Gosbertgoodluck
JF-Expert Member
- Mar 3, 2008
- 2,855
- 401
Ndugu zangu wana JF,
Hivi wananchi wanaolalamika kuhusu kupanda kwa bei ya umeme, walitarajia nini wakati wenyewe ndiyo walioichagua ccm?? Mtazamo wangu ni kuwa kama wamemchagua jk na ccm yake, basi watulie wanyolewe vizuri.
Kamwe wasilalamike maana wao ndiyo walioiweka serikali madarakani. Kupanda bei kwa huduma muhimu kutaendelea mtindo mmoja mpaka kieleweke.
Hivi sasa sumatra wapo kwenye mchakato wa kupitisha nauli mpya za usafiri wa mabasi. Ewura wana maombi lukuki ya kupandisha bei za huduma ya maji kutoka miji mbalimbali nchini.
Kwa kuwa wenyewe ndiyo tumeichagua CCM basi siyo busara kuleta usumbufu. Tutulie tunyolewe hata kama wembe unaotumila ni butu. Maumivu tutakayopata yatatusaidia kufanya uamuzi wa busara ifikapo 2015.
Hivi wananchi wanaolalamika kuhusu kupanda kwa bei ya umeme, walitarajia nini wakati wenyewe ndiyo walioichagua ccm?? Mtazamo wangu ni kuwa kama wamemchagua jk na ccm yake, basi watulie wanyolewe vizuri.
Kamwe wasilalamike maana wao ndiyo walioiweka serikali madarakani. Kupanda bei kwa huduma muhimu kutaendelea mtindo mmoja mpaka kieleweke.
Hivi sasa sumatra wapo kwenye mchakato wa kupitisha nauli mpya za usafiri wa mabasi. Ewura wana maombi lukuki ya kupandisha bei za huduma ya maji kutoka miji mbalimbali nchini.
Kwa kuwa wenyewe ndiyo tumeichagua CCM basi siyo busara kuleta usumbufu. Tutulie tunyolewe hata kama wembe unaotumila ni butu. Maumivu tutakayopata yatatusaidia kufanya uamuzi wa busara ifikapo 2015.