Tumechoka kuonewa na Polisi

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,143
18,774
Sisi ni watanzania katika nchi huru
Tumechoka kuonewa na polisi
Tumechoka kubambikiwa kesi za uongo
Tumechoka kupigwa ili kutuliza frustration za ugumu wa maisha ya askari
Tumechoka kutozwa rushwa kwa kila jambo linalohitaji huduma ya polisi
Tumechoka kusikia uongo wa polisi kila wanapokiuka haki zetu
Tumechoka kuwa chanzo cha kitoweo cha askari wa usalama barabarani
Tumechoka kuzika ndugu zetu na rafiki zetu wanaofia mikononi mwa polisi
Tumechoka kuuguza majeraha yanayotokana na polisi
Tumechoka kukataliwa haki yetu ya dhamana kwa ubinafsi wa polisi badala ya sheria
Tumechoka polisi kutumiwa na matajiri wachache kutunyima haki zetu
Tumechoka kuona polisi wakigeuzwa kuwa chombo cha ukatili cha wanasiasa
Tumechoka kuona polisi wakijifanya miungu wadogo katika kushughulika na raia
Tumechoka kuchukuliwa na polisi kama watu tusio na uwezo wa kufikiri
Tumechoka kuona haki zetu za kiraia zikiwekwa mikononi mwa polisi pasipo utashi wetu

Si unyonge wetu uliotufanya tukubali kuonewe na polisi muda wote huu, tuna nguvu ya wingi wetu
Si ujinga wetu unaotufanya tudhalilishwe na polisi katika nchi yetu wenyewe, tuna uvumilivu
Si umasikini wetu unaotufanya tuwavumilie polisi muda wote huu, tuna amani

Lakini sasa tunasema basi inatosha
 
Unayosema ni kweli. Mimi nilipata kuishi jirani na nyumba ya maiti pale Muhimbili miaka ya 80-90 nilikuwa nashanga sana kuona polisi wakileta maiti pale karibu usiku kucha.Nilikuwa najiuliza kama ni ajali mbona sizisikii katika radio na kusoma katika magazeti? Sasa nimeamini polisi wanaua watu wengi bila taarifa kuwa wazi.
Haya mauaji ya Mwangosi yamedhihirisha haya, ushahidi wa picha halisi sio picha duka umeonyesha marehemu akiwa katikati ya polisi huku wakiwa wamekamata silaha na bado serikali inasema hawahusiki na kifo cha marehemu. Je ni watu wangapi wanafia mikononi mwa polisi bila kuwa na ushahidi angalau wa picha kama huu? na je kama wahusika wangekuwa kutoka chama tofauti na CCM wangesema hawahusiki na mauaji?
Hali kama hii inajenga chuki katika jamii na ndio maana katika nchi zenye matukio ya ugaidi mambo yalianza hivi hivi. Tuepushe nchi yetu kuingia katika machafuko yasiyo na sababu.
 
MTALIA MPAKA MTOE MACHOZI YA DAMU,dawa ya hawa polisi wetu ni kwa nguvu zote KULIBWAGA CCM mwaka 2015 na pia KUBADILISHA SHERIA KANDAMIZI!!
 
Sisi ni watanzania katika nchi huru
Tumechoka kuonewa na polisi
Tumechoka kubambikiwa kesi za uongo
Tumechoka kupigwa ili kutuliza frustration za ugumu wa maisha ya askari
Tumechoka kutozwa rushwa kwa kila jambo linalohitaji huduma ya polisi
Tumechoka kusikia uongo wa polisi kila wanapokiuka haki zetu
Tumechoka kuwa chanzo cha kitoweo cha askari wa usalama barabarani
Tumechoka kuzika ndugu zetu na rafiki zetu wanaofia mikononi mwa polisi
Tumechoka kuuguza majeraha yanayotokana na polisi
Tumechoka kukataliwa haki yetu ya dhamana kwa ubinafsi wa polisi badala ya sheria
Tumechoka polisi kutumiwa na matajiri wachache kutunyima haki zetu
Tumechoka kuona polisi wakigeuzwa kuwa chombo cha ukatili cha wanasiasa
Tumechoka kuona polisi wakijifanya miungu wadogo katika kushughulika na raia
Tumechoka kuchukuliwa na polisi kama watu tusio na uwezo wa kufikiri
Tumechoka kuona haki zetu za kiraia zikiwekwa mikononi mwa polisi pasipo utashi wetu

