Mwakyembe, Wafanyakazi wa Mahakama Waliorudishwa Nyumbani watarudi kazini lini?

LTN USU WA MADOSO

JF-Expert Member
Sep 14, 2016
1,193
859
Ndugu wana jf nichukue nafasi hii kwa masikitiko makubwa sana yanayofanywa na wizara hii nyeti ya katiba na sheria ambayo ni kinyume na taratibu kanuni na maadili ya kazi

Mno tarehe 29/05/2016 tume ya utumishi wa mahakama iliwaita watu waliofaulu usaili kuripoti kazini tarehe hiyo 29 mwezi wa tano walianza kazi hao waajiriwa wapya ni mahakimu ,wasaidizi wa ofisi,walinzi,watunza kumbukumbu nk takribani watu 1500 tanzania nzima walisainishwa mikataba yote ya kazi na kuanza kufanya kazi hawa watu walikuwa wanafanya kazi mikoa mbalimbali nchini ilipofika tarehe 27/06/2016 walipewa barua za kusimamishwa kazi kwa mda usiojulikana

Waliamliwa kurudi nyumbani mpaka utaratibu mwingine utakapotolewa mpaka sasa miezi mitatu imepita serikali ipo kimya na hawa watu walikuwa na kazi zao kwenye mashirika binafsi baada ya kuwaita kazini waliacha kazi kwenye mashirika hayo na kuja serikalini wengine wakiwa na familia zao mpaka sasa wanataabika hawajui hatima yao mahakama ni chombo cha kutenda haki je?

Haki ya hawa watanzania iko wapi ?

Namuomba waziri mwenye dhamana kuliangalia suala hili ili hawa watu wajue hatima yao kama kazi bado wanayo au wafanya taratibu zingine maana wanaogopa hata kusaini mikataba wakihofia mda wowote watahitajika serikali saidieni hili sawa

Mungu ibabariki Wizara ya katiba na sheria Mungu ibariki Tanzania.
 
Kwa kuwa waathirika wanatoka katika kada au taaluma ya sheria kwa nini wasingefungua KESI kudai kuvunjiwa mkataba??
 
Kwa kuwa waathirika wanatoka katika kada au taaluma ya sheria kwa nini wasingefungua KESI kudai kuvunjiwa mkataba??
Wanafki wanajua sheria zote...taifa la wasomi wanafiki ndio tatizo fungua kesi komaeni nao tu.....unafki n more than ujinga aiseee......mwanasheria unadhulumiwa du
 
Wanafki wanajua sheria zote...taifa la wasomi wanafiki ndio tatizo fungua kesi komaeni nao tu.....unafki n more than ujinga aiseee......mwanasheria unadhulumiwa du
Its strange kwa sababu ukisha saini mkataba anayeuvunja anatakiwa alipe sasa tena hao ni mahakimu na wamesoma sheria wanaogopa nn? Au wana vyeti feki??
 
umajua kuna mambo mengine serikali inafanya lakini sijui kama rais angefanyiwa yeye angejisikiaje
 
Hivi ulisoma ili serikali ikuajiri? Mbona kuna nchi kama Uganda hamna ajira watu wanaishi. Kila anayesoma sheria anataka awe hakimu wa serikali?

Kweli baado tutailau serikali kwa wanaojifanya wana akili wakati hawana. Anzisha hata mradi wa kuchimba mitaro!!
 
1474305565703.jpg


Uchokozi huu
 
Mtoa post acha ubinafsi ilo tatizo ni la waajiriwa wapya wote kuanzia feb wamesimamishwa kupisha uhakiki na wala mwankyembe alimuhusu ilo n jambo la mkuu huo n uchochezi tuvute subra
 
Ndugu wana jf nichukue nafasi hii kwa masikitiko makubwa sana yanayofanywa na wizara hii nyeti ya katiba na sheria ambayo ni kinyume na taratibu kanuni na maadili ya kazi

Mno tarehe 29/05/2016 tume ya utumishi wa mahakama iliwaita watu waliofaulu usaili kuripoti kazini tarehe hiyo 29 mwezi wa tano walianza kazi hao waajiriwa wapya ni mahakimu ,wasaidizi wa ofisi,walinzi,watunza kumbukumbu nk takribani watu 1500 tanzania nzima walisainishwa mikataba yote ya kazi na kuanza kufanya kazi hawa watu walikuwa wanafanya kazi mikoa mbalimbali nchini ilipofika tarehe 27/06/2016 walipewa barua za kusimamishwa kazi kwa mda usiojulikana

Waliamliwa kurudi nyumbani mpaka utaratibu mwingine utakapotolewa mpaka sasa miezi mitatu imepita serikali ipo kimya na hawa watu walikuwa na kazi zao kwenye mashirika binafsi baada ya kuwaita kazini waliacha kazi kwenye mashirika hayo na kuja serikalini wengine wakiwa na familia zao mpaka sasa wanataabika hawajui hatima yao mahakama ni chombo cha kutenda haki je?

Haki ya hawa watanzania iko wapi ?

Namuomba waziri mwenye dhamana kuliangalia suala hili ili hawa watu wajue hatima yao kama kazi bado wanayo au wafanya taratibu zingine maana wanaogopa hata kusaini mikataba wakihofia mda wowote watahitajika serikali saidieni hili sawa

Mungu ibabariki Wizara ya katiba na sheria Mungu ibariki Tanzania.
huyo ndo rais shupavu tuliyemsubiri kwa miaka mingi hamna kubembeleza na anachukua maamzi magumu. kama vipi kachukueni majembe mashamba yako ya kutosha tu.
 
Hivi ulisoma ili serikali ikuajiri? Mbona kuna nchi kama Uganda hamna ajira watu wanaishi. Kila anayesoma sheria anataka awe hakimu wa serikali?

Kweli baado tutailau serikali kwa wanaojifanya wana akili wakati hawana. Anzisha hata mradi wa kuchimba mitaro!!
Hapa mkataba umevunjwa ndugu karibu kuwa muelewa na kidogo
 
Hakuna mikataba iliyovunjwa. Si kwamba wewe ndo unajua Tz pekee yako. Mimi nakaa na binti upande wa Afya. Alipokwenda kuripoti walimwambia asubiri kwanza ataitwa kuanza kazi. Tangu mwezi wa Tano yupo.

Kuitwa kazini si kuingia mkataba na serikali. Kumbuka hata wakiamua kuna kipindi cha probation wanaweza kukuondoa kwa sheria ya kuridhika na utendaji wako.

Hivyo basi, usindanganye watu kwa kuona unajua hayo pekee yako.

Ndo maana nikasema, nchi ambayo watu wanasoma ili waajiriwe na serikali siku zote inaleta shida. Hapa si kwamba naitetea serikali ila inahitajika kuaandaa mazingira ya vijana kujiajiri na si kukaa kwenye mitandao na kufanya kampeni za ajira hata kama ajira hazipo.
Hapa mkataba umevunjwa ndugu karibu kuwa muelewa na kidogo
 
KUNA WATU WALIAJIRIWA MWEZI WA TANO MWAKA HUU NDANI YA MAHAKAMA MBALIMBALI HAPA TANZANIA MAHAKIMU,WATUNZA KUMBUKUMBU ,WALINZI,MADREVA NK, WALIKUWA WAMESAINISHWA MIKATABA YA KAZI NA KUANZA KUFANYA KAZI TAKRIBANI MWEZI MZIMA WALIPEWA NA PESA ZA KUJIKIMU WAKAPANGA VYUMBA NA WAKALETA FAMILIA ZAO MIKOA MBALIMBALI YA TANZANIA BAADA YA KUFANYA KAZI MWEZI MMOJA WALIPEWA BARUA ZA KUSIMAMISHWA KAZI KWA MDA USIOJULIKANA MPAKA SASA WANA MIEZI MINNE WAPO NYUMBANI HUU NI UNYANYASAJI MKUBWA SANA KABLA HAWAJAWAITA KAZINI WATU WALIKUWA WANAFANYA KAZI PRIVATE SECTOR BAADA YA KUWAITA KAZINI WALIACHA KAZI SEKTA BINAFSI NA KUJA SERIKALINI KUFANYA KAZI HUU NI UNYANYASAJI WA HALI YA JUU SANA KAMA HIKI CHOMBO KINASIMAMIA HAKI KWANINI KISITENDE HAKI KWA HAWA WATUMISHI HATA KWA KUWAWEKA WAZI TU .
 
Tunaposema weka swiswism mbali na kiumbe chochote kile mtuelewe kuwa tuna maanisha na hatutanii,chama na watu wake ndiyo wametufikisha hapa tulipo toka uhuru zaidi ya miaka 55 hata mlo mmoja ni msamiati kwa wengi wetu.
Na bado ni ahadi ya kuwa watu wakaishi kama mashetani.....hii niTrailler bado hata Movie haijaanza.
 
Mkuu waambie wawe na subira kama alivyoimba bella na kassim over.
 
Back
Top Bottom