Tunahitaji mfumo mpya wa kijasusi?

Kaka nimeona. Nadhani uko sawa. ukiangalia harakaharaka utagundua kigezo kikubwa ni hali ya usalama. kwa mfano ukiangalia Israel, Pakistan na India ambao ndio wanaongoza hali zao za usalama ni tete sana. Australia ambao wanashika namba 10 unaona kuwa wamejikita kwenye masilahi yao ya kiuchumi zaidi (na hasa ni sector ya madini). CIA wao wako kila mahala lakini usiri wao wa habari sio mzuri ingawa wanawezeshwa kuliko agency yoyote duniani. Swali la ziada, Hivi hii dhana ya kuwa na mpelelezi anayeongoza (kama inavyopenda kuwekwa kwenye sinema na vitabu vya hadithi) huwa ni ya kweli? kwa mfano james bond, willy Gamba, Joram kiango n.k je? ni kweli huwa kuna mpelelezi anayeongoza kati ya wenzake na kujichukulia umaarufu?
Mkuu hakuna mpepelezi anayeongoza kama akina Jack Baur na kina Wily Gamba, Joram Kiango n.k.
Ila kunakuwa na Unit flan ndani ya agencyambayo ndio inakuwa inategemewa sana lakini sio mtu individual.
 
Mimi nina swali kwa intelijens kabisa, ni kweli eti kuwa hizi harakati za Miamsho ya Kiislamu Zanzibar yenye nia ya kuvunja Muungano na kuunda Jamhuri ya Kiislamu, eti harakati zote zinafanyika Iran ili zanzibar pahala bila uchafu wa kimagharibi kama Utalii, Ulevi, nk, kweli?
 
Kama serikali haina mpango wa kuimarisha usalama wa nchi, na sisi tunaona kabisa usalama wetu uko mashakani suluhisho ni nini? tulalamikie nini ili wafanye nini? je? ni rahisi kiasi gani kutenganisha siasa na usama wa nchi?

Mkuu Mpingauonevu, maswali yako yameibu maswali mengi kichwan mwangu hasa juu ya uwezekano wa kuwa na utawala wa sheria/intelijensia isiyo na chembe ya siasa katika dunia yetu hii ya tatu hasa Tanganyika tulio fundishwa kuishi kindugu, kusaidiana na kuhurumiana, tuliofundishwa misemo na methali za kuvutia(zimwi likujualo halikuli likakwisha, heri shetani uliyemzoea kuliko malaika usiyemjua nk.). Itanipa shida kukuweka kwenye kitengo wewe nisiyekufaham usije ukaniharibia mipango yangu. Kama ina wezekana, inawezekanaje kufanya tofauti na matakwa ya aliyekuweka katika kitengo ikiwa sote twajua kuwa mkuu wa kitengo cha upekuzi/ujasusi/intelijensia (whatever you call it) hupointiwa? Aina ya demokrasia tuliyonayo sisi wa dunia ya3, pia inanipa shida kuamini kuwa hii kitu inawezekana kwa sasa hapa kwetu.
 
Wadau ivi hapa kwetu tz kuna kipaumbele cha kuwatumia watalaamu wetu hususani vijana kwa manufaa ya taifa la kesho kuweza kutumia teknolojia ya kwa manufaa ya taifa siyo tu kukaa na utamaduni wa zamaaaaaaaaani wa kusikiliza watu wanaongea nn? sawa hauwezi kuacha ila dunia imebadilika kila nyanja leo ujasusi wa wenzetu uko ktk uchumi na tekn zaidi sijui hawa UWT.....? ukienda ubalozi wa japan DSM watakwambia ni magari mangai yameingia $$$ ila upande wa pili sijui hata kama wana dalili yeyote ile
 
