Tumpime Magufuli kwa sifa hizi na nafasi aliyoomba

mandago shululu

Senior Member
Mar 24, 2013
124
34

Top of Form
Bottom of Form
Top of ForBottom ofTop of Form Bottom of Form

TUTAKUWA WAKWELI KUSEMA UKWELI

Magufuri ni mtu mwenye visasi sana na yu tayari kuumiza uma wa watu katika kulipa visasi kwa wasio mjua mh. magufuri alipata kugombea ubunge jimbo la biharamulo mara mbili bila kupita mara zote aliangushwa na kina marehemu phares Kabuye kwa kura nyingi sana ,aliweza kupata ubunge pale tu wilaya ya biharamulo ilipogawanywa majibo mawili yaani Biharamulo Magharibi na Biharamulo mashariki Hivyo akafanikiwa kuingia bungeni kwa rushwa kubwa sana na kuwa mbunge wa Biharamulo mashariki wakati upande wa Biharamulo magharibi akiwa Mh. Choya.

Baada ya kupata ubunge Aliapa kiapo kama atahakikisha Biharamulo mashariki inakufa, kipindi hicho Magufuri alipata unaibu waziri hivyo alitumia nafasi hiyo kuivuruga Halmashauri ya Biharamulo na kwa influence miradi yote mikubwa ya wilaya ikawa inaenda jimboni kwake moja kwa moja bila hata kupitia Halmashauri watu wote walitishwa makao makuu ya wilaya na hakuna aliyeweza kusema lolote kama mnakumbuka vizuri alifikia kugombana na mbunge mwenzake wa mashariki aliyefikia kusema kama magufuri anatumia uwaziri wake kumhujumu jimboni mwake (kitendo kilichomuudhi sana magufuri na kuhakikisha nakufanikisha Mh.Choya anadondoka ktk ubunge wa Biharamulo Magharibi. Alifikia kuwa analeta wageni wakitaifa direct jimboni kwake hata bila kupitia makao makuu ya wilaya lakini nia ikiwa ni kiapo alichokiweka kuwa lazima ataiua biharamulo Magharibi kwa kumnyima ubunge mara mbili hapa nataka kuwaonyesha kiongozi huyu mcheshi mchapa kazi lakini mwenye visasi vyenye kuleta maafa kwa wazee wanawake na watoto.

Je, mtu huyu anaweza kuwa kiongozi wa umma?

Mwaka uliofuatia mheshimwa Magufuli alipita bila kupingwa baada mgombea mwingine aliyekuwa tishio kwake (jina nalihifadhi) kufanyiwa mizengwe wakati wa kurudisha form mpokea form alijificha na alijitokeza wakati mda wa kurudisha form umekwisha akaonekana mrudisha form amerudisha form too late lakini Mh. Magufuli alikuwa ameisha watisha viongozi wa chama na serikali wilayani biharamulo atakaepokea form za Bwana huyo basi yeye ni naibu waziri atahakikisha hana kazi watu wakatii na wakafanya dhuruma ya kumpitisha magufuri bila kupingwa.Je mtu huyu anaweza kuwa kiongozi wa umma?

Mwaka 2005 kijana mdogo anaitwa nahifadhi jina lake kupitia chama cha CUF ambaye alikuwa katibu wa wilaya wa CUF wilayani biharamulo alichukuwa form kugombea jimbo la biharamulo mashariki kwa magufuri huku akiwa na suport kubwa sana ya vijana na alikuwa anaenda kumwamgusha mh. Magufuli katika kinyanganyiro hicho, alichofanya Mh. Magufuli alimteka kijana huyo na kumpakia kwenye gari hadi mwanza kutoka mji mdogo wa Buseresere walimpelekea mke wa huyo bwana pesa wakampatia simu aongee na mme wake wakimshawishi waende hadi Mwanza wampatie pesa aondoe jina kwani pesa kidogo ya matumizi wameishamwachia mke wake yule bwana. Alipofika mwanza akapandishiwa dau hadi milioni 60 akubali kutorudisha form za ubunge ikiwa hapo imebaki siku 4 kabla form kurudishwa kijana akakabidhi form zake kwa Magufuli wakaenda nae hadi bank kijana kabaki kwenye bench mh. waziri akaingia ndani akatoka akamwambia account yake pale haina pesa waongozane hadi Dar es salaam. Wakapanda ndege hadi Dar kijana akafikishiwa kwenye 3 star hotel kwa bili ya mheshimiwa siku tatu bila kuonanana Mh. Magufuli.

