‘Tumejivua gamba kujenga imani kwa vijana’

Lilombe

JF-Expert Member
Apr 11, 2011
242
39
KATIBU wa Mambo ya Nje ya Sekreatarieti ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Januari Makamba amesema chama hicho kimejivua gamba ili kujenga imani kwa umma hasa vijana ambao ni wapiga kura.Kwa mujibu wa Makamba, CCM imefikia mahali ambako ilikuwa haiaminiki kwa umma kutokana na baadhi ya wanachama wake wakiwamo viongozi wa ngazi za juu kuhusishwa na tuhuma za rushwa na ufisadi.


“Kujenga uaminifu kwa wananchi ni kazi kubwa ambayo tunatakiwa kuifanya, yaani wananchi watuamini kwani kama chama Serikali yetu inafanya kazi kubwa za maendeleo, lakini kama huaminiki hata kazi hizo zinaonekana kuwa ni bure,”alisema.

Alisema katika mchakato wa kukijenga upya chama hicho, lazima idadi ya wanachama wa CCM waongezeke kutoka milioni tano wa sasa na pamoja na kujenga mfumo utakaokiwezesha chama hicho kuwa na viongozi waadilifu na weledi.

“Miongoni mwa hatua tunazochukua ni kuhakikisha tunakuwa na viongozi wasio na madoa, pia watuhumiwa wote wa rushwa na ufisadi wajiondoe bila,”alisema Makamba.

Makamba alisema hayo katika mahojiano maalumu na Mwananchi jijini Dar es Salaam."Chama kina wasemaji wake, Mwenyekiti, Katibu Mkuu na hasa Katibu wa Itikadi na uendezi si mimi, lakini niseme dhana ya kujivua gamba nia yake ni kujenga nchi ikiwa na CCM imara, madhubuti na kuleta maendeleo kwa wananchi wa Tanzania kupitia rasilimali zilizopo nchini," alisema Makamba.

Alifafanua kuwa msingi wa kuanzishwa CCM ni kuwaletea wananchi maendeleo na kwamba ili kufanikisha hilo chama hicho kinapaswa kujivua gamba kwa lengo la kurejea katika misingi yake.

"CCM ni 'progressive party', hivyo lazima kirudi katika msingi wake ambao ni kuleta maendeleo ya jamii kutumia rasilimali zilizopo," alisema Makamba.

Kuhusu nafasi yake ya sasa ndani ya Sekretarieti ya CCM, Makamba alisema kinachofanyika katika idara hiyo ni kujifunza na kwamba watafanya kazi kisayansi kwa kuyachambua mambo ili majibu yawe sahihi na yaliojitosheleza.

Alisema majukumu ya idara yake yametajwa katika Ibara ya 113 (3) ya Katiba ya CCM ambayo alisema ni mazito likiwemo la kukijenga upya chama hicho ili kipendwe, kipate wanachama wengi zaidi, viongozi weledi na waadilifu ili kishinde uchaguzi kwa urahisi bila kutumia nguvu zaidi.

Alipotakiwa kueleza chama gani kinaonekana kuwa tishio kwa CCM, Makamba alisema mtazamo wake ni kuwa vyama vyote vya upinzani ni sawa na kwamba katika ushindani wa kisiasa jambo la msingi ni kushindana kuwa na fikra na sera bora zinazovutia wananchi na kuwaletea maendeleo badala ya kupigana vijembe.
 
shiiiiiiiiiiiiiiiiiiiit. january kapata mtindio wa ubongo. anadhani hilo la kujivua gamba litawasaidia kwa kiasi fulani. hajui kwamba hata wale waliokuwa wkikisupport ccm ndo wa kwanza kukilaumu na kukikimbia baada ya ccm kukiri wana magamba.
 
