Tumeshindwa, tuombe msaada kwa wazungu?

duu! Mkuu Makanyaga maandishi hayo, mimi nimeshindwa kusoma too much, pls mods help him.
 
Alfu mnasema abolish the death penalty...! A society that butchers its own... If it were up to me i would have them Hung Drawn and Quartered. Or if that is too harsh then I would have them publicly executed, tena Mnazi mmoja. Barbaric animals,
 
Nikushangaze! Hata hao polisi upelelezi na TISS ukiwawekea dau la milioni 2 kwa kichwa wakuletee watu wanaouza viungo vya albino, nakuhakikishia utaletewa watuhumiwa, exhibits na ushahidi wa kutosha kuwatia hatiani. Ni njaa tu zinatesa watu. Hii mbinu ya kutangaza dau mbona hata nchi za wazungu (huko tunakoiga mambo mengi) huwa zinatumia kukamatia wahalifu sugu au korofi.

Wala sidhani kama wanahitaji kuwawekea dau la milioni mbili, nadhani wakubwa wao (IGP, Mkurugenzi wa TISS, makamanda wa mikoa/wilaya etc ) wakijua kuwa cheo ni dhamana na anaweza kunyang'anywa wakati wowote akapewa mtu mwingine atakayeweza kufanya kazi watafanya kazi.

Ila kama tukiendelea na mtindo wa mazoea kuwa wananchi watapiga kelele mwisho watasahau hakuna kitu kitafanyika....au tusipojali kwa sababu wanaokufa hawatuhusu mambo yataendelea. Mbona waliopiga msafara wa rais mawe wamepatikana baada ya siku chache na hatukusikia zawadi ya millioni 2 imeahidiwa?

Mbona ujambazi wa kuiba benki ulikuja kupungua kwa kasi ya ajabu, si baada ya kuona unaleta picha mbaya ....na unajua wenzetu serikalini wanavyowaogopa wawekezaji tena. Kwa hiyo nadhani issue hapa ni commitment tu ...wakiamua inawezekana.
 
Back
Top Bottom