tunaelekea kizazi kinachokuja kitakuwaje

Chauro

JF-Expert Member
Aug 20, 2010
2,968
1,475
wanajamvi kuna jambo limekuwa likisumbua akili yangu muda wote hasa nikitizama watoto tuliozaa huwa nawaza mambo mengi sana.nakumbuka hapo nyuma tulipokuwa tunakua wengi watakuwa mashahidi kila mtu mzima alichukua jukumu la kulea mtoto wa mwenzake bila kuangalia ni wa nani leo hii ambapo muda mwingi hatupo majumbani ukikuta mwanao kachapwa na jirani au kakaripiwa unaanza kukuna mengine mengi naamini mtayaweka humu tusisahau hata kama utawalea kwa maadili gani watoto wako kama watazungukwa na uchafu kila mahali itakupa wakati mgumu sana kwenye malezi tupende watoto wa wenzetu na tuwatazame kwa jicho lile lile tunalowapa watoto wetu naamini tutatengeneza kizazi bora na sisi sio kuwa maangamizi wa malaika hawa wa malai
 
mmmhhh yaani ni kweli kabisa uliyosema hapo juu..
lakini yanini ujitafutie balaa.. kwa kumgusa au kumkemea mtoto wa mtu...
kwanza huyo mtoto atakutukana na mama akitoka huko ndani ndo yatakuishia shingoni....
siku hizi ni kila mtu na chake...
 
Ndo maana Wazee wanatongoza mabinti (watoto) wa Wazee wenzake na kuwamega
Hakuna aibu hata kidogo:A S-alert1:
 
subhana llah,,,,,lakini nahisi yatakuwa yakitendeka hayo kwa ajili binaadam sasa hivi tumetokwa sana na imani wallah!!!!! ya rabb tunusuru sisi na unusuru vizazi vyetu ya allah???
Ndo maana Wazee wanatongoza mabinti (watoto) wa Wazee wenzake na kuwamega
Hakuna aibu hata kidogo:A S-alert1:
 
Lakini tusisahau maisha yetu ya sasa muda mwingi tunakuwa mbali na familia tusipokubali watoto wetu waonywe na hawa tunawaachia tunajenga au kubomoa

mmmhhh yaani ni kweli kabisa uliyosema hapo juu..
lakini yanini ujitafutie balaa.. kwa kumgusa au kumkemea mtoto wa mtu...
kwanza huyo mtoto atakutukana na mama akitoka huko ndani ndo yatakuishia shingoni....
siku hizi ni kila mtu na chake...
 
Ukitaka kesi gusa mtoto wa mtu sasa hivi uone kitakachokupata hata kumwambia wee acha kuchezea mchanga au maji machafu ni issue utavaliwa kibwebwe na mama yake mpaka utashangaa
 
jamani Dena ndo hicho nachosikitika unajua hata mimi na watoto unapokuta mzazi mpaka mwalimu wa mtoto hutaki amkemee mwanao tunategemea nini kutoka kwa watoto hawa

Ukitaka kesi gusa mtoto wa mtu sasa hivi uone kitakachokupata hata kumwambia wee acha kuchezea mchanga au maji machafu ni issue utavaliwa kibwebwe na mama yake mpaka utashangaa
 
jamani Dena ndo hicho nachosikitika unajua hata mimi na watoto unapokuta mzazi mpaka mwalimu wa mtoto hutaki amkemee mwanao tunategemea nini kutoka kwa watoto hawa

Tena Chauro huko shuleni mie nilishangaa sana siku moja nilikwenda kulipa ada ya mtoto wangu nikakuta mtoto kachapwa sijui alifanya kosa gani sikuuliza lakini huyo mzazi alivyokuwa anaongea laahhhh nilishindwa hata sijui alikuwaje maana anaonekana mtu na heshima zake lakini maneno aliyokuwa anatoa mie hoi nasikia baadae alimhamisha mwanae shule ile kampeleka St....... badala ya ile nyingine usimguse kabisa mtoto wa mtu kipindi hiki ni kujitafutia matatizo
 
mi sijui lakini mimi nalitazama kama tatizo kubwa sana kwenye familia zetu maana malezi yamekuwa magumu kuliko tutahangaika sana kutafuta pesa na mali nyingi lakini kama tutakuwa na familia mbovu ni kazi bure na yote kwangu nahesabu kama ni ubatili mtupu upewe mali na amani mali bila amani ni kifo
 
wanajamvi kuna jambo limekuwa likisumbua akili yangu muda wote hasa nikitizama watoto tuliozaa huwa nawaza mambo mengi sana.nakumbuka hapo nyuma tulipokuwa tunakua wengi watakuwa mashahidi kila mtu mzima alichukua jukumu la kulea mtoto wa mwenzake bila kuangalia ni wa nani leo hii ambapo muda mwingi hatupo majumbani ukikuta mwanao kachapwa na jirani au kakaripiwa unaanza kukuna mengine mengi naamini mtayaweka humu tusisahau hata kama utawalea kwa maadili gani watoto wako kama watazungukwa na uchafu kila mahali itakupa wakati mgumu sana kwenye malezi tupende watoto wa wenzetu na tuwatazame kwa jicho lile lile tunalowapa watoto wetu naamini tutatengeneza kizazi bora na sisi sio kuwa maangamizi wa malaika hawa wa malai