Imani kwa vijana imesharudi na sasa vijana wanajipanga kuwaletea ushindi mwaka 2015 ukizingatia ajira zilizoongezeka baada ya sera za kuvuana magamba kuanza hadi kufikia 2015 hakutakuwa na kijana ambaye atakuwa hana ajira so ushindi huo unakujaaaa!!!!:smile-big::smile-big::smile-big::smile-big:
 
ccm haiwezi kuwa na mvuto tena kwa vijana, lakini ni lazima upinzani hasa chadema kupita kijiji baada ya kijiji na kuhakikisha chadema inatambulika kila kona ya nchi, wasilale kama walivyolala katika jimbo la newala ambapo mpaka siku za mwisho kabisa walikua hawajapata wa kusimama nafasi ya ubunge. hii inamaana kwamba kwenye hiyo wilaya wafuasi wake walikua ni wachache sana au hakuna kabisa.
 
Imani kwa vijana imesharudi na sasa vijana wanajipanga kuwaletea ushindi mwaka 2015 ukizingatia ajira zilizoongezeka baada ya sera za kuvuana magamba kuanza hadi kufikia 2015 hakutakuwa na kijana ambaye atakuwa hana ajira so ushindi huo unakujaaaa!!!!:smile-big::smile-big::smile-big::smile-big:
Ni wiki kadhaa (chache) zimepita tangu ccm kutoa kauli ya kujivua magamba. Ikumbukwe kuwa hiyo ni kauli tu na sio vitendo. Matokea ya vitendo vya magamba hayo hayawezi kufutwa na kauli za mdomoni. Mimi naona kuwa wapambe wa magamba na ccm hawajajua bado kina cha taabu, vifo na dhiki ambazo wamezipata wananchi, wakiwemo pia vijana. Hivyo ni dharau kubwa, au ujinga kusema kuwa imani ya vijana imesharudi baada ya kusikia hiyo kauli ya kujivua magamba. Inamaanisha kuwa vijana wa Kitanzania wana kumbukumbu fupi sana, na hata hali yao ya kimaisha inawezwa kubadilishwa na maneno ya majukwaani.

Naamini kuwa vijana wa Kitanzania wana akili nyingi za kujua nani anawahadaa na nani anawapa matumaini. Mpaka hivi leo, 'kujivua magamba' kumebakia kauli tupu pamoja na kusogezwa kwa magamba machache katika nyadhifa zao. Mpaka hivi sasa, Tanzania imeshikiliwa na inaendeshwa na magamba, ambayo kiukweli ni kuwa kujivua kwao kwa magamba hayo ni kifo chao. Umeshawahi kumvua kobe gamba lake? Ukumvua gamba kobe, utamuua, kwa vile hataweza kuishi bila gamba lake.
Tafakari...!
 
Nyoka ni nyoka tu siku zote...hawezi kubadilika kua mjusi kisa tu kajivua gamba! CCM ni chama cha waoga! walioiibia nchi hii na wanatumia nguvu nyingi kuficha maovu yao,nadhani hofu ya kuadhirika ii wazi vichwani mwao!...
 
CCM watakapojua watanzania wanahitaji nini ndipo watapata suluhisho. Lakini hii misamiati na kufungua matawi mapya sijui Marekani hayana maana kabisa. Mbona matawi yapo kibao tu. Tafuteni watanzania wanahitaji nini kwa sasa na siyo kuongeaongea tu kwenye vyombo vya habari.
 
huu wimbo wa kuvua gamba kutoka ccm haona beat na vina
kila siku ccm wanasema wanavua gamba na kuna watu wanatuhuma za ufisadi
lakini hakuna siku waliyotutendea haki wananchi kwa kutuambia hizo tuhuma ni zipi?
kama ni zile za DR SLAA, ina maana wanamfukuza mwenyekiti wa chama chao?
tunaomba ccm waucheze mziki wa DR SLAA kwa staha na kwa step,
kama watamwacha mwenyekiti wao kupiga ngoma za huu muziki , sisi wananchi
hatuta rudisha imani kamwe maana MKUU WA KAYA n miongozi wa wezi wa ngoma,
naye avuliwe gamba kisha njooni kutuomba imani

KATIBU wa Mambo ya Nje ya Sekreatarieti ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Januari Makamba amesema chama hicho kimejivua gamba ili kujenga imani kwa umma hasa vijana ambao ni wapiga kura.Kwa mujibu wa Makamba,CCM imefikia mahali ambako ilikuwa haiaminiki kwa umma kutokana na baadhi ya wanachama wake wakiwamo viongozi wa ngazi za juu kuhusishwa na tuhuma za rushwa na ufisadi.