Mkuu Mpingauonevu, maswali yako yameibu maswali mengi kichwan mwangu hasa juu ya uwezekano wa kuwa na utawala wa sheria/intelijensia isiyo na chembe ya siasa katika dunia yetu hii ya tatu hasa Tanganyika tulio fundishwa kuishi kindugu, kusaidiana na kuhurumiana, tuliofundishwa misemo na methali za kuvutia(zimwi likujualo halikuli likakwisha, heri shetani uliyemzoea kuliko malaika usiyemjua nk.). Itanipa shida kukuweka kwenye kitengo wewe nisiyekufaham usije ukaniharibia mipango yangu. Kama ina wezekana, inawezekanaje kufanya tofauti na matakwa ya aliyekuweka katika kitengo ikiwa sote twajua kuwa mkuu wa kitengo cha upekuzi/ujasusi/intelijensia (whatever you call it) hupointiwa? Aina ya demokrasia tuliyonayo sisi wa dunia ya3, pia inanipa shida kuamini kuwa hii kitu inawezekana kwa sasa hapa kwetu.

hivi haiwezekani kitengo cha intelijensia kuwa kinajitegemea na ajira zikawa ni za kuomba? nasikia (sina uhakika) kwamba CIA ni kitengo (taasisi) kwa hiyo unapoomba kazi unatoa vielelezo vyote. Kwa nini na sisi kwetu isiwe hivyo ili tuondokane na huu usalama wa ndugu na tupate usalama wa taifa wa kikweli? je? hili la usalama wa taifa linajadilika kikatiba?

 
Nimezisoma bwana ishu siyo kiingereza nakijua sana tu..haya ni maneno ya Internet usije dhani hizi categories zimewekwa na taasisi fulani ya intelijensia ni interests za watu tu kufanya uchambuzi kama huo na kuweka kwenye internet, ndiyo maana kwenye chuo nilichosomea Masters ukiweka reference ya material kuwa umeipata kwenye net imekula kwako!

wapi? ulikosomea masters Rukwa? walikueleza reference za net hazifai?? inaonekana bado haukumuelewa mwalimu wako mkuu........muulize tena!!! wengine tunafundisha vyuo vikuu humu!
 
Huwezi kuimarisha ulinzi wakati watu wanaingia nchini kiholela ati kwa sababu tu ni member wa EAC. Subirini matokeo yanakuja very soon.

Ongezea..........Wanaingia kiholela na kuchukua passport yetu kama njugu vile............we are so lousy kwenye suala la immigration.........na tunadharaulika sana Kimataifa kwenye hili suala la immigration...............
 
mkuu ni utaratibu gani unaotumika kuwapata hao majasusi?

kuna kitengo cha wachapakazi hasa kiko jeshini.., kitengo cha ujasusi ambacho hadi sasa kiko free from politics ni CMI (central military intelligence)..., lakini upande wa foreign assets ndo wazuri sana wako bize kukusanya taarifa hatarishi dhidi ya nchi yenu hiyo...,

Hawa wamegawanyika..., kuna wanaofanya kazi kufatilia mienendo na tabia za maofisa na askari ndani ya vikosi hata nje,

kuna wakusanya habari za ndani ya nchi zenye maslahi na jeshi, mfano kuna watu kazi yao ni kusoma magazeti daily, magazeti ya ndani na hata ya majirani au kuangalia tv, au kushinda kwenye mitandao kama humu, pia kuna ambao kazi yao ni kunasa mawasiliano ya jirani zenu...,

na kuna foreign assets.., wanaishi na kukaa nje...., kuna wanaotumwa for a specific mission na kuna wanaokaa tu huko kukusanya taarifa yoyote ambayo ina maslahi na usalama wa nchi.., na wapo ambao ni infiltrated kwny majeshi jirani na serikali za jirani

hawa ndo wamebaki kuwa pillar ya nchi from outside threats

Ila ile cream ilokua trained russia, israel, cuba ndo inastaafu..., wamebaki wale mnaowafundisha pale mikumi
 
nimekuwa nafuatilia sana report zinazoachiliwa na CIA. Inaonesha CIA wanaijua dunia kuliko dunia inavyojijua. NIkaanza kufuatilia mashirika ya Kimarekani ya usalama - Police, FB!, secret service zao unakuja kujua kumbe mfumo wa ulaya unafanana.Eneo kubwa linalofanana ni kwamba mfumo wao wa usalama hauingiliwi na wanasiasa. Ikishafikia habari ya usalama ni wananchi na mali zao! Sasa sisi Tanzania mfumo wetu wa usalama ukoje? Je? ni shirika gani linashika usalama wa tanzania bila kuingiliwa na wanasiasa? halafu tunaweza kweli kuchunguza nchi zingine kwa manufaa yetu?

