliki.
iii) Kulaani tukio ni jambo mmoja, lakini nadhani kuendelea kukaa dhidi ya polisi wanaokaa kimya na kupuuzia matukio haya ni jambo baya zaidi. Hali hii ya polisi kutochukua hatua ndiyo hatimaye inawafanya raia wema kujichukulia Sheria mikononi mwao. Tusingelipenda kuona haya yanatokea. Hivyo, wote wenye nia njema tutoe kauli kali kuishinikiza polisi ichukue hatua za kisheria kulinda raia zake.
iv) Mengine sina sababu ya kuyazungumza hapa, wenzanguwamekwisha yasema. Nauungana mkono nao.
 
mtu unakuwa mkimbizi kwenye nchi yako mwenyewe? this is real bad, wako wapi wakina mama wanaojua kulia na kuomboleza waiombee nchi yetu? maana naona Mungu keshaghairi na amani imepotea kabisa.
babu yangu aliwahi niambia kuwa Tz now ni kama shamba lenye nyasi zilizokauka, siku likitiwa moto linalipuka lote. siombei tufike huko but where are we going?

Kwenye rangi- usingeweza kuwa sahihi zaidi!
 
Nami naungana na wengine kulaani kitendo hiki.

Kwanza, sikubaliani na wale wanaohusisha tukio hilo na ugomvi binafsi. Kuna ushahidi usio na shaka kwamba kila gazeti linapoandika taarifa za EL na RA, Kubenea anatumiwa ujumbe wa maandishi wa vitisho. Hata sasa ambapo gazeti limeibua mapya ya EL, Kubenea ametishwa kupitia ujumbe wa simu ya mkononi SMS ambao tayari ameuripoti polisi.

Lakini jingine ni hili: Kwamba kila pale ambapo gazeti limekuwa likiibua taarifa na makala za uchambuzi zinazomhusu Lowassa, maisha ya Kubenea yanakuwa hatarini. Anatishwa na kusakamwa.

Hivyo, mimi nakunganisha tukio hilo na mambo manne.

Kwanza, Lowassa aliyeanikwa na Mwanahalisi kuwa alifuta zabuni ya CDC na kuipa kazi kampuni yake ya Richmond.

Pili, kauli ya "Bwanamkubwa" pale Dodoma, kwamba gazeti hilo limemgombanisha na viongozi wa kidini baada ya gazeti kumuanika kwamba alikataa kula chakula cha viongozi wa kidini kule Bukoba.

Tatu, makala ya yule mwanamipasho (Sofia Simba) ambaye imesababisha serikali kuja juu na kutaka kufunga gazeti.

Nne, mgogoro wa muda mrefu kati ya Rostam na Kubenea uliosababisha kufikisha mahakamani na hivi karibuni kumlipua kwamba ndiye mfadhiri mkuu wa kampeni za urais za Dk. Mohammed Gharib Bilali kule Visiwani.

Hayo ndiyo yaliyojiri kwa leo…
 
Huamini nini wakati ulimsikia kiranja mkuu wa viranja akisema kuwa atawashughulikia wote wanaomsema vibaya na wengine ameshawashughulikia?

nalaani hichi kitendo sana....lakini,hivi kweli watu unaosema wanamtafuta watashindwa kujua kahamia wapi na umaarufu wake wote huyo KUBENEA??
 
Nami naungana na wengine kulaani kitendo hiki.

Kwanza, sikubaliani na wale wanaohusisha tukio hilo na ugomvi binafsi. Kuna ushahidi usio na shaka kwamba kila gazeti linapoandika taarifa za EL na RA, Kubenea anatumiwa ujumbe wa maandishi wa vitisho. Hata sasa ambapo gazeti limeibua mapya ya EL, Kubenea ametishwa kupitia ujumbe wa simu ya mkononi SMS ambao tayari ameuripoti polisi.

Lakini jingine ni hili: Kwamba kila pale ambapo gazeti limekuwa likiibua taarifa na makala za uchambuzi zinazomhusu Lowassa, maisha ya Kubenea yanakuwa hatarini. Anatishwa na kusakamwa.

Hivyo, mimi nakunganisha tukio hilo na mambo manne.

