Raia Fulani
JF-Expert Member
- Mar 12, 2009
- 10,877
- 2,758
Leo nimeona gari ya mh Hawa Ghasia-mbunge na waziri (kumbe nao hukaa kwenye foleni). Kwenye kava ya tairi ya spea pameandikwa President's Office Planning Commission-National Think Tank. Nilikuwa najiuliza, think tank ya taifa iko wapi? Na kuiita hii tume 'think tank' ni sawa? Hii tume ina 'vichwa' vyote vinavyohitajika na taifa? La msingi la kujiuliza ni kama wanakidhi vigezo vya kuitwa hivyo. Hii tume ni mwarobaini wa matatizo yanayolikabili taifa? Tulipokabiliwa na matatizo ya uchaguzi mkuu na makandokando yake tume ilifanya nini. Tunapokabiliwa na matatizo ya kiuchumi tume inafanya nini. Tunapokabiliwa na gharama na ukosefu wa umeme tume imefanya nini. Wasomi na wanazuoni wetu wamehusishwaje na hii tume katika kuleta ufumbuzi wa matatizo yanayotukabili kama taifa? Au ndio yale yale ya maisha bora kwa kila mtanzania kwa ari zaidi, nguvu zaidi na kasi zaidi