"AN INDIVIDUAL IS THE BEST JUDGE OF HIS OWN INTEREST"( GEREMY BENTHAM) haya mambo ya kumparamia mtoto wa watu na kumkanya jamani kwa dunia ya leo ambapo maisha na utaratibu wa mtu kuishi yeye na kizazi chake ni mali yake binafsi hauwezekani.
Enzi za zamani wajibu (responsibility) wa mtu ndio uliokuwa unatawala kuliko haki ya mtu mwingine, na ndio maana jirani kukanya mtoto wa mwenzie alijua kuwa anatimiza wajibu wake kama mzazi na mtoto hakuwa na naki ya kuibishia adhabu hiyo, leo neno haki(right) limepiku wajibu, kumbuka leo hii suala la kumuadhib mtoto ni haki ya mzazi wake, wewe ni kuripoti tu juu ya kosa la mtoto kwa mzazi husika, huna haki japo unalimited responsibility juu ya mtoto wa mwenzio, sasa tunaishi kiubinafsi zaid(individualism) tumeyakubali mawazo ya Bentham na ndiyo yanatukeketa
 
nafikiri hujanielewa sio lazima kumuadhibu huyu mtoto hata mtu mzima anapotoa report kwako kama mzazi huwa tunarespond vip hata hawa walimu basi tunaokabidhi watoto wetu nao waogope kuwakanya sababu ya utandawazi unaongelea tena kuparamia ivi kweli kumkanya mtoto ni kumparamia sisi ni wazazi wa aina gani ndo maana sishangai pale tunaposhabikia mambo yanayobomoa badala ya kujenga


"AN INDIVIDUAL IS THE BEST JUDGE OF HIS OWN INTEREST"( GEREMY BENTHAM) haya mambo ya kumparamia mtoto wa watu na kumkanya jamani kwa dunia ya leo ambapo maisha na utaratibu wa mtu kuishi yeye na kizazi chake ni mali yake binafsi hauwezekani.
Enzi za zamani wajibu (responsibility) wa mtu ndio uliokuwa unatawala kuliko haki ya mtu mwingine, na ndio maana jirani kukanya mtoto wa mwenzie alijua kuwa anatimiza wajibu wake kama mzazi na mtoto hakuwa na naki ya kuibishia adhabu hiyo, leo neno haki(right) limepiku wajibu, kumbuka leo hii suala la kumuadhib mtoto ni haki ya mzazi wake, wewe ni kuripoti tu juu ya kosa la mtoto kwa mzazi husika, huna haki japo unalimited responsibility juu ya mtoto wa mwenzio, sasa tunaishi kiubinafsi zaid(individualism) tumeyakubali mawazo ya Bentham na ndiyo yanatukeketa
 
nimeweka tu watu tujadili kuna mambo tunapuuzia lakini kwakweli yatatumiza sisi wenyewe sijui kwanini tunafumbia macho mambo ya msingi kabisa


Kuwa mpole tu mwanakwetu hiyo ndo dunia ya tekinolojia ilivyo kwa sasa
 
Lakini tusisahau maisha yetu ya sasa muda mwingi tunakuwa mbali na familia tusipokubali watoto wetu waonywe na hawa tunawaachia tunajenga au kubomoa

chauro bibie nakubaliana nawe watoto wanahitaji maadili kutoka kwa watu mbali mbali lakini mmmhhhh
we watu wazima wenyewe hawana heshimma kabisa sasa hivi..
ndo maana nikasema kila mtu na chake wazazi ndo wanaotakiwa kumfundisha mwanao maadili mema..
sanasana na familly members pamoja na walimu.... Dunia hii imesha badilika Chauro huwezi kumuani kila mtu..

na kingine labda we unapoishi ni sehemu yenye amani na ambapo watu bado wana maadili na heshima ......
ningependa kusema kama ungekuwa unaishi ninapoishi huku ndo story nyingine kabisa....
mtoto anakula darasani halafu akimaliza analala kwenye dawati ....
mwalimu akimwamsha ni balaa tupu..iliwahi kutokea mbele ya macho yangu...

Hii dunia ya sasa imeguaka 360 degrees .....

AD
 
wanajamvi kuna jambo limekuwa likisumbua akili yangu muda wote hasa nikitizama watoto tuliozaa huwa nawaza mambo mengi sana.nakumbuka hapo nyuma tulipokuwa tunakua wengi watakuwa mashahidi kila mtu mzima alichukua jukumu la kulea mtoto wa mwenzake bila kuangalia ni wa nani leo hii ambapo muda mwingi hatupo majumbani ukikuta mwanao kachapwa na jirani au kakaripiwa unaanza kukuna mengine mengi naamini mtayaweka humu tusisahau hata kama utawalea kwa maadili gani watoto wako kama watazungukwa na uchafu kila mahali itakupa wakati mgumu sana kwenye malezi tupende watoto wa wenzetu na tuwatazame kwa jicho lile lile tunalowapa watoto wetu naamini tutatengeneza kizazi bora na sisi sio kuwa maangamizi wa malaika hawa wa malai

ni mambo ya kukumbushana na kila mtu atekeleze wajibu wake kama mzazi,maana sikuu ya hesabu kila mtu atawasilisha mahesabu yake.
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom