Tunahitaji chama kipya?

Najiuliza kama kuna watu wameanza kuwa kama mimi; vyama vyote vya kisiasa vilivyopo nchini haviwezi kutupatia kile tunachohitaji kama taifa. Siyo CCM, Chadema, CUF au TLP ambacho kilivyo sasa kinaweza kuwa tumaini la Watanzania. Je kuanzisha chama kingine ambacho kitatoka kwa wananchi na chenye ajenda ya mabadiliko ya kweli na kikiongozwa na watu wenye mwelekeo wa mabadiliko na wasiogopa political confrontation na ambacho hakitasita kufanya what is necessary to restore law and order and a constitutional rule kitaweza kuwa na nafasi.

Thanx Mzee, lakini hicho chama kipya sijui kitatoka Mbinguni? Hata hivyo vyama vilivyopo vinafanya kazi zao chini ya KATIBA ya CCM, maana yake mpaka CCM iridhie hicho chama kipya ambacho kitakuwa tishio kwa CCM yenyewe. Kwa maana hiyo ni kujitia kitanzi CCM. Katu kwa mwenendo huu hakuna chama kitakachofurukuta, hata kama kitakua na nguvu kama simba. Katiba iliweka kakipengele ya vyama vingi ili kumfurahisha Mwalimu JKN amalize maisha yake ya mwisho duniani kwa furaha, lakini hakuna katiba ya vyama vingi na kila chama kinachoonekana kukitingisha CCM wanapelekwa machekecheo huko wakachekeche maeneo nyeti kudistabilize strategies.

Tyson wa Las Vegas atagombanaje na Bwana Boramaisha wa Nyarugusu? Au Bill Gate agombane na Machinga? Timu ya kijiji cha msichoke haiwezi kupambana na Manchester United, bado ikang'ang'aniwa kwamba ni fair play.

Kama kweli tunataka mabadiliko yaliyokubaliwa kwa dhati, kila kitu kianze upya. Katiba Mpya, Mali za CCM ambazo zilikuwa za watu wote zamani ziende serikalini au kwa wananchi na kila chama kianze from zero level, halafu kila mmoja wao atueleze kwa nini yeye tumwamini zaidi ya mwenziwe.

Leka
 
Chama kipya kama ni kwa 2010, its too little too late unless chama hicho kipya kitoke within CCM ili litimie lile neno la Baba wa Taifa " upinzani wa kweli, utatoka CCM Tuu!".
Huyu Mzee ni kama Masiya, kaona mbali na kwa sasa huo muda haujafika ila amini nawaambieni, kuna siku utafika.

Tatizo la Tanzania siyo hitaji la vyama, hoja ya Mwanakijiji ni nzuri tatizo ni too idealistic na sio reality, hivyo inaishia kubakia kama utopia tuu. Realistic ya hitaji la kitaifa inaonekana kwenye battle ground,(chaguzi), sio kwenye laptop au PC. Tatizo haswa la Watanzania ni "Awareness". Nimeshuhudia chaguzi ndogo za Tarime, Mbeya Vijijini, Busanda na Biharamulo, watu wanaichagua CCM sio kwa sababu wanaipenda, ama wanaikubali, wanaichagua CCM, kwa sababu hawaelewi maana halisi ya uchaguzi wa vyama vingi, kwao chama ni CCM tuu, hii iko kwenye mind set. Mabadiliko ya kweli ni kuibadili hii mind set kwanza, na ikibadilika, mengine yote yatafuatia.

Kama ya Nyerere ni ya kweli, natoa wito, Mwanakijiji, Zitto, Mbowe, Dr. Slaa, Lipumba, Mkandara, etc, etc jiungeni CCM ili mpigane from within, mlete mabadiliko ya kifikra from within, awareness ikifika kwa wote, mjikate pande la haja haswaa ambalo mtaondoka nalo na wapiganaji wenu wote na damu changa za vijana kama kina Mnauye, Januari etc wenye mwelekeo wa matumaini, muunde hicho chama kipya na Watanzania watawaamini, CUF, Chadema na vyama vingine vya upinzania vitajifia natural death kutokana na wanachama wao wote wasiopenda maroroso yaliyopo, watavikimbia na kujiunga na chama kipya cha matumaini, and you never know, hata wale watu makini kama kina Shivji, etc, wanaweza ingia kwenye siasa, Watanzania watawakabidhi nchi, mtashika dola na ndio utakuwa mwanzo wa siasa za upinzani wa kweli kwa CCM kuwa ni chama cha upinzani.

