Synthesizer
JF-Expert Member
- Feb 15, 2010
- 11,143
- 18,774
Sisi ni watanzania katika nchi huru
Tumechoka kuonewa na polisi
Tumechoka kubambikiwa kesi za uongo
Tumechoka kupigwa ili kutuliza frustration za ugumu wa maisha ya askari
Tumechoka kutozwa rushwa kwa kila jambo linalohitaji huduma ya polisi
Tumechoka kusikia uongo wa polisi kila wanapokiuka haki zetu
Tumechoka kuwa chanzo cha kitoweo cha askari wa usalama barabarani
Tumechoka kuzika ndugu zetu na rafiki zetu wanaofia mikononi mwa polisi
Tumechoka kuuguza majeraha yanayotokana na polisi
Tumechoka kukataliwa haki yetu ya dhamana kwa ubinafsi wa polisi badala ya sheria
Tumechoka polisi kutumiwa na matajiri wachache kutunyima haki zetu
Tumechoka kuona polisi wakigeuzwa kuwa chombo cha ukatili cha wanasiasa
Tumechoka kuona polisi wakijifanya miungu wadogo katika kushughulika na raia
Tumechoka kuchukuliwa na polisi kama watu tusio na uwezo wa kufikiri
Tumechoka kuona haki zetu za kiraia zikiwekwa mikononi mwa polisi pasipo utashi wetu
Si unyonge wetu uliotufanya tukubali kuonewe na polisi muda wote huu, tuna nguvu ya wingi wetu
Si ujinga wetu unaotufanya tudhalilishwe na polisi katika nchi yetu wenyewe, tuna uvumilivu
Si umasikini wetu unaotufanya tuwavumilie polisi muda wote huu, tuna amani
Lakini sasa tunasema basi inatosha
Tumechoka kuonewa na polisi
Tumechoka kubambikiwa kesi za uongo
Tumechoka kupigwa ili kutuliza frustration za ugumu wa maisha ya askari
Tumechoka kutozwa rushwa kwa kila jambo linalohitaji huduma ya polisi
Tumechoka kusikia uongo wa polisi kila wanapokiuka haki zetu
Tumechoka kuwa chanzo cha kitoweo cha askari wa usalama barabarani
Tumechoka kuzika ndugu zetu na rafiki zetu wanaofia mikononi mwa polisi
Tumechoka kuuguza majeraha yanayotokana na polisi
Tumechoka kukataliwa haki yetu ya dhamana kwa ubinafsi wa polisi badala ya sheria
Tumechoka polisi kutumiwa na matajiri wachache kutunyima haki zetu
Tumechoka kuona polisi wakigeuzwa kuwa chombo cha ukatili cha wanasiasa
Tumechoka kuona polisi wakijifanya miungu wadogo katika kushughulika na raia
Tumechoka kuchukuliwa na polisi kama watu tusio na uwezo wa kufikiri
Tumechoka kuona haki zetu za kiraia zikiwekwa mikononi mwa polisi pasipo utashi wetu
Si unyonge wetu uliotufanya tukubali kuonewe na polisi muda wote huu, tuna nguvu ya wingi wetu
Si ujinga wetu unaotufanya tudhalilishwe na polisi katika nchi yetu wenyewe, tuna uvumilivu
Si umasikini wetu unaotufanya tuwavumilie polisi muda wote huu, tuna amani
Lakini sasa tunasema basi inatosha