Rev. Kishoka
JF-Expert Member
- Mar 7, 2006
- 4,526
- 1,529
Pamoja na tofauti zetu na mvutano wa hoja tunazojenga kila siku, tunakoelekea ni kwema na kwenye tumaini.
Ndiyo, bado hatujaweza kuwa na uwakilishi mzuri, lakini kwa udogo wetu, tunajifunza mengi na kuonyesha ni upeo gani mkubwa tulionao zaidi ya ule waliokuwa nao Babu na baba zetu.
TUmejikusanya humu kutoka kila upande wa dunia. Tukiwa na mvuto wa Gandhi, Mandela, Churchill, Roosevelt, Nkrumah, Toure, Bandaranaike, Somoza, Lenin, Mao, Reagan, Gorbachev, Morales, Lula, Ghadafi, Seretse Khama, Kenyatta, Khomeini na kila mvuto, uwe ni wa kibepari, kijamaa, kijimaa, kikabaila hata leo kwenye soko huria.
Sisi ni kizazi ambacho kitaiwezesha Tanzania iwe nchi yenye kufuata demokrasia ya kweli.
Hebu angalia jinsi Kuhani na FMES, wanavyoweza kubanjuana makonzi kwenye hoja moja, kisha wakaelewana kwenye hoja nyingine.
Angalia tulivyogawanyika katika suala hili la Mwakyembe, Dowans, Madili, Utu na haki, kila mmoja akifafanua upande wake na kuutetea.
Nakumbuka majuzi ni Susuviri kama si Companero, aliyetoa mfano wa jinsi gani Marekani ilivyoundwa na watu waliokuwa na mtazamo tofauti, ambao walikata shauri wakae chini wakajadili, wakawa na midahalo na mwishowe, wakazalisha katiba moja ambayo inaiongoza nchi yao mpaka leo, miaka zaidi ya 200!
Sisi ni fursa yetu, katika kizazi hiki, kutumia nafasi hii si kutengemana kwa kuwa hoja zetu zinapingana, bali ni kufungamana na kuheshimu uhuru wetu wa maoni, na kuidumisha Demokrasia inayoturuhusu kusikilizana na kubishana, huku tukinywa maji kwenye kisima kimoja na kukaa kwenye mkeka tukila chakula pamoja.
Laiti, kama wanasiasa wetu, babu na Baba zetu wangekuwa an mwamko na moyo wa kuwa wazi wenye kukubali kukosoana, kujadiliana na kutafuta kitu muafaka kwa ajili ya vizazi vijavyo.
Ni aibu kubwa sana, mpaka leo kuna makundi yanayoamini kuwa wao pekee ndio wenye kustahili kuiongoza Tanzania. hawa ni wale wenye kudai Tanzania ina wenyewe, kwamba hakuna mwingine kama wao, na wengine mkiamka kujitutumua kujitangaza, mtakandamizwa na kusahauliwa.
Mwanafalsafa Socrates alisema "The Unexamined life is not worth living", je sisi nasi tukubali kupokea ya Wazazi wetu ambao mpaka leo wanalataa kufanya tathmini ya kweli ya walichofanya na hata kukiri pale walipokosea.
Tunabalehe, Tunapevuka... Tunakomaa...
Idumu Jamii Forum!
Ndiyo, bado hatujaweza kuwa na uwakilishi mzuri, lakini kwa udogo wetu, tunajifunza mengi na kuonyesha ni upeo gani mkubwa tulionao zaidi ya ule waliokuwa nao Babu na baba zetu.
TUmejikusanya humu kutoka kila upande wa dunia. Tukiwa na mvuto wa Gandhi, Mandela, Churchill, Roosevelt, Nkrumah, Toure, Bandaranaike, Somoza, Lenin, Mao, Reagan, Gorbachev, Morales, Lula, Ghadafi, Seretse Khama, Kenyatta, Khomeini na kila mvuto, uwe ni wa kibepari, kijamaa, kijimaa, kikabaila hata leo kwenye soko huria.
Sisi ni kizazi ambacho kitaiwezesha Tanzania iwe nchi yenye kufuata demokrasia ya kweli.
Hebu angalia jinsi Kuhani na FMES, wanavyoweza kubanjuana makonzi kwenye hoja moja, kisha wakaelewana kwenye hoja nyingine.
Angalia tulivyogawanyika katika suala hili la Mwakyembe, Dowans, Madili, Utu na haki, kila mmoja akifafanua upande wake na kuutetea.
Nakumbuka majuzi ni Susuviri kama si Companero, aliyetoa mfano wa jinsi gani Marekani ilivyoundwa na watu waliokuwa na mtazamo tofauti, ambao walikata shauri wakae chini wakajadili, wakawa na midahalo na mwishowe, wakazalisha katiba moja ambayo inaiongoza nchi yao mpaka leo, miaka zaidi ya 200!
Sisi ni fursa yetu, katika kizazi hiki, kutumia nafasi hii si kutengemana kwa kuwa hoja zetu zinapingana, bali ni kufungamana na kuheshimu uhuru wetu wa maoni, na kuidumisha Demokrasia inayoturuhusu kusikilizana na kubishana, huku tukinywa maji kwenye kisima kimoja na kukaa kwenye mkeka tukila chakula pamoja.
Laiti, kama wanasiasa wetu, babu na Baba zetu wangekuwa an mwamko na moyo wa kuwa wazi wenye kukubali kukosoana, kujadiliana na kutafuta kitu muafaka kwa ajili ya vizazi vijavyo.
Ni aibu kubwa sana, mpaka leo kuna makundi yanayoamini kuwa wao pekee ndio wenye kustahili kuiongoza Tanzania. hawa ni wale wenye kudai Tanzania ina wenyewe, kwamba hakuna mwingine kama wao, na wengine mkiamka kujitutumua kujitangaza, mtakandamizwa na kusahauliwa.
Mwanafalsafa Socrates alisema "The Unexamined life is not worth living", je sisi nasi tukubali kupokea ya Wazazi wetu ambao mpaka leo wanalataa kufanya tathmini ya kweli ya walichofanya na hata kukiri pale walipokosea.
Tunabalehe, Tunapevuka... Tunakomaa...
Idumu Jamii Forum!