Vinginevyo tukiendelea hivi tulivyo na upinzani hivi ulivyo....

CCM ITATAWALA MILELE!.
 
Mkuu MMKj,
Naona kama kuanzisha chama kipya sio solution kwasababu mindset za watu bado zimegubikwa na matatizo ya aina ileile ambayo tunayaona kwenye vyama vilivyopo. Kwa bahati mbaya ma opportunist ndo wamekuwa wanatamba kwenye hivi vyama kwa kudandia kila kinachoonekana kinalipa kwao. Naona sasa ingekuwa busara kuwa na independents ambao wanasimama kama wao bila kuburuzwa na matakwa ya vyama vya siasa. Kama hawa idadi yao itakuwa kubwa na agenda ya mabadiliko ikawa kweli ni ya moto, naamini hata vyama vitakuwa na mitazamo tofauti. Hivi vyama vimekuwa kama nyumba za baadhi ya watu na wanaviendesha kama wanavyotaka
 
nahisi kukata Tamaa na siasa nzima ya nchi yetu ...2010 sijaona wa kumpigia kura kabisa ..sijui nifanyeje ???
 
watanzania wenyewe tuna akili za kifisadi naweza kusema.
chukua mfano mdogo tu.....watu wenye mshahara wa chini ya milioni moja kwa mwezi( ukichanganya mshahara wa baba na mama), wanapeleka watoto wawili shule za primary watoto zenye kulipiwa zaidi ya milioni moja kwa mwaka kwa kila mtoto.
hapa kama wazee hawajawa mafisadi, hawawezi kutimiza maihati yao

wazee wanajua hilo na wanalifanya kwa kujua kuwa kila mwezi atafanya ufisadi fulani maisha yende.
kwa utamaduni wa aina hii, hata kije chama gani, hakuna mabadiliko
 
Tuanze kuimarisha vyama vya WAFANYAKAZI. Wafanyakazi wa Nchi hii ndio wanaoweza kuleta MABADILIKO tunayoyataka. Tumewaacha wanahangaika wenyewe pamoja na kwamba wao ndio vyanzo muhimu vya taarifa nyeti za ufisadi. Badala yake wameamua kujiunga na mafisadi angalau waambulie hata makombo tu.
Kundi jingine ambalo linaweza kuleta mabadiliko ni WANAFUNZI na WANAVYUO. Nao tumewaacha wahangaike kivyao pamoja na kwamba ni wanetu wenyewe.
 
Kabla ya kuanzisha chama kipya, kama kinataka kuwa cha maana, inabidi waanzilishi wajiulize maswali yafuatayo.

1. Kuna haja ya chama kipya?
2. Vyama vilivyopo haviwezi kukidhi mahitaji?
3. Kuna tofauti gani ya kimsingi kati ya vyama vilivyopo na hiki kipya?
4. Ni kwa vipi chama hiki kipya kitajizuia kurudia makosa ya vyama vilivyopo?
5. Chama hiki kipya kitachangia nini kipya?
 
Watanzania hawawezi kubadilika fikra kwani fikra walizonazo zinawafaa katika mazingira haya ya kifisadi.

Nimejaribu kuamsha mapambano ya kifikra lakini matokeo yake mgongano unaoendelea ni wa kibinafsi zaidi kuliko wa kifikra. Karibu wanasiasa wetu wote wana fikra zinazofanana!

kwanza nani atatokea kuwa Obama wetu!
Asili ya matatizo na suluhu yake imo ndani ya CCM. Vyama vyote, kama ulivyoeleza mwanzo vina matatizo lakini kimsingi, ukiyachunguza matatizo yanayokana na kutokuwepo kwa itikadi zinazoeleweka ambazo vyama hicyo vinazisimamia.

Tangu kufa kwa Ujamaa, haieleweki CCM inafuaa itikadi gani. Wenyewe wanaweza kubabaisha kuelezea wanafuata itikadi gani, lakini ukiangalia hicho qwanaxchoamini kwua ni itikadi, si itijadi haswa.

Kama CCM ingekuwa na itikadi inayoeleweka, ingekuwa rahisi sana kuanzisha chama kingine kinachotofautiana na CCM kiitikadi kwani huo ndio msingi wa vyama vingi. Leo hii, vyama vilivyopo (nje ya CCM) navyo havijulikani hasa itikadi yake ni nini, navyo vimekuwa kama CCM. Hili linaweza kuwa tatizo la vyama hivyo vyenyewe au tatizo lililotokana na kukosekana kwa itikadi inayoeleweka ndani ya CCM hivyo nao wakashindwa kutengeneza itikadi mbadala.

