rifwima
JF-Expert Member
- Apr 21, 2010
- 507
- 212
Habari wan JF
Mimi ni Mhitumu wa shahada ya kwanza Chuo kikuu cha Dar es Salaam. Baada ya masomo ya degree yangu ya kwanza nikapata kazi Iringa. Katika kuangalia mstakabali wa kujiendeleza nikaamua kujoin na kusoma Postgraduate Chuo Kikuu cha Tumaini - Iringa.
Mwaka jana 29[SUP]th[/SUP] October 2011, niligraduate Tumaini University. Vifuatavyo ni baadhi ya vitu ambavyo vinanifanaya ni discredit chuo hiki:
Nilijaribu kufuatilia kujua utaratibu na namna wanavyofanya kazi pale Tumaini; haya yalijitokeza:
Naomba kuwasilisha, mwenye hoja tofauti kuhusu chuo hiki, na vyuo vingine vya namna hii Tanzania huu ndo wakati wake, jimwage hapa jamvini.
Naomba ujikite kwenye hoja za msingi, siyo umbea na utani!!!!!.
Mimi ni Mhitumu wa shahada ya kwanza Chuo kikuu cha Dar es Salaam. Baada ya masomo ya degree yangu ya kwanza nikapata kazi Iringa. Katika kuangalia mstakabali wa kujiendeleza nikaamua kujoin na kusoma Postgraduate Chuo Kikuu cha Tumaini - Iringa.
Mwaka jana 29[SUP]th[/SUP] October 2011, niligraduate Tumaini University. Vifuatavyo ni baadhi ya vitu ambavyo vