kbm
JF-Expert Member
- Oct 5, 2012
- 5,222
- 1,670
Mwenyekiti wa Tume ya maoni ili kuweza kupata katiba mpya, amesema kuwa kwa wananchi wa Dar es salaam kutoa maoni yao ni katikati ya mwezi ujao. Pia amesema hawataweze kuwafikia kila mtu. Kwa maana hiyo, mimi na wewe tusipate nafasi ya kutoa maoni na dukuduku zetu ili kusaidia kuunda sheria zitakazo tuongoza kwa miaka ijayo. Natumaini wakati ni huu kuweka mikakati kuhakikisha kila mdau anatoa maoni yake, kama inawezekana naomba wanaJF tuwekewe kitufe cha kudumbukiza maoni yetu kiurahisi. Chakushangaza serikali iliweza kuwafikia raia wote watanzania wauchaguzi mkuu, pia wakati wa kuhesabu na zoezi la kuandikisha vitambulisho wote tulishirikishwa vizuri. Sasa inakuwaje jaji Warioba anatamka waziwazi kuwa hawatashirikisha wananchi wote, wakati huo anasema katiba hii ndiyo itumike katika mchakato wa uchaguzi mkuu 2015. Je hii ni sawa?