Lakini, kama watatokea watu wenye kuelewa kwa undani tatizo hili, wanaweza kuangalia hali halisi na kuja na chama mbadala ambacho kitajikita katika itikadi ya aina fulani na kutokengeuka na kuanza kufanya siasa hizi tulizozizoea na makundi na ubinafsi.

Kama tunataka kuwa na chama imara mbadala, kijikite kwenye itikadi
 
Chama kipya kama ni kwa 2010, its too little too late....
Pasco, nadhani ni vibaya sana kuwa na mawazo kama haya, lengo lisiwe 2010, lengo liwe ni kuwakomboa watanzania kutokana na haya yanayowasibu hivi sasa
 
Kuanzisha chama kipya inawezekana, lakini kinaweza kisilete mabadiliko yoyote, badala yake kikawa na sera kama za vyama vilivyopo na hapo tutawakatisha tamaa zaidi raia.
 
Najiuliza kama kuna watu wameanza kuwa kama mimi; vyama vyote vya kisiasa vilivyopo nchini haviwezi kutupatia kile tunachohitaji kama taifa. Siyo CCM, CHADEMA, CUF au TLP ambacho kilivyo sasa kinaweza kuwa tumaini la Watanzania. Je kuanzisha chama kingine ambacho kitatoka kwa wananchi na chenye ajenda ya mabadiliko ya kweli na kikiongozwa na watu wenye mwelekeo wa mabadiliko na wasiogopa political confrontation na ambacho hakitasita kufanya what is necessary to restore law and order and a constitutional rule kitaweza kuwa na nafasi.

Chama ambacho mrengo wake itakuwa ni kuhakikisha kuwa hakuna kuremberiana macho na mafisadi tena wala kuufafanua ufisadi bali kuushughulikia moja kwa moja.

Chama ambacho kitalenga kuleta mabadiliko ya kimfumo na kimuundo wa serikali yetu ndani ya miaka mitano ya kuingia madarakani kikibeba ajenda ya mabadiliko ya kweli (kikatiba, kisiasa, na kiutendaji) huku kikiwashughulikia kama simba mkali wale wote ambao wamelifikisha taifa letu hapa ikiwemo kutaifisha mali zao, kuwasweka jela na wale ambao ni vigogo wa ufisadi "kunyongwa" kama wanavyofanya huko China!

Chama ambacho hakitawabembeleza wawekezaji kama wakwe zetu!

Au ndiyo tubanane mumu kwa mumu huku tukiulizana "kajamba nani'!

MKJJ,
Unaloliongea inaonesha namna gani watanzania tumechoka, kwamba tunakwenda kama vile hatuna mwelekeo. Ila kama tukianzisha chama, na sasa vipo zaidi ya 17, sidhani kama itakuwa ni solution ya matatizo. Maana hata hivyo kumi na saba vilianzishwa kwa agenda hiyo hiyo ya mabadiliko. Tutajuaje kama hicho kipya hakitalewa na madaraka? Nadhani the best option ni wanaharakati wa Tanzania, mimi na wewe, kupiti vyama vilivyopo vya siasa, kuamua kujenga vijana wapya wenye moyo wa uzalendo, hasira ya mafanikio na roho ya mabadiliko. Kama hili likifanyika kwa dhati, kukawa kuna true and meaningful investment in human resources in political parties, with etermination, goals and true commitment, I beleive we can make! Nataka kuamini hata ushindi wa Democrat Marekani, pamoja na kwamba chama kilikuwa na sera nzuri, mchamgo binafsi wa uwezo wa Ubama ulichangia.
 
Pasco, nadhani ni vibaya sana kuwa na mawazo kama haya, lengo lisiwe 2010, lengo liwe ni kuwakomboa watanzania kutokana na haya yanayowasibu hivi sasa

Mimi sioni kwanini tuanze kuona vyama vyetu vya upinza havifai? ambao hawafai ni sisi wenyewe ambao hatuwezi kuleta mageuzi. Chukulia uchaguzi wa jana CCM imewekeza pesa nyingi mno kwenye huo uchaguzi angalia kampeni zao ni pesa tupu ndo ilikuwa inatembea utadhani uchaguzi niwa ubunge na udiwani.

Hivi vyama vya siasa vinahita pesa navyenyewe kusudi vishindane na hawa. Juzi nilienda kwa mgombea nikamwambia nipe basi tshirt na bendera nikufanyie kampeni akanijibu hana hata ile ya kuuza nikanununue.
Cha muhimu ni kuwawezesha Upinzani nawenyewe wawe na pesa kwenye chaguzi, mimi nimeona mwenyewe ni aibu sana hata kusema we fikiria mgombea hana hata hiyo baiskeli atafanyaje kampeni mbele ya mafisadi.
 
Tatizo ni vyama yaliyotokea uchaguzi wa CUF kwa Professor Saffari kukashifiwa au Chadema Zitto Kabwe kuzuiliwa nani anaweza kuviamini vyama hivi kienyeji tu?TLP uchaguzi wao walitaka kugombea wakavuliwa uanachama.

Kibanda alikuwa mkali kama Mbogo sababu kubwa ni mkate wa Tajiri yake kuhatarishwa.uchaguzi wa vijana umeahirishwa hadi miezi sita ijayo sababu Mgombea wa kaskazini alikosa nafasi.

nani Mwenye akili timamu anaweza kujiunga huko Chadema kwenye mazingira kama haya? Zitto ana miaka 16 ndani ya Chadema haaminiwi.jee Mkandara anaweza kuaminiwa?

Hivi karibuni imeletwa Taarifa kuwa Maaskofu wako nyuma ya DR.Slaa /Chadema ambaye alikuwa katibu mkuu wao kwa miongo kadhaa nani atajiunga kwenye chama ambacho hakina maaamuzi ya kikatiba zaidi ya vizee vinne tu?

Nadhani uchaguzi wa chadema ulikwisha salama na kambi zote mbili zilivunjwa siku hiyo kwa ajili ya kuleta mshikamano kwenye chama. Nadhani tusikae tuna quote mambo ya nyuma kila chama kina matatizo yake.
 
Hii topic ni nzuri.
mjj amelenga pazuri.
kuunda chama kipya itatuchukua muda mrefu kutarua matatizo ya nchii hii. tuwasaidie hawa viongozi wa vyama vilivyopo katika uteuzi mzuri wa kiongozi wa kitaifa (Rais) ambaye ana sifa zote ambazo sisi wananchi tunazi afiki. na ana maadili mema ya kiungozi na hasa mkali kwa tukio lolote linalokwenda kinyume na matakwa ya wananchi (adhabu iwepo pale pale kwa mtuhumu huyu). naamini candidates hao wapo. support ni muhimu sana baada ya kupatikana mtu huyu. natuanze kumfikiri sasa. Mimi nitaanza na dr slaa sisna mrengo wowote wa kichama. kama kuna mtu wa kunikosoa na anikosoe sasa.
 
Mkuu MJJ mawazo yako ni sahihi kabisa na kila mtanzania anayeipenda nchi naamini ameshajiuliza kuhusu hilo. Kuundwa kwa vyama vingi Tanzania kulitokea wakati ambao wananchi hawakua tayari au hawakuandaliwa vyakutosha. Na hii ilifanyika kwa makusudi na chama tawala CCM. Baadhi ya hivi vyama vilivyopo wengi tumeshahisi kuwa ni ofisi ndogo za CCM.
Nakubalina pia na mwandishi/mchangiaji aliyeshauri kuwa ni vyema tukaanza upya CCM irudishe mali zote ambazo ilikuwa nazo kabla ya vyama vingi ili tuanze upya na katiba ibadilishwe iwe inakidhi mahitaji na mazingira halisi ya kidemokrasia.
Wakati nikichangia ile mada ya wapiganaji wabakie CCM au wasibakie niligusia haja ya kuundwa kwa chama kipya. Ambacho kitaweza kukata kiu iliyopo ya kisiasa nchini, lakini inabidi wapiganaji wabakie CCM hadi hapo itakapoeleweka CCM inamuelekeo gani. Kama inaamua kukumbatia mafisadi na haitaki kubadilika ili kujibu malalamiko ya wananchi basi itakuwepo haja ya chama kipya.
Lakini wapo walioshauri pia kuwa hakuna haja kuongeza vyama bali muhimu zaidi ni kuviimarisha vilivyopo. Hili linahitaji utafiti mkubwa sawasawa na itakavyo hitajika kabla ya kuamua kuunda chama kipya.
 
