BongoLogik
JF-Expert Member
- Aug 10, 2009
- 260
- 44
Ikiwa unatumia LUKU na umenunua na kuweka umeme wa kutosha kwa matumizi yako mbali mbali, kama vile TV, music system,fridge, cooker etc. ina maana umelipia huduma ya umeme na hivyo inatakiwa upate umeme kwa kulingana na kiasi ulichonunua na kwa wakati muafaka, sasa inapotokea TANESCO wanakata umeme ovyo ovyo kwa sababu ambazo tumechoka kuzisikia miaka nenda rudi bila kuona juhudi za makusudi kukabiliana na kutatua tatizo hilo na badala yake tunapewa misamiati kama mpango mkakati,mpango kabambe,upembuzi yakinifu, mchakato unaendelea,mkandarasi ameshapatikana n.k inanisaidia nini mimi niliyeshanunua perege wangu kilo tano au kumi na kuwaweka kweye friji nikiwa na imani nitasogeza siku kadhaa, leo nina hasira nilinunua perege wangu juzi mama watoto akawaweka kwenye friji, nimeamua nishinde nyumbani jumapili hii ili tujinome ubwabwa kwa perege na familia yangu, nimeshindwa kumuelewa mama watoto eti perege wamechina kisa nini?! kisa kukatika ovyo kwa umeme! hivi hawa TANESCO wanadhani mimi nitakula nini leo na familia yangu? sasa naona hawa TANESCO wanataka kutupangia ratiba ya milo majumbani kwetu! imebidi mama ambilikile(mwanangu anaitwa ambilikile) akaniombee mlenda kwa shosti wake nikala na ubwabwa na sasa nataka nielekee palee nikapate tusker bariiidi nipunguze kama si kuongeza ghadhabu. Mimi nadhani tuna haki ya kudai fidia kwa TANESCO, ni kama vile mtu anapolipia huduma ya ulinzi kwa mwezi mmoja kwenye kampuni fulani ya ulinzi halafu walinzi wasifike kwenye lindo siku kadhaa ndani ya siku ulizolipia na uhalifu ukatokea, si utakuwa una haki ya kudai fidia? na sio wakuambie eti kwa kuwa walinzi hawakuja lindo siku tatu basi watazifidia hizo siku! si inatakiwa walipe hasara iliyotokana na uhalifu huo? hivyo hivyo na TANESCO inatakiwa wanilipe perege wangu na pia kwa wengine wote walioshapata madhara na hasara kwa kukatika umeme ovyo ovyo.