"Kujenga uaminifu kwa wananchi ni kazi kubwa ambayo tunatakiwa kuifanya, yaani wananchi watuamini kwani kama chama Serikali yetu inafanya kazi kubwa za maendeleo, lakini kama huaminiki hata kazi hizo zinaonekana kuwa ni bure,"alisema.

Alisema katika mchakato wa kukijenga upya chama hicho, lazima idadi ya wanachama wa CCM waongezeke kutoka milioni tano wa sasa na pamoja na kujenga mfumo utakaokiwezesha chama hicho kuwa na viongozi waadilifu na weledi.

"Miongoni mwa hatua tunazochukua ni kuhakikisha tunakuwa na viongozi wasio na madoa, pia watuhumiwa wote wa rushwa na ufisadi wajiondoe bila,"alisema Makamba.

Makamba alisema hayo katika mahojiano maalumu na Mwananchi jijini Dar es Salaam."Chama kina wasemaji wake, Mwenyekiti, Katibu Mkuu na hasa Katibu wa Itikadi na uendezi si mimi, lakini niseme dhana ya kujivua gamba nia yake ni kujenga nchi ikiwa na CCM imara, madhubuti na kuleta maendeleo kwa wananchi wa Tanzania kupitia rasilimali zilizopo nchini," alisema Makamba.

Alifafanua kuwa msingi wa kuanzishwa CCM ni kuwaletea wananchi maendeleo na kwamba ili kufanikisha hilo chama hicho kinapaswa kujivua gamba kwa lengo la kurejea katika misingi yake.

"CCM ni 'progressive party', hivyo lazima kirudi katika msingi wake ambao ni kuleta maendeleo ya jamii kutumia rasilimali zilizopo," alisema Makamba.

Kuhusu nafasi yake ya sasa ndani ya Sekretarieti ya CCM, Makamba alisema kinachofanyika katika idara hiyo ni kujifunza na kwamba watafanya kazi kisayansi kwa kuyachambua mambo ili majibu yawe sahihi na yaliojitosheleza.

Alisema majukumu ya idara yake yametajwa katika Ibara ya 113 (3) ya Katiba ya CCM ambayo alisema ni mazito likiwemo la kukijenga upya chama hicho ili kipendwe, kipate wanachama wengi zaidi, viongozi weledi na waadilifu ili kishinde uchaguzi kwa urahisi bila kutumia nguvu zaidi.

Alipotakiwa kueleza chama gani kinaonekana kuwa tishio kwa CCM, Makamba alisema mtazamo wake ni kuwa vyama vyote vya upinzani ni sawa na kwamba katika ushindani wa kisiasa jambo la msingi ni kushindana kuwa na fikra na sera bora zinazovutia wananchi na kuwaletea maendeleo badala ya kupigana vijembe.
 
Nipewe mdahalo na huyu kijana,awaeleze watanzania mambo yafuatayo:-
1. Akiwa mwanaccm mwaminifu, awaambie watanzania,ii wapi pesa yetu waliyiba hao anaowaita magamba kwa sasa?
2. Akiwa kiongozi wa ccm sasa, awaambie watanzania, je kama wamevua magamba kwa tuhuma za ufisadi, wamewafikisha mahakamani ili wachukuliwe hatua za kisheria kwa kuhujumu uchumi?
3. Awaambie watanzania, kama ccm imeinua mikono juu kwa cdm, kwa kutekeleza matamko ya cdm ya kuwaadhibu mafisadi?
4. Nini faida kwa watanzania, kwa kitendo chao cha kujivua hayo magamba hewa?
5. January sio gamba changa limealo, baada ya baba yake kuitwa gamba zee lililovuliwa?
 
Back
Top Bottom