Raia Fulani
JF-Expert Member
- Mar 12, 2009
- 10,876
- 2,747
Muda si mrefu napata habari. Kijana wa watu, tena graduate safi! yuko katika wakati mgumu kisaikolojia. Wasipompa nasaha vya kutosha atakuwa chapombe na asiye na mwelekeo daima. Msichana wake walianza mahusiano toka sekondari kisha binti akamtema huko huko na kumpata 'muungwana' zaidi. Wote wakaingia chuo na binti alipoona shule inakaribia kumchoka akaanza tena kumnyemelea jamaa warudiane, ikiwa ni pamoja na kumsaidia kimasomo. Jamaa baada ya kumkatalia sana akamkubalia kurudiana. Binti akawa njema kishule, ila shule ilipoisha akaanza tena makeke. Kampata wa juu zaidi ya mshkaji. Kamtosa jamaa. Jamaa anaugulia mno! Binti anatanua. Kapata kazi bomba, bwana mwenye nazo. Kijana anajuta. Alimtoa binti mbali na sasa katoswa. Anaumia. KWa nini wadada mnafanya haya? Sio mfano mmoja tu, iko mingi. Wadada wasomi mnatafuta nini maishani? Hata nyie wa kawaida pia. Kama humhitaji mwanaume jaribu kumuepuka kuliko kumtumia hivi. Hata kama unampenda na unaona utamwacha baadae, mwache sasa na uhangaike kivyako. Mnachuma lawama. Hii pia ni kwa pande zote, ila mada ni kuhusu hawa watu wawili