Siku ya nne kijana anaona kwenye TV Magufuli amepita bila kupingwa akashtuka kaulizia hadi ofisini kwa waziri kafika akakaribishwa Mh. kama hamjui akamuuliza shida yako nini akasema nipe pesa zangu mh. akamwambia unakuja kuniomba rushwa nikuachie ubunge wewe kijana huna adabu kabisa. Mkifuatilia CUF, hiki kisa wanakijua vizuri kwani walipelekewa taarifa kama kuna mgombea wao ameenda kuuza ubunge kwa Magufuli ikabidi Green GUARD ya CUF iende kum-arrest na kumpeleka Buguruni makao makuu na kurudi Biharamulo kwa aibu kubwa lakini baadae alimtafutia kazi kwenye mgodi huko Tulawaka anafanya kazi kumziba mdomo kwa sababu kijana alikuwa ameapa kumfanyizia.

Huyu ndiye Magufuli, je anaweza kuwa kiongozi wa nchi katika uhuni wa namna hii?

Sinema ya Magufuli haiishi hapo; kile kiapo chake cha kulipa kisasi Biharamulo Magharibi kiliendelea alipolazimisha kupindisha barabara ya lami kuingia Chato toka Mwanza kwenda Bukoba kupitia Biharamulo makao makuu ya wilaya akaipindishia Chato nyumbani kwake na kuua makao makuu ya wilaya ya Biharamulo. Huyu ndiye kiongozi anayeweza kuongoza watu?

Mh. Magufuli alipigana na kulobby kwa nguvu zote kuhakikisha Chato inakuwa wilaya ili Biharamulo Magharibi wasifaidi mapato ya ziwa ambalo yanapatikana upande wa Chato na Nyamirembe na ndiyo kilichokuwa chanzo kikuu cha mapato cha wilaya ya Biharamulo lengo ikiwa ni katika kuendelea kulipa visasi kwa nini upande wa magharibi walikuwa hawampi kura kwa mihura takribani miwili alifaulu na Chato ikawa wilaya mpya toka Biharamulo.

Alipojikuta amesahau kuwa mgodi wa Tulawaka upo Biharamulo na haupo Chato alianza kuharasi uongozi wa wilaya ya Biharamulo kuwa ule mrahaba wa mwisho wa mwaka unaotolewa na migodi kwenye halmashauri za wilaya migodi ilipo alitaka Biharamulo igawane nusu kwa nusu mrahaba wake na wilaya ya Chato. Huyu ndiye Mh. Magufuli, je rais anaweza kuwa na tabia hizi chafuchafu namna hii?

Iliposhindikana akiwa waziri wa ardhi Mh. magufuri kwa makusudi kabisa alibadilisha mawe ya mpaka kwa amri kama waziri wa ardhi kuiingiza Tulawaka ndani ya wilaya ya chato hivyo siku si nyingi chato itadai Tulawaka ipo kwao na watapola haki ya wana biharamulo swala hili lipo wazi kabisa halmashauri ya wilaya kupitia baraza la madiwani limelalamika sana kuhusu ushenzi huu wa magufuri huyu ndiyo mtu anaweza kuwa raisi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania?

Mwaka jana katika mpaka mwingine wa biharamulo na chato kijiji cha biharamulo kinachopakana na chato huko kata ya Runazi wanakijiji waligundua kuna dhahabu na kuna wachimbaji wadowadogo Mh. magufuri yupo analazimisha kubadili mipaka ili hiki kijiji kihamie wilayani chato na kumekuwa na mgogoro wa kiutawala unochochewa na yeye Huyu ndiyo Mh. Magufuli anaepigiwa debe humu ndani kama anaweza kuwa rais rais huangaliwa pande zote mafanikio na madhaifu kwangu mimi madhaifu ya magufuri ni mengi kuliko mafanikio mtakumbuka kilio cha nyumba za serikali lakini huyu jamaa mkumbuke ni bingwa wa kusimamia wakandarasi na kutaka viwango kktk ujenzi lakini yote tisa kumi mh. anajenga ghotofa pale kwake anapoishi Osterbay yeye nendeni mkaone maajabu ya mussa wajenzi mafundi mchundo hata ramani hazijapitishwa sababu wachoraji ni watu wa mitaani na mafundi ni ni vibaruwa mchundo huyu ndiyo Mh. Magufuli.

Lakini skendo kubwa ya huyu bwana ambayo waandishi wangefuatilia kumjua vizuri ni jinsi alivyochezea mipaka ya wilaya ya Biharamulo kubadilisha DN za vijiji na kusogezwa mawe yalioizinishwa na serikali bila hata serikali kujua kuzipeleka Chato hii ni hujuma kubwa na anastahili kujiuzulu waandishi nendeni mkawahoji wananchi na viongozi wa wilaya biharamulo mjue huyu mtu kitu alichofanya mtu namna hii hawezi kuwa kiongozi kabisa

Huko jimboni kwake wafanyakazi wa serikali wote walio against naye amewaumiza sana wengine hata kufunga vibiashara vyao vidogovidogo ili tu wakubaliane naye kifupi hajawahi kupita bila kupngwa ila amekuwa akipita kwa hila kubwa.

Naomba kuwasilisha ili tumpime kwa pamoja. Je, tabia hizi zinaweza kumpa urais kweli?

Mandago
Katibu Chadema (W) Kwimba

Hayo ni machache tu, kwa mengi zaidi tuwasiliane kwa
mshululu@yahoo.com
0765183733,0782270412.

 
Magufuli atakuwa hovyo tu kama mtangulizi wake,mbaya zaidi atakuwa kibaraka wa Mzee Msoga,Prince,Wama na mafisadi wengine,nothing new zaidi ya speech za kukariri kama kasuku na majigambo ya kisukuma na kihaya kwa mbaaaalii
 
Huyu ata katiba mpya .itapitishwe ile ile tulio tengenezewa na chama cha ccm.huyu nikuakikisha ashindi urais
 
Unatafuta umaarufu kuptia magufuli ulikuwa wapi kusema cku zote hadi leo Kama cyo mnafki ungesema mapema Kama unamapenzi ya dhati na nchi ww cyo mzalendo unasubri hadi ki2 kinahappen ndo unaanza unafki 2mia akili Tanzania imebadilika xana
 
Magufuli atakuwa hovyo tu kama mtangulizi wake,mbaya zaidi atakuwa kibaraka wa Mzee Msoga,Prince,Wama na mafisadi wengine,nothing new zaidi ya speech za kukariri kama kasuku na majigambo ya kisukuma na kihaya kwa mbaaaalii
JK amemsifia kwamba HUWA ANAJUA NINI ATAKAIWA FANYA NA AFANYE VIPI?CCM wamemsifia sana kwamba ana nidhamu na kufuata maelekezo...hawakumpa jukumu la kuelekeza tunarudi palepale Magufuli ni Kibaraka,ni Nyapara...ni wa kuelekezwa akakimbize vibarua ila si wa kutoa maelekezo.
 
ccm hata imsimamishe malaika lazima atakuwa fisadi maana wote ni mafisadi walio shindikana. kwa hiyo magufuli hata kama akishinda ataenda kucheza atakavyoelekezwa na walisaini mikataba ya gezi na sio matakwa ya wananchi
 
magufuri amesema wazee watalindwa,mikataba ya mwinyi,mkapa na gesi yetu wote watalindwa.Tutavfute mengine
 
Hizi tuhuma nafikiri sio mwafaka katika darubani sanifu lenye mawani sahihi katika tija kwa Taifa.
Basi na Mwanza nao walalamike kwamba jamaa kawamegea Geita kutoka katika mkoa wa Mwanza na anaihujumu. Hizi nafikiri ni inferiority complex ama ni maono yasiyo na dhamira sahihi.