Si unyonge wetu uliotufanya tukubali kuonewe na polisi muda wote huu, tuna nguvu ya wingi wetu
Si ujinga wetu unaotufanya tudhalilishwe na polisi katika nchi yetu wenyewe, tuna uvumilivu
Si umasikini wetu unaotufanya tuwavumilie polisi muda wote huu, tuna amani

Lakini sasa tunasema basi inatosha

As long as jeshi la polisi wanaajili failures katika mitihani-div 4 and 0, then utendaji wapolisi hautabadilika. Ukiacha akina Kaqmuhanda ambao wanatafuta kuifurahisha CCM, with education naamini tunaweza kulibadilisha jeshi letu. lazima katiba itamke wazi kuhusu polisi na ukatili wao.
 
As long as jeshi la polisi wanaajili failures katika mitihani-div 4 and 0, then utendaji wapolisi hautabadilika. Ukiacha akina Kaqmuhanda ambao wanatafuta kuifurahisha CCM, with education naamini tunaweza kulibadilisha jeshi letu. lazima katiba itamke wazi kuhusu polisi na ukatili wao.

Ina maana kua na mapolisi failures ndio sababu ya kuwa chombo chenye mamlaka ya kuonea mpaka kuua raia??sio kwamba muundo na uongozi wao kua mbaya na kufuata matakwa ya wakubwa wao??? sio kuwa na serikali yenye kutumia vyombo vya usalama kwa maslai yao binafsi??sio sheria mbovu zinazowakinga wao kama vyombo husika vya ulinzi??
 
Ina maana kua na mapolisi failures ndio sababu ya kuwa chombo chenye mamlaka ya kuonea mpaka kuua raia??sio kwamba muundo na uongozi wao kua mbaya na kufuata matakwa ya wakubwa wao??? sio kuwa na serikali yenye kutumia vyombo vya usalama kwa maslai yao binafsi??sio sheria mbovu zinazowakinga wao kama vyombo husika vya ulinzi??

Yote hayo uliyoyasema yana mantiki kubwa, very true!. lakini mtu aliyeelimika, na sio mitulinga ya kwata, na songa mbele kuruta, anaweza aka-reason kuwa hili nisilifanye! Naamini aliyemuua mwangosi elimu yake ni duni, huwezi fanya hivyo kwa mtu ambaye uneshamdhibiti na ni mwandishi wahabari unamjua fika , hana silaha etc. Poor reasoning. Kumbambikia mtu kesi, sidhani kama university graduate polis anaweza fanya hivyo- I stand to be corrected, labda siwajui vizuri polis. Hawa wa chaspa mguu siwaamini hata! Moreover wengi wao bado ni darasa la saba!
 
Hatuna jeshi la polisi! IGP ni shemeji wa dhaifu! jeshi halina nidhamu! wanababimbikia watu kesi,Jeshi linanuka rushwa! kuingia kituo cha polisi bure kutoka na hela.Jeshi la polisi ni tawi la magamba!
 
Hatuna jeshi la polisi! IGP ni shemeji wa dhaifu! jeshi halina nidhamu! wanababimbikia watu kesi,Jeshi linanuka rushwa! kuingia kituo cha polisi bure kutoka na hela.Jeshi la polisi ni tawi la magamba!

Wakuu mie nimeathiriwa na utendaji wa Polisi kiasi kwamba kweli nina chuki na askari yeyote ninaemuona. Nadhani Watanzania wengi wana hisia kama zangu. Sasa hii ni hatari sana, kwa watu ambao twapaswa kuwaona Polisi kama walinda amani na usalama.

Juzi hapa kuna askari alinikamata na insurance iliyopita muda wake, maana nilikuwa nimejisahau, alinidai chochote nikamjibu wazi, kwamba ni heri aniandikie faini nikalipe isaidie mapato ya nchi hata kama ni mara kumi ya kiasi ambacho angetaka, kuliko kumpa yeye binafsi akatumie na familia yake! Nilisema hivi wazo la kwanza kichwani likiwa ni chuki yangu kwake binafsi kutokana na utendaji wa Polisi na si rushwa aliyotaka!

Iringa wanasema uhusiano wa polisi na waandishi wa habari umeharibika. Mie nasema uhusano wa Polisi na raia wa Tanzania kwa ujumla umeharibika!
 
Kuna askari waliombambikizia mama mjane kesi. Wakamptupa rumande bila kujali ukiwa alionao wa kufiwa na mumewe gafla aliyemwachia watoto saba akiwapo wa mwaka mmja na miezi. Mama huyo analilia rumande. Watoto wake wanasota bila baba wala mama. Mhusika wa kesi alitoa rushwa ya kutosha kwa polisi wakamwachia na kumchua huyu mjane maskini asiye na mtetezi na kumfungia badala ya yule mhusika.
Je hawa polisi waliofanya hiki kitendo watasalimika? Kilio cha huyu mjane ambaye amesotea rumande sasa ni mwezi wa tatu kitaliacha hili taifa katika usalama? Kwa uhakika hana cha kufanya isipokuwa kulia na kusali. Ipo siku moja kilio chake kitayafikia masikio ya mwuumba wake. Huyo Mwuumba aafanya nini kwa hawa waliomtendea unyama kama huu masikini huyu? Tusumbiri tuone kwani maandiko yanasema nitakisikia kilio cha majane na yatima. Polisi jiangalieni sana hii rushwa imewapeleka mbali mno!
 
Kuna askari waliombambikizia mama mjane kesi. Wakamptupa rumande bila kujali ukiwa alionao wa kufiwa na mumewe gafla aliyemwachia watoto saba akiwapo wa mwaka mmja na miezi. Mama huyo analilia rumande. Watoto wake wanasota bila baba wala mama. Mhusika wa kesi alitoa rushwa ya kutosha kwa polisi wakamwachia na kumchua huyu mjane maskini asiye na mtetezi na kumfungia badala ya yule mhusika.
Je hawa polisi waliofanya hiki kitendo watasalimika? Kilio cha huyu mjane ambaye amesotea rumande sasa ni mwezi wa tatu kitaliacha hili taifa katika usalama? Kwa uhakika hana cha kufanya isipokuwa kulia na kusali. Ipo siku moja kilio chake kitayafikia masikio ya mwuumba wake. Huyo Mwuumba aafanya nini kwa hawa waliomtendea unyama kama huu masikini huyu? Tusumbiri tuone kwani maandiko yanasema nitakisikia kilio cha majane na yatima. Polisi jiangalieni sana hii rushwa imewapeleka mbali mno!
Haya, jana tu nimeweka hii thread, leo tunasikia Ofisa Uhamiaji Mkoa wa Mwanza, Albert Buchafwe amenusurika kuuawa kwa risasi na Mkuu Msaidizi wa Kituo cha Polisi Nyakato, Abubakar Zebo. Halafu kwa ujinga usio kifani kama vile watanzania wote ni mambumbumbu wa kudanganywa kirahisi, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Leberatus Barlow, bila hata kumhoji alieyetaka kuwawa, anasema ana uhakika ni bahati mbaya kwani jeshi lake lilipata taarifa za Kiintelijensia za kuwapo kwa majambazi wakidaiwa kutumia gari sawa na la ofisa huyo. (Na kwa jinsi magari yanavyofanana Tanzania kama polisi wanashambulia gari kwa kuwa tu linafanana na wanalotafuta basi wao ni polisi mbumbumbu kuliko wote duniani)

Swali la msingi limeulizwa, tangu lini polisi wanatumia magari yao binafsi, kama Suzuki binafsi aliyokuwa nayo huyu Msaidizi wa Kituo cha Polisi Nyakato, Abubakar Zebo, kwenda kuweka mitego ya kuwakamata majambazi?

Buchafwe aliyetaka kuuwawa amesema wazi, kwamba huyu askari Abubakar Zebo ana uhusiano wa karibu na mkewe, ambaye wamekuwa na ugomvi naye pamoja na kesi ya kutalikiana mahakamani.

Yaani tuna jeshi la Polisi limefikia hatua kutumia silaha za dola kwa ajili ya kuua wananchi hadi kwa ajili ya ngono!!! Sijawahi kusikia ufilauni wa kiasi hiki.
 
Back
Top Bottom