Invisible
Robot
- Feb 11, 2006
- 9,075
- 7,878
Usiku wa kuamkia leo tumepata taarifa za kuvamiwa eneo ambalo alikuwa akiishi Said Kubenea wa MwanaHalisi huku waliofanya uvamizi wakiwalazimisha vijana wa eneo hilo kusema alipo Kubenea.
Taarifa hizi zinadokeza kuwa pamoja na vijana hao kuwafahamisha kuwa Kubenea kahama takribani mwezi mmoja uliopita wavamizi hawakuacha kuwatesa vijana wa mtaa huo na kisha kutokomea kusikojulikana.
Pamoja na kuwa Said katoa taarifa hizi Polisi nao kuthibitisha kutokea kwa tukio hilo, sisi kama JamiiForums tunapinga kwa nguvu namna yoyote ile ya kujaribu kuwanyamazisha waandishi wa habari na vyombo vyao vya habari (si MwanaHalisi pekee) ndani ya nchi yetu. Tunalaani kitendo hiki kwa nguvu zote na kuliomba jeshi la polisi kufanya uchunguzi wa kina juu ya tukio hili ili ukweli ujulikane (ukizingatia kuwa wavamizi walienda kwa lengo la Kubenea na imethibitika).
Tunaamini jeshi letu halitosita kuchukua hatua pindi wahusika watakapobainika na hata kuweza kutoa taarifa juu ya nini walifuata na nani aliwatuma na kwanini.
Taarifa hizi zinadokeza kuwa pamoja na vijana hao kuwafahamisha kuwa Kubenea kahama takribani mwezi mmoja uliopita wavamizi hawakuacha kuwatesa vijana wa mtaa huo na kisha kutokomea kusikojulikana.
Pamoja na kuwa Said katoa taarifa hizi Polisi nao kuthibitisha kutokea kwa tukio hilo, sisi kama JamiiForums tunapinga kwa nguvu namna yoyote ile ya kujaribu kuwanyamazisha waandishi wa habari na vyombo vyao vya habari (si MwanaHalisi pekee) ndani ya nchi yetu. Tunalaani kitendo hiki kwa nguvu zote na kuliomba jeshi la polisi kufanya uchunguzi wa kina juu ya tukio hili ili ukweli ujulikane (ukizingatia kuwa wavamizi walienda kwa lengo la Kubenea na imethibitika).
Tunaamini jeshi letu halitosita kuchukua hatua pindi wahusika watakapobainika na hata kuweza kutoa taarifa juu ya nini walifuata na nani aliwatuma na kwanini.