Ku-decetralize huduma za jamii ni kurahisisha upatikanaji wa huduma na kuwarahisishia wananachi kufikia huduma kwa mda. Fikiria Walimu walikuwa wanatembea kwa mguu siku mbili nzima takribani KM 80 kwenda kufuata mishara yao Biharamulo wilayani na hapo kati kati kuna kipori kina simba. Sasa kuwasogezea huduma karibu ni kuwasogezea maendeleo zaidi na isitafsiriwe ni kuitenga sehemu fulani.

Chukulia mfano, watoto upande ule karibu wote wa umrifulani karibu wote walikuwa hawana vyeti vya kuzaliwa kwa sababu nani atembee Km kadhaa kwenda kutafuta cheti cha kuzaliwa cha mtoto, na huko atasumbuliwa siku kadhaa, hivyo ni msisitizo tu decetralization ni njia sahihi inayotumika kuwaletea maendeleo karibu wananchi na isitafsriwe vinginevyo.

Kuhusu barabara, lengo lilikuwa ni kutoka Mwanza hadi Bukoba, ili wananchi wa Bukoba wasipite Kenya Uganda na kuingia Bukoba, hivyo hii serikali ni masikini sasa kama lengo ni kufika Bukoba kwanini njia fupi isitumike kufikia malengo yale yale kwa gharama nyepesi zaidi? Barabara ile ingepitishwa kama mdau anavyodai basi ongezeko la KM nyingi zaidi ya 100 zingeongezeka.

Tuhuma za kutekwa mgombea nafikiri intuitively sio kweli, maana wagombea hao wote mara zote wao wanarudisha form dakika za mwisho tu?? kuna maswali mengi ya kuhoji.
 
Unatafuta umaarufu kuptia magufuli ulikuwa wapi kusema cku zote hadi leo Kama cyo mnafki ungesema mapema Kama unamapenzi ya dhati na nchi ww cyo mzalendo unasubri hadi ki2 kinahappen ndo unaanza unafki 2mia akili Tanzania imebadilika xana

tatizo mda mwingne watanzania hawajui wanataka nini.
 
No cyo hvo Kama ww n mzalendo wa kwel lazma ukemee makoxa mwanzon kabxa cyo kuja kulaumu huu n unafki mkubwa na lazma ukemewa labxa
 
Hizi tuhuma nafikiri sio mwafaka katika darubani sanifu lenye mawani sahihi katika tija kwa Taifa.
Basi na Mwanza nao walalamike kwamba jamaa kawamegea Geita kutoka katika mkoa wa Mwanza na anaihujumu. Hizi nafikiri ni inferiority complex ama ni maono yasiyo na dhamira sahihi.

Ku-decetralize huduma za jamii ni kurahisisha upatikanaji wa huduma na kuwarahisishia wananachi kufikia huduma kwa mda. Fikiria Walimu walikuwa wanatembea kwa mguu siku mbili nzima takribani KM 80 kwenda kufuata mishara yao Biharamulo wilayani na hapo kati kati kuna kipori kina simba. Sasa kuwasogezea huduma karibu ni kuwasogezea maendeleo zaidi na isitafsiriwe ni kuitenga sehemu fulani.

Chukulia mfano, watoto upande ule karibu wote wa umrifulani karibu wote walikuwa hawana vyeti vya kuzaliwa kwa sababu nani atembee Km kadhaa kwenda kutafuta cheti cha kuzaliwa cha mtoto, na huko atasumbuliwa siku kadhaa, hivyo ni msisitizo tu decetralization ni njia sahihi inayotumika kuwaletea maendeleo karibu wananchi na isitafsriwe vinginevyo.

Kuhusu barabara, lengo lilikuwa ni kutoka Mwanza hadi Bukoba, ili wananchi wa Bukoba wasipite Kenya Uganda na kuingia Bukoba, hivyo hii serikali ni masikini sasa kama lengo ni kufika Bukoba kwanini njia fupi isitumike kufikia malengo yale yale kwa gharama nyepesi zaidi? Barabara ile ingepitishwa kama mdau anavyodai basi ongezeko la KM nyingi zaidi ya 100 zingeongezeka.

Tuhuma za kutekwa mgombea nafikiri intuitively sio kweli, maana wagombea hao wote mara zote wao wanarudisha form dakika za mwisho tu?? kuna maswali mengi ya kuhoji.
Maadam sio malaika nafikiri dark side zake pia ni vema zifahamike ili mizani ya kumpima ifanye kazi bila upendeleo.
 