TISS yetu ya TZ inafanya kazi kwa maslahi ya:
1. Wawekezaji walioko na wanaotaka kuiba mali za watanzania
2. Wanasiasa wanaofanya kazi kwa maslahi yao.
3. CCM na Wezi wengine nchi hii, Ndiyo Maana kina Kombe waliuawa
 
Mbona wamerakani walienda kumchukua Osama Bin Laden na kumuua bila ya wao kujua??? Je CIA taarifa walizipata wapi? Hebu jifunze kuunganisha dots bana!

UNA UHAKIKA GANI KUWA HAWAKUJUA MKUU! Wao ndo walikuwa wanamlea na ndo wao walowapatia wamarekani kwa makubaliano kuwa wahakikishe anauwawa.
 
wapi? ulikosomea masters Rukwa? walikueleza reference za net hazifai?? inaonekana bado haukumuelewa mwalimu wako mkuu........muulize tena!!! wengine tunafundisha vyuo vikuu humu!

Rukwa? Nina MBA kaangalie chuo cha 4 africa kwa ubora kwa MBA na cha kwanza Tanzania ndiko nilikosomea mimi....
 
mkuu ni utaratibu gani unaotumika kuwapata hao majasusi?

Big up man. Kinachoendelea sasa ni kwamba vijana wengi wanaohudumia idara yetu nyeti wanapoteza maadili kidogo but they are doing good job. Watu wanalaumu tu lakini lazima wajue bila hiki kikosi tusingekua tuonaongea hapa kwani uslama wetu usikingekuwepo kutokana na maadui wa nje na ndani ya nchi yetu. Wakati wa Mwalimu na mpaka sasa jukumu la usalama wa nchi yetu ni wetu sote na si kusema eti idara ya usalama haifanyi kazi.

Ukiona usalama wanchi unayumba basi ujue sisi wananchi(raia) hatufanyi kazi ya kulinda nchi yetu. Usama wa awali juu ya maadui zetu ni wewe mwananchi, ukiona mtu anaihujumu nchi yetu na wewe hutoi taarifa kwa vyombo vya usalama, then wewe mwananchi umehusika kuingamiza nchi yetu japo utailaumu idara husika.

Ushauri wangu wananchi wezangu sote tuilinde nchi yetu kwa kushirikiana na vyombo husika. Sote tupo kwenye meli moja waliochini wakiamua kutoboa meli wasifikirie ikizama utawalaumu watoboaji, maana yake ni kwamba ukiona mtu anatishia usalama wa raia mwenzako au wa nchi yetu aidha kwa tamaa zake au kutokujua na usitoe taarifa basi jua hata wewe umehusika kuliangamiza taifa. Tuwe wazalendo wa nchi yetu, tuache kulaumiana.
Mungu ibariki Tanzania.
 
wapi? ulikosomea masters Rukwa? walikueleza reference za net hazifai?? inaonekana bado haukumuelewa mwalimu wako mkuu........muulize tena!!! wengine tunafundisha vyuo vikuu humu!

Hakika hakumwelewa. Hata mimi ukiniletea references za google.com au wikipedia.com,nitakutimulia mbali.
 
mimi nina swali kwa intelijens kabisa, ni kweli eti kuwa hizi harakati za miamsho ya kiislamu zanzibar yenye nia ya kuvunja muungano na kuunda jamhuri ya kiislamu, eti harakati zote zinafanyika iran ili zanzibar pahala bila uchafu wa kimagharibi kama utalii, ulevi, nk, kweli?
hii iko conc sana hebu tuone wadau wanasemaje?japo naweza amini kwani niiliwahi kuwa kule kipindi cha uchaguzi walisema hawana nia na muungano kwani hata nyanya walikua wanapata za kopo toka arabuni.
 
Back
Top Bottom