Kwanza, Lowassa aliyeanikwa na Mwanahalisi kuwa alifuta zabuni ya CDC na kuipa kazi kampuni yake ya Richmond.

Pili, kauli ya "Bwanamkubwa" pale Dodoma, kwamba gazeti hilo limemgombanisha na viongozi wa kidini baada ya gazeti kumuanika kwamba alikataa kula chakula cha viongozi wa kidini kule Bukoba.

Tatu, makala ya yule mwanamipasho (Sofia Simba) ambaye imesababisha serikali kuja juu na kutaka kufunga gazeti.

Nne, mgogoro wa muda mrefu kati ya Rostam na Kubenea uliosababisha kufikisha mahakamani na hivi karibuni kumlipua kwamba ndiye mfadhiri mkuu wa kampeni za urais za Dk. Mohammed Gharib Bilali kule Visiwani.

Hayo ndiyo yaliyojiri kwa leo…

Kama nilivyotamka katika reply yangu hapo juu (#42) siyo kazi kubwa kubaini ni akina nani wana ijasiri wa kufanya uharamia huu bila kuguswa na vyombo vya dola. Hawa wanajulikana na kila mtu ambaye anaitakia nchi hii mema kwa kuwepo utawala wa haki na kuzingatia sheria. Nadiriki kusema kuwa nchi hii haitatulia kamwe, hata kama JK akishinda term ya pili -- hadi hapo wanaotamba kuuweka utawla wake mfukoni watachukuliwa hatua kwa madhambi yao.
 
.. du, kusema ukweli Tz sasa inakwenda kubaya zaidi. Mbona hii inataka kufanana na ile ya the late Prof wetu wa Sheria?... Tuliombee taifa letu limgeukie Mungu.
 
Wasubiri chadema wachukue inji hii
Wao kwa sasa wana kinga maana ni mojawapo ya watu wanaolinda ufisadi na kuchagua nani akamatwe nani aachwe na kulindwa
Jamani tulaani haya mambo lakini tunahitaji mabadiliko ya dhati kabisa.

Kumbukeni kwa miaka hii mitano waandishi machachari wangapi wameingia matatizoni kwa kuandika na kutangaza ukweli. na tunakwenda wapi.
Jamani mabadiliko ya uongozi tuyaombe kama mama mgumba anayeteswa na mmewe na nduguze aombavyo.
tukemee na kulaani kwelikweli. lakini hii ni mifugo ya uongozi uliopo na nafasi yetu ya kubadilisha ndo hii.
 
.. du, kusema ukweli Tz sasa inakwenda kubaya zaidi. Mbona hii inataka kufanana na ile ya the late Prof wetu wa Sheria?... Tuliombee taifa letu limgeukie Mungu.
Ni kweli hata huyo na wengine kibao. Inaonesha kuwa hawa jamaa ndo zao kwa sasa na tuweni makini kwa sasa.
Tupo pabaya na tunazidi kuelekea kubaya zaidi tene kwa speed kali kweli maana hakuna wa kuzuia.
 
Hiizi ni habari za kusikitisha sana, ninamuombea sana kwa Mungu ndugu yangu Kubenea, Mungu akuongoze na kukulinda na mafisadi wasio na huruma kwa Taifa, Wananchi wake, Serikali mpaka sasa Waandishi Wa habari, Saeed wembe uwe ni ule ule.

Otherwise:-

Unajua recently nilikuwa bungeni Dodoma na I had little nice chat na RO, well I was humbled na how well he was current na JF na some of us kama mimi na Mkulu Wangu Mwanakijiji, infact I was proud kwamba tunasikika huko juu na alinishauri sana kwamba tujaribu kuwa wakweli na nifikishe salam zake za heri back na niwe mkweli na niliyoyaona pale, Well Mkuu RO heshima mbele sana mkuu hasa kwa ustaraabu wako ulionionyesha kwamba it is okay kutofautiana kimawazo kuhusu muelekeo wa uongozi wa taifa, bila kukasirikiana wala visasi I was impressed mkuu, pia heshima zangu sa juu sana kwa Viongozi wengine niliobahatika ku-chat nao kama Dr. Slaa, Zitto, Lowassa, Mahanga, Nchimbi, Kajege, Mkullo, PM Pinda, CDF - Gen. Mwamunyange, Mwakyembe, Spika Sitta, Masha, Aunt Sophia, na Mh. Membe pamoja na wengineo wengi ambao walinifahmaisha kwamba they were well aware of JF na some of us na kwamba wako okay na most of Constructive Criticism from here, heshima na salute kwa all members hapa.