Maadam sio malaika nafikiri dark side zake pia ni vema zifahamike ili mizani ya kumpima ifanye kazi bila upendeleo.

Siyo Malaika
Kweli, lakini mfano aliweza je kushawishi serikali igawe jimbo wakati huo alikuwa Mkemia nyaza. Sioni feasiblility iliyopo hapo, na kwanini serikali iliamua kuligawa jimbo maana liligawiwa kabla hata ya kuwa mbunge. Kuna maswali mengi ya kuhoji hiyo unayoita dark side.

Mfano mtoa tuhuma anaposema viongozi walikuwa wanaenda moja kwa moja kwa jimbo la Magufuli, sasa swali kwani Magufuli alikuwa mbunge wa majimbo yote mawili? kila mtu si anapigania jimbo lake bwana ili wananchi wa jimbo lake wapate kumchagua ama sio? kuna conflict za information nyingi sana ktk unayoita dark side.
 
Mnataka perfection. Kachongeni gogo la mvule mliweke ikulu. Magufuli rais kwisha habari
 
magufuri amesema wazee watalindwa,mikataba ya mwinyi,mkapa na gesi yetu wote watalindwa.Tutavfute mengine

Huyu mwenye kuamka na kusems "wewe nimekufukuza kazi", wakati yeye mwenyewe ndiye amempa tender kwa mbwembwe kibao. Naona mna mstumaini makubwa kwa marudio ya vitu ambavyo 'hamtaki kuviona' .
 
Salaam!

Sitaki tubishane ama kuwekeana ushabiki katika hili. Lakini ukitazama kwa jicho kubwa namna Magufuli alivyopenya ndani ya CCM utabaini kuwa huenda ni matokeo ya sala za watanzania kuhusu nchi yao. Mara nyingi kumekuwa na makongamano ya madhehebu mbalimbali ya kuombea mema katika nchi yao.

Na bila shaka tunatamani kuamini kuwa huenda ushindi wa Magufuli ndani ya CCM ni matokeo ya sala za watanzania kwa taifa lao. Hakuna mwenye maandishi mazuri ya kuweza kuelezea ujio wa Magufuli kwenye urais hapa Tanzania.

Kama utabisha endelea kubisha kufurahisha jukwaa!
TeamLowassa

Wakuu.

Wakati huu tunapoelekea uchaguzi mkuu wa mwezi Oktoba mwaka 2015, hatuna budi kujikumbusha matuikio kadhaa ya nyuma ambayo yanamhusu mgombea wa nafasi ya Uras kupitia chama cha mapinduzi CCM, John Pombe magufuli.

Naelewa kuwa yapo matukio mengi (ya kulisaidia taifa) ambayo ndani ya jamvi au hata nje wapo wanayoyafahamu na kama watahiari kuyatoa hadharani litakuwa jambo jema.

Wakati Mkapa akijiandaa kutoka madarakani (2005) serikali yake ilikuwa imekamilisha mradi wa ujenzi wa barabara za lami za jiji la Mwanza hivyo Rais Mkapa alifika Mwanza kwa ajili ya uzinduzi huo wa kuliondoa jiji hilo kutoka kwenye adha kubwa ya vumbi na mashimo kama sio mahandaki.

Katika uzinduzi huo (nafikiri wa km 53 za lami) uliofanyika katika mzunguko wa barabara za Kenyetta, Nyerere na Uwanja wa ndege, viongozi mbalimbali walihudhuria ikiwa ni pamoja na waziri wa maendeleo ya maji wa wakati huo, Edward Lowassa.

mara baada ya magufuli kumaliza kushusha takwimu kuhusu barabara nchini na kuahidi kuwa itawezekana kusafiri kwa teksi kutoka Bukoba hadiMtwara ifikapo mwaka 2006, bila kutarajiwa Lowassa, (labda la bifu, au kutoka kuonekana na yeye ni mchapa kazi) alikisongelea kipaza sauti na kuanza kuzungumza kwa kujisifia kuwa naye ni "Askari wa Mwamvuli" kwani anatekeleza mradi wa kutoka Maji Ziwa Viktoria kwenda Kahama mkoani Shinyanga, hivyo sio Magufuli tu ndiye Waziri anayepaswa kusifiwa kwa uchapakazi!

