Tunakwenda au tunarudi?

JENSENE

Member
Mar 7, 2011
52
6
Hivi karibuni tumeshuhudia mijadala mbalimbali ya bageti ikiendelea bungeni. kitu cha kushangaza wabunge wengi wameonekana wakiwasahau wapiga kura wao na kujita ktk kutetea maslahi yao. Wabunge wengi wa sisi emu wamekuwa wakitumia wingi wao/nguvu kupinga hoja muhim zenye manufaa kwa taifa na wananchi wa hali ya chini. Hii inaonesha ni jinsi gani watu tuliowachagua si kwa ajili yetu. Katika hali wazi kabisa tazama akina Mnyika, Tundu Lisu,Zitto wanavyopambana. Watz tuamke tupambanue hoja na si ushabiki tu tuangalie maisha yetu tunapelekwa wapi.
 
nchi haina mwenyewe, hata wewe kama una uwezo wa kuila usifanye ajizi - ikifikia point mwakilishi wa watu bungeni anatetea posho yake ya kukalia kiti bungeni wakati wapiga kura wake wanakufa hawana hata matibabu - think twice.
 
Wakati wa uchaguzi tuliwatahadharisha wananchi hatari ya kuwachagua wana ccm ambao wanawagawia pesa huko majimboni, kuwa kamwe hawataenda bungeni kuwatetea kwavile wametumia pesa zao kununua kura kutoka kwenu. Kwa maneno rahisi ya kibiashara ni kwamba "mlishamalizana" kwa kuwauzia kura zenu ambazo mliziona thamani yake ni doti 1 ya khanga na kapero. Wananchi hawana tena haki ya kuwalalamikia watu ambao walishamalizana nao, kwani walishafanya kosa ambalo kwalo wanapata maumivu, hadi jamaa warudishe fedha zao na faida juu. Hiyo ndo kanuni ya biashara. Maumivu yakizidi subiri sanduku jingine la kura 2015, pengine akili za wapiga kura wengi zitajua kosa walilolifanya kipindi hiki. Sipendi kabisa kusikia wananchi wakilalamikia jambo ambalo lilikuwa ndani ya uwezo wao!
 
elimu ya uraia ndiyo tatizo kuu, sipendi sana kuwatupia lawama wapiga kura kwa asilimia mia. Hili la elimu ya uraia, ufukara na umaskini uliokithiri wa baadhi ya koo vijijini ndiyo mtaji mku wa CCM.

Lazima tusaidiane kufikisha elimu hii vijijini, vinginevyo yatakuwa haya haya ifikapo 2015.
 
Back
Top Bottom