Mchekechoni
JF-Expert Member
- Apr 24, 2008
- 279
- 19
Kwa muda mrefu nimekuwa nafuatilia na kuchunguza kinachoendelea katika mitandao mbalimbali ya simu hapa nchini. Leo naona ni siku mwafaka kuweka bayana jinsi Vodacom inavyoibia wateja wake kama ifuatavyo: Leo asubuhi saa 10:48 salio langu lilikuwa shs.278.21 - saa 11:33 ni shs.278.17 - saa 12:29 ni shs.278.15 na saa 12:43 ni shs.278.13. Yaani salio linajipunguza lenyewe automatically bila ya kuitumia simu yako kwa rate ya shs.0.08 kila baada ya masaa mawili. Ndani ya masaa 24, tayari nakuwa nimeibiwa na Vodacom toka kwenye salio langu kiasi cha shs.0.96. Hivyo basi ukichukulia kwa uchache tu, kiasi cha wateja milioni mbili wa Vodacom ni kwamba tunaibiwa jumla ya shs.1,920,000/= ndani ya siku moja tu! Ukichukulia kwa mwaka mzima, wateja hao hao milioni mbili tunaibiwa jumla ya shs.702,720,000/=. To prove this; hakikisha salio lako kwenye laini yako ya Vodacom, kisha usipige simu wala kutuma sms ila angalia salio kila baada ya masaa mawili utaona kinachoendelea. Wanasheria tuungane kuwafikisha kortini Vodacom kwa wizi huu! Mitandao mingine (Airtel, Tigo, Zantel) hainyonyi wateja wake kwa mtindo wa aina hii!