Hii topic ni nzuri.
mjj amelenga pazuri.
kuunda chama kipya itatuchukua muda mrefu kutarua matatizo ya nchii hii. tuwasaidie hawa viongozi wa vyama vilivyopo katika uteuzi mzuri wa kiongozi wa kitaifa (Rais) ambaye ana sifa zote ambazo sisi wananchi tunazi afiki. na ana maadili mema ya kiungozi na hasa mkali kwa tukio lolote linalokwenda kinyume na matakwa ya wananchi (adhabu iwepo pale pale kwa mtuhumu huyu). naamini candidates hao wapo. support ni muhimu sana baada ya kupatikana mtu huyu. natuanze kumfikiri sasa. Mimi nitaanza na dr slaa sisna mrengo wowote wa kichama. kama kuna mtu wa kunikosoa na anikosoe sasa.
mmmhhh Dr slaa tunamuhitaji bungeni, urais hawezi kumshinda JK, vijijini hawajui ufisadi ni nini, na hiyo ndo silaha kubwa ya Dr slaa mpaka sasa.
Pili tatizo si kuwa na kiongozi mzuri atakaegombea urais, chamuhim ni kuwa na team nzuri [chama], ambacho kimeweka vichwa vingi si kwa mfano CUF ukitoa Lipumba na akina safari then chama kimeisha. Chama hakitakiwi kuwa na watu 5 u 1 kinatakiwa kuwa na watu wengi ambao ni DR slaaz.
 
Mwalimu alitoa nyasia miwili kuwa upinzani wa kweli utatoka CCM na kuwa wapinzania wapiganie ubunge kwanza,waachane na urais.Ukisahkuwa na wabunge wengi ndio uende kwenye Urais.Vyama vyetu vilivyopo vinang'ang'ania kugombea urais hata leo.

Logic ni kuwa wengi bungeni wa upinzani tupate katiba mpya na nzuri.Vinginevyo CCM haitoki na itajiimarisha zaidi kukaa mdarakani kwa kutumia pesa.
 
Mwalimu alitoa nyasia miwili kuwa upinzani wa kweli utatoka CCM na kuwa wapinzani wapiganie ubunge kwanza,waachane na urais.Ukishakuwa na wabunge wengi ndio uende kwenye Urais.Vyama vyetu vilivyopo vinang'ang'ania kugombea urais hata leo.

Logic ni kuwa wengi bungeni wa upinzani tupate katiba mpya na nzuri.Vinginevyo CCM haitoki na itajiimarisha zaidi kukaa mdarakani kwa kutumia pesa.
 
Najiuliza kama kuna watu wameanza kuwa kama mimi; vyama vyote vya kisiasa vilivyopo nchini haviwezi kutupatia kile tunachohitaji kama taifa. Siyo CCM, CHADEMA, CUF au TLP ambacho kilivyo sasa kinaweza kuwa tumaini la Watanzania. Je kuanzisha chama kingine ambacho kitatoka kwa wananchi na chenye ajenda ya mabadiliko ya kweli na kikiongozwa na watu wenye mwelekeo wa mabadiliko na wasiogopa political confrontation na ambacho hakitasita kufanya what is necessary to restore law and order and a constitutional rule kitaweza kuwa na nafasi.

Chama ambacho mrengo wake itakuwa ni kuhakikisha kuwa hakuna kuremberiana macho na mafisadi tena wala kuufafanua ufisadi bali kuushughulikia moja kwa moja.

Chama ambacho kitalenga kuleta mabadiliko ya kimfumo na kimuundo wa serikali yetu ndani ya miaka mitano ya kuingia madarakani kikibeba ajenda ya mabadiliko ya kweli (kikatiba, kisiasa, na kiutendaji) huku kikiwashughulikia kama simba mkali wale wote ambao wamelifikisha taifa letu hapa ikiwemo kutaifisha mali zao, kuwasweka jela na wale ambao ni vigogo wa ufisadi "kunyongwa" kama wanavyofanya huko China!

Chama ambacho hakitawabembeleza wawekezaji kama wakwe zetu!

Au ndiyo tubanane mumu kwa mumu huku tukiulizana "kajamba nani'!

tatizo la hivi vyama vya upinzani vinakatisha tamaa kwa sababu hizi tu hayo maadili uliyoyatoa amna ata mmoja anae yapigia debe moja kwa moja. sasa iwapo mtu unaona matatizo yenyewe alafu hata hawa yagusii hata hao walio bungeni ndio unapo jiuliza kuna upinzani kweli?
 
Back
Top Bottom