Kwa heri ya kuonana tena!


FMEs!
 
Hiizi ni habari za kusikitisha sana, ninamuombea sana kwa Mungu ndugu yangu Kubenea, Mungu akuongoze na kukulinda na mafisadi wasio na huruma kwa Taifa, Wananchi wake, Serikali mpaka sasa Waandishi Wa habari, Saeed wembe uwe ni ule ule.

Otherwise:-

Unajua recently nilikuwa bungeni Dodoma na I had little nice chat na RO, well I was humbled na how well he was current na JF na some of us kama mimi na Mkulu Wangu Mwanakijiji, infact I was proud kwamba tunasikika huko juu na alinishauri sana kwamba tujaribu kuwa wakweli na nifikishe salam zake za heri back na niwe mkweli na niliyoyaona pale, Well Mkuu RO heshima mbele sana mkuu hasa kwa ustaraabu wako ulionionyesha kwamba it is okay kutofautiana kimawazo kuhusu muelekeo wa uongozi wa taifa, bila kukasirikiana wala visasi I was impressed mkuu, pia heshima zangu sa juu sana kwa Viongozi wengine niliobahatika ku-chat nao kama Dr. Slaa, Zitto, Lowassa, Mahanga, Nchimbi, Kajege, Mkullo, PM Pinda, CDF - Gen. Mwamunyange, Mwakyembe, Spika Sitta, Masha, Aunt Sophia, na Mh. Membe pamoja na wengineo wengi ambao walinifahmaisha kwamba they were well aware of JF na some of us na kwamba wako okay na most of Constructive Criticism from here, heshima na salute kwa all members hapa.

Kwa heri ya kuonana tena!


FMEs!

Heshima mbele Mkuu..............usipotee sana tafadhali..................mchango wako hapa ni muhimu kama ulivyo-site hapo juu...........
 
hivi mbona hawawafuati akina manyerere jackton na vibaraka wegine wa habari corporation? ploeni vijana mliopewa bugudha.
 
Too bad.

Lakini inabidi tujipange na tutegemee mengi zaidi katika uchaguzi huu madamu kuna upinzani wa kweli dhidi ya CCM. CCM, in my view, are far more brutal than KANU was. Hatujawahi kuona unyama wao kwa kuwa walikuwa hawajapata upinzani wa maana. Kwa kuwa wamempata a real threat and real possibility that power could be sliding off their hands, tutawaona. Hawajazoea ushindani zaidi ya kutumia mabavu.

Tunachotakiwa kufanya kwa sasa ni kuelekeza nguvu zetu kwa wafanyakazi wa vyombo vyetu vya ulinzi na usalama kuwaelimisha kuwa nchi hii ni ya maana zaidi kuliko CCM na viongozi wake. Inabidi tuwahakikishie pia kwamba nchi itakuwepo bila kuwepo CCM na kwamba wanazo hizo kazi kwa sababu ya utaalimu wao na wala sio fadhila ya CCM, na kwa hivyo wataendelea kuwa nazo hata bila CCM kuwepo. Vyombo hivi vikielimishwa vikaelimika vitatenda haki. Hii ndio salama yetu.

Tunapolaani hili lililotokea kwa ndugu yetu Kubenea, inabidi sasa tufikirie mbele zaidi ili kuhakikisha kwamba hili jambo halitokei tena kwake au kwa mtu mwingine yeyote yule. Of course kupiga kelele za laana ni muhimu, lakini pengine lazima twende mbele zaidi. What is this mbele zaidi, that is where we need to put our heads together.
 
Usiogope kifo wewe ni shujaa wa nchi hii, na tunahitaji vijana kama wewe.mungu atakulinda
 
Back
Top Bottom