Tabutupu
JF-Expert Member
- Nov 26, 2010
- 13,108
- 18,325
TUMEDANGANYWA NA UTANDAWAZI
1. Hivi ni kweli kuwa kila tunacho kiona kwenye medi ndio maisha halisi ya Mzungu .
2. Je kuna umihimu wowote kuendeleza tamaduni zetu ambazo tuliachiwa na babu zetu.
Mi e binafsi naona kama tunajidanganya kwani mara nyingi tumeingizwa mkenge kwa kutokujua kwanini tunafanya vile. Kila kitu kinacho fanywa na binadamu kina maana kwake. Mungu alituumba weusi kwa sababu zake na hakukosea ( acheni mikorogo).
Wazo mcharuko
1. Kuna wanawake wanafikiri kuvaa suruali ni kwenda na wakati (Ati uonekana ni mwanamke wa kizungu) na si vazi ambalo wanalivaa kwa sababuza msingi wakati huohuo kuna wanaume kamwe hawata oa mwanamke ambaye anava suruali wakiamini kuwa ni ishara ya tabia mbaya.
2. Kuna wanawake wanaamini kuto vaa kimini ni kuto kwenda na wakati na kuna wanaume wapo wanao amini mwanamke akivaa kimini mi mhuni (Ati nafsi zao zinaumizwa).
3. Kuna binadamu wanaamini wakijichubua ndio wanakuwa binadamu wa kweli ( wazungu).
4. Wapo vijana ambao wanaamini kutofanya mapenzi hadi ndoa ni ushamba mkubwa .
5. Kuna binadamu wanaamini kuwa kutoka ndani ya ndoa ni kitu cha kawaida ili mradi mume au mke asijue eti kwa kuwa kwa wazungu sio issue ( eti wazungu ndio walivyo).
6. Kubwa zaidi ni kuwa tumefika hadi kutojali watoto wanapo kosea na kujiingiza katika mapenzi na hata tumeona ni kitu cha kawaida . Sipingani na hio ila kwa ni tusiwe fundishe moral values wajue kabisa kufanya mapenzi hairuhusiwi hadi aoe au aolewe.
Yapo mengi ambayo kutokana na kuzing'ang'ania desturi za kigeni tumejikuta tukifanya mambo ambayo hata wenyewe tunao wasingizia wanafanya hawafanyi.
Je Tunacho kiona katika media ni kweli ndio uhalisia wa maisha tunayo takiwa tuyaishi au ni kweli kwamaba mara nyingi vitu vya onyo onyo ndivyo vinavyo pendwa na na jamii.