KATIBU wa Mambo ya Nje ya Sekreatarieti ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Januari Makamba amesema chama hicho kimejivua gamba ili kujenga imani kwa umma hasa vijana ambao ni wapiga kura.Kwa mujibu wa Makamba, CCM imefikia mahali ambako ilikuwa haiaminiki kwa umma kutokana na baadhi ya wanachama wake wakiwamo viongozi wa ngazi za juu kuhusishwa na tuhuma za rushwa na ufisadi.
Kujenga uaminifu kwa wananchi ni kazi kubwa ambayo tunatakiwa kuifanya, yaani wananchi watuamini kwani kama chama Serikali yetu inafanya kazi kubwa za maendeleo, lakini kama huaminiki hata kazi hizo zinaonekana kuwa ni bure,alisema.
Alisema katika mchakato wa kukijenga upya chama hicho, lazima idadi ya wanachama wa CCM waongezeke kutoka milioni tano wa sasa na pamoja na kujenga mfumo utakaokiwezesha chama hicho kuwa na viongozi waadilifu na weledi.
Miongoni mwa hatua tunazochukua ni kuhakikisha tunakuwa na viongozi wasio na madoa, pia watuhumiwa wote wa rushwa na ufisadi wajiondoe bila,alisema Makamba.
Makamba alisema hayo katika mahojiano maalumu na Mwananchi jijini Dar es Salaam."Chama kina wasemaji wake, Mwenyekiti, Katibu Mkuu na hasa Katibu wa Itikadi na uendezi si mimi, lakini niseme dhana ya kujivua gamba nia yake ni kujenga nchi ikiwa na CCM imara, madhubuti na kuleta maendeleo kwa wananchi wa Tanzania kupitia rasilimali zilizopo nchini," alisema Makamba.
Alifafanua kuwa msingi wa kuanzishwa CCM ni kuwaletea wananchi maendeleo na kwamba ili kufanikisha hilo chama hicho kinapaswa kujivua gamba kwa lengo la kurejea katika misingi yake.
"CCM ni 'progressive party', hivyo lazima kirudi katika msingi wake ambao ni kuleta maendeleo ya jamii kutumia rasilimali zilizopo," alisema Makamba.
Kuhusu nafasi yake ya sasa ndani ya Sekretarieti ya CCM, Makamba alisema kinachofanyika katika idara hiyo ni kujifunza na kwamba watafanya kazi kisayansi kwa kuyachambua mambo ili majibu yawe sahihi na yaliojitosheleza.
Alisema majukumu ya idara yake yametajwa katika Ibara ya 113 (3) ya Katiba ya CCM ambayo alisema ni mazito likiwemo la kukijenga upya chama hicho ili kipendwe, kipate wanachama wengi zaidi, viongozi weledi na waadilifu ili kishinde uchaguzi kwa urahisi bila kutumia nguvu zaidi.
Alipotakiwa kueleza chama gani kinaonekana kuwa tishio kwa CCM, Makamba alisema mtazamo wake ni kuwa vyama vyote vya upinzani ni sawa na kwamba katika ushindani wa kisiasa jambo la msingi ni kushindana kuwa na fikra na sera bora zinazovutia wananchi na kuwaletea maendeleo badala ya kupigana vijembe.
Kujenga uaminifu kwa wananchi ni kazi kubwa ambayo tunatakiwa kuifanya, yaani wananchi watuamini kwani kama chama Serikali yetu inafanya kazi kubwa za maendeleo, lakini kama huaminiki hata kazi hizo zinaonekana kuwa ni bure,alisema.
Alisema katika mchakato wa kukijenga upya chama hicho, lazima idadi ya wanachama wa CCM waongezeke kutoka milioni tano wa sasa na pamoja na kujenga mfumo utakaokiwezesha chama hicho kuwa na viongozi waadilifu na weledi.
Miongoni mwa hatua tunazochukua ni kuhakikisha tunakuwa na viongozi wasio na madoa, pia watuhumiwa wote wa rushwa na ufisadi wajiondoe bila,alisema Makamba.
Makamba alisema hayo katika mahojiano maalumu na Mwananchi jijini Dar es Salaam."Chama kina wasemaji wake, Mwenyekiti, Katibu Mkuu na hasa Katibu wa Itikadi na uendezi si mimi, lakini niseme dhana ya kujivua gamba nia yake ni kujenga nchi ikiwa na CCM imara, madhubuti na kuleta maendeleo kwa wananchi wa Tanzania kupitia rasilimali zilizopo nchini," alisema Makamba.
Alifafanua kuwa msingi wa kuanzishwa CCM ni kuwaletea wananchi maendeleo na kwamba ili kufanikisha hilo chama hicho kinapaswa kujivua gamba kwa lengo la kurejea katika misingi yake.
"CCM ni 'progressive party', hivyo lazima kirudi katika msingi wake ambao ni kuleta maendeleo ya jamii kutumia rasilimali zilizopo," alisema Makamba.
Kuhusu nafasi yake ya sasa ndani ya Sekretarieti ya CCM, Makamba alisema kinachofanyika katika idara hiyo ni kujifunza na kwamba watafanya kazi kisayansi kwa kuyachambua mambo ili majibu yawe sahihi na yaliojitosheleza.
Alisema majukumu ya idara yake yametajwa katika Ibara ya 113 (3) ya Katiba ya CCM ambayo alisema ni mazito likiwemo la kukijenga upya chama hicho ili kipendwe, kipate wanachama wengi zaidi, viongozi weledi na waadilifu ili kishinde uchaguzi kwa urahisi bila kutumia nguvu zaidi.
Alipotakiwa kueleza chama gani kinaonekana kuwa tishio kwa CCM, Makamba alisema mtazamo wake ni kuwa vyama vyote vya upinzani ni sawa na kwamba katika ushindani wa kisiasa jambo la msingi ni kushindana kuwa na fikra na sera bora zinazovutia wananchi na kuwaletea maendeleo badala ya kupigana vijembe.