Rev. Kishoka
JF-Expert Member
- Mar 7, 2006
- 4,526
- 1,529
Masatu,Mwakjj.
Ushauri tu, mara nyingi wageni wako hawa wanakuwa ni viongozi wakubwa serikali kutoka vyama vya upinzani. Tunafurahia kuwa na watu wa aina hii ktk mahojiano nao ktk kujua mustakbal wa nchi yetu.
Kumezuka mtindo wa baadhi ya wachangiaji kufurumusha kashfa kwa viongozi hawa na kuwaita majinaya kebehi, dharau, na kejeri. Nadhani hii sio nzuri na sio utamaduni wetu na nadhani pia itawafanya wengine waone kama kuja kwao hapa ndio kumefungulia milango ya matusi kwao.
Naomba nieleweka sisemi na wala sishauri kuwa wasibanwe kwa matendo yao na kama ni criticism basi ziwe ni constructive crticism sio mambo majina kama Kara-mavi, Kara-bangi, selfish katibu etc nadhani huk ni kupotoka.
Yawezekana kabisa wakawa sio wasafi lakini kitendo cha kubadili jina la kiongozi lisomeke ndivyo sivyo sidhani kama kunatusaidia sana hapa bali kama sio kutoshusha hadhi yetu na kuonekana ni genge la wahuni.
Ombi langu kwako ni jaribu kuwaomba wasikiliza wako wajiheshimu kwa hilo.
Naomba kuwasilisha
Inapofikia mahali kuwa wananchi wamechoshwa na kauli hewa zilizoandamana na uongozi wa sera za udhalimu, uhujumu, dhuluma, ufisadi na kichwa ngumu, basi ni matusi hutembea.
Keep up with your civility. Siye tumechoka kugeuza mashavu left to right while we continue to suffer!
Did you hear what happened in Mtwara yesterday? it is much better for us to call him Kala-Mavi than those who have now decided that enough is enough and dawa ni kuchoma moto nyumba zao.
Tumechoka kudhihakiwa na viongozi hawa hawa. Mikataba mibovu, dharau tele na kadhalika.
Tutawatukana, kisha tuwapige mawe na mwisho kuwachoma moto.
Revolution will never be televised, it will be live and just like a thief, it will arrive unexpectedely, unannounced!