MrFroasty
JF-Expert Member
- Jun 23, 2009
- 1,195
- 590
Fredy Azzah
TUME ya Maadi ya Utumishi wa Umma, imesema ripoti ya mali ya watumishi wa umma, itakamilika baada ya wiki mbili zijazo.
Akizungumza na Mwananchi jana, Ofisa habari wa tume hiyo, Ally Mataula, alisema ripoti kutoka katika mikoa yote zitatumwa makao makuu ya tume hiyo yaliyopo jijini Dar es Salaam, baada ya kukaguliwa.
Alisema wiki mbili kuanzia sasa, taarifa kutoka katika ofisi za kanda mbalimbali nchini, zitakuwa zimekwisha kamilika na kupelekwa makao makuu.
Ofisi za tume hiyo zimegawanyika katika Kanda ya Kaskazini (Arusha), Kanda ya Kati (Dodoma) na Kanda ya Kusini (Mtwara).
Hali kadhalika Kanda ya Ziwa (Mwanza), Kanda ya Juu Kusini (Mbeya) na Kanda ya Mashariki ( Dar es Salaam).
"Kutokana na uchache wetu, zoezi la kukagua ujazaji wa taarifa hizi utachukua muda kama wiki mbili hivi, ukaguzi huo utahusisha kuangalia kama kiongozi amejaza kama ilivyotakiwa kisheria.Taarifa zilizopo katika ofisi zetu mbalimbali za kanda, zitaletwa hapa baada ya kukaguliwa huko katika kanda," alisema Mataula.
Alisema kwa wale ambao hawatarejesha fomu hizo, watachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria ikiwa ni pamoja na kufukuzwa kazi, kushauriwa kustaafu, kushushwa cheo ama kuonywa.
Alisema baadhi ya masharti yanayopaswa kutimizwa na mwananchi anayetaka kukagua ripoti hizo kwanza ni kutoa taarifa kwa kamisha kuhusu malalamiko yake juu kiongozi husika.
Hali kadhalika kulipa ada ya Sh1,000.
Alisema endapo kamishina hatoridhika na sababu zilizotolewa na mwananchi anayetaka kukagua mali za kiongozi huyo, anaweza kukataa ombi hilo.
Kwa mujibu wa Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma Na.3 ya mwaka 1995 (pamoja na marekebisho ya mwaka 2002), kiongozi wa umma anatakiwa kutangaza mali zake katika kipindi cha siku 30 baada ya kupewa wadhifa, kila mwisho wa mwaka na mwisho wa kutumikia wadhifa wake.
Sheria inamtaka kiongozi wa umma kumpelekea kamishna tamko la maandishi katika hati rasmi, linaloorodhesha mali zake.
Sheria hiyo pia inabainisha kuwa masharti katika sheria hiyo yatakuwa ni sehemu ya maadili ya viongozi wa umma kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri ya Muungano.
Chanzo:mwananchi
TUME ya Maadi ya Utumishi wa Umma, imesema ripoti ya mali ya watumishi wa umma, itakamilika baada ya wiki mbili zijazo.
Akizungumza na Mwananchi jana, Ofisa habari wa tume hiyo, Ally Mataula, alisema ripoti kutoka katika mikoa yote zitatumwa makao makuu ya tume hiyo yaliyopo jijini Dar es Salaam, baada ya kukaguliwa.
Alisema wiki mbili kuanzia sasa, taarifa kutoka katika ofisi za kanda mbalimbali nchini, zitakuwa zimekwisha kamilika na kupelekwa makao makuu.
Ofisi za tume hiyo zimegawanyika katika Kanda ya Kaskazini (Arusha), Kanda ya Kati (Dodoma) na Kanda ya Kusini (Mtwara).
Hali kadhalika Kanda ya Ziwa (Mwanza), Kanda ya Juu Kusini (Mbeya) na Kanda ya Mashariki ( Dar es Salaam).
"Kutokana na uchache wetu, zoezi la kukagua ujazaji wa taarifa hizi utachukua muda kama wiki mbili hivi, ukaguzi huo utahusisha kuangalia kama kiongozi amejaza kama ilivyotakiwa kisheria.Taarifa zilizopo katika ofisi zetu mbalimbali za kanda, zitaletwa hapa baada ya kukaguliwa huko katika kanda," alisema Mataula.
Alisema kwa wale ambao hawatarejesha fomu hizo, watachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria ikiwa ni pamoja na kufukuzwa kazi, kushauriwa kustaafu, kushushwa cheo ama kuonywa.
Alisema baadhi ya masharti yanayopaswa kutimizwa na mwananchi anayetaka kukagua ripoti hizo kwanza ni kutoa taarifa kwa kamisha kuhusu malalamiko yake juu kiongozi husika.
Hali kadhalika kulipa ada ya Sh1,000.
Alisema endapo kamishina hatoridhika na sababu zilizotolewa na mwananchi anayetaka kukagua mali za kiongozi huyo, anaweza kukataa ombi hilo.
Kwa mujibu wa Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma Na.3 ya mwaka 1995 (pamoja na marekebisho ya mwaka 2002), kiongozi wa umma anatakiwa kutangaza mali zake katika kipindi cha siku 30 baada ya kupewa wadhifa, kila mwisho wa mwaka na mwisho wa kutumikia wadhifa wake.
Sheria inamtaka kiongozi wa umma kumpelekea kamishna tamko la maandishi katika hati rasmi, linaloorodhesha mali zake.
Sheria hiyo pia inabainisha kuwa masharti katika sheria hiyo yatakuwa ni sehemu ya maadili ya viongozi wa umma kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri ya Muungano.
Chanzo:mwananchi