Tuliokwepo tulibaki tukitafakari mantiki ya Kitendo hicho cha Lowassaa kwani hakuwa miongoni mwa waliokuwa wamepangwa kuzungumza katika tukio hilo. Wachache tuliona kuwa suala hilo lina uhusiano kwa kiasi kikubwa na mbio za kutaka kuingia Ikulu, ingawa wakati huo Magufuli hakuwa ametangaza kuitaka nafasi hiyo. LOwassaa alikuwa akimuogopa Magufuli tangu wakati huo?

Jambo la pili ambalo pia linahusika na ujenzi wa barabara za Mwanza ni kumhusu Naibu waziri wa uchukuzi wa sasa Dr Tizeba. wakati wa serikali ya awamu ya Tatu Tizeba alikuwa Mhandisi wa jiji la Mwanza na inafahamika kwamba wawili hawa hazikuwa zinaiva, kwa magufuli kubeza elimu ya uhandisi ya Tizeba aliyopata nchini Urusi huku hali ya miundombinu ya jiji ikiendelea kuzorota.

kilele cha yote ilikuwa ni kubomolewa kwa kituo cha mafuta kilichojengwa ndani ya hifadhi ya barabara eneo la makongoro. Inaelezwa Tizeeba ndiye aliyefanikisha kutolewa kwa kiwanja hicho na badaye kupewa kazi ya ujenziwa kituo hicho mali ya mbunge wa sasa wa kwimba.

Sakata hilo lilipelekea Tizeba kufukuzwa kazi, ingawa haielezeki hata sasa nini kilitokea tena kwa serikali iliyomtimua kumrejesha hadi kumpatia wadhifa wa naibu waziri. Labda siku moja tutakuja kupata maelezo ya kilichotokea kwa Tizeba kurudi na kisha iwapo wawili hawa wanaweza kufanya kazi pamoja.

Tanzania ni nchi unayofuata mfumo wa siasa za vyama vingi, Kitu cha kushangaza wapo watu wamejenga dhana potofu, Na kuamini nchii hii ni ya CCM tu"Ni yetu sote".

Hii inapelekea hata Nape kuongea upuuzi wa kwenda ikulu kwa goli la mkono.

Na hata media nyingi kujikomba kwa CCM sababu ya dhana ya kijinga uliyojengwa na CCM mioyoni mwa watanzania.
NASEMA"Si lazima mteule wa CCM awe rais wa nch hii (Tanzania) Vipo na vyama vingine vingi tena Imara vinafanya siasa,Kuna dhana na hisia za kipuuzi zishateka watu kuwa mtu aliyeteuliwa na CCM tayari ni rais wa nchii hii hata kabla uchaguzi kufanyika.

Huu ni ulimbukeni na ni utumwa wa kifkira. Na mwisho wake ni Octoba 25

 
Salaam!

Sitaki tubishane ama kuwekeana ushabiki katika hili. Lakini ukitazama kwa jicho kubwa namna Magufuli alivyopenya ndani ya CCM utabaini kuwa huenda ni matokeo ya sala za watanzania kuhusu nchi yao. Mara nyingi kumekuwa na makongamano ya madhehebu mbalimbali ya kuombea mema katika nchi yao.

Na bila shaka tunatamani kuamini kuwa huenda ushindi wa Magufuli ndani ya CCM ni matokeo ya sala za watanzania kwa taifa lao. Hakuna mwenye maandishi mazuri ya kuweza kuelezea ujio wa Magufuli kwenye urais hapa Tanzania.

Kama utabisha endelea kubisha kufurahisha jukwaa!
TeamLowassa


nakubaliana nawe mkuu! kwa sababu ukiangalia wale watano waliokuwa wamepitishwa na chama kikuu, unaona wazi lengo lilikuwa ni kuwadididmiza wagalatia na kuendeleza mikakati na agenda za ABUJA! lakini mapinduzi yaliyofanyika, hapo ndipo unajua kweli Mungu amejibu sala za wagalatia!:glasses-nerdy:
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom