Elections 2010 Tume ya uchaguzi litazameni hili.

politiki

JF-Expert Member
Sep 2, 2010
2,376
1,507

KWENU TUME YA UCHAGUZI,
swala la mabango kuwa na picha za ikulu sio kitu muhimu sana ukilinganisha na maeneo mengine muhimu ambayo yanaweza kwa kiasi kikubwa kuchangia kushindwa kwa wagombea wengine. maeneo muhimiu ambayo ilibidi kuyafanyie kazi ili kuleta usawa katika uchaguzi ni kama haya.
SWALA LA VYOMBO VYA HABARI VYA UMMA vyombo vingi vya habari vya umma vimekuwa vikitagnaza zaidi kupendelea ccm wakati vyombo hivyo ni vya umma. chamsingi hapa ni kuakikisha mnakuwa na mtu maalum kuakikisha vyombo vya umma vinatoa equal time kwa kila chama.
SWALA LA PILI NI WAKUU WA WILAYA NA MIKOA KUTUMIA VYOMBO VYA SERIKALI KUIFANYIA KAMPENI CCM.
SWALA LA TATU NI LA MKE WA RAIS, Pesa anazotumia kwenye kampeni ni za ccm au zinatoka ikulu?? ni nani analipia safari zake za kumnadi mumewe??
WAKATI LIPUMBA AKILALA VIJIJINI akiwa mtwara analala hotelini kwa pesa zake LAKINI JK akiwa Mtwara atalala na kula IKULU KWA PESA ZA WANANCHI. HAPA hakuna usawa. NI KWELI RAIS INABIDI ALALE IKULU KWA AJILI YA USALAMA LAKINI ILIBIDI WAPINZANI NAO WAFIKIRIWE KWA KUWAWEZESHA KIFEDHA KULALA SEHEMU NYINGINE KWA GHARAMA ZA SERIKALI ILI KUJARIBU KULETA USAWA. GHARAMA ZA ULINZI WA RAIS ZINALIPWA NA WANANCHI LAKINI INABIDI ZILIPWE TU KWA AJILI YA KUWATUMIKIA WATU WOTE NA SIO KWENYE MIKUTANO YAKE YA CCM, HAPA ILIBIDI TUME IWE FAIR KWA KUWAFIKIRIA WAPINZANI KWA KULIPIA AU KUTOA RUZUKU ZA GHARAMA ZAO ZA ULINZI ILI KULETA USAWA KWANI TUNGELIPENDA RAIS AENDELEE NA ULINZI WAKE LAKINI WAKATI HUO HUO WAPINZANI NAO WAKIFIKIRIWA. KINACHOFANYIKA HIVI SASA AMBAPO RAIS ANATUMIA PESA ZA WALIPA KODI KWA AJILI YA KAMPENI ZAKE BINAFSI WAKATI WAPINZANI WAKE HAWANA HIYO NAFASI KWA SABABU HAWAKO IKULU. HII SIO HAKI KAMA KWELI TUNANIA YA KULETA DEMOKRASIA YA KWELI.
 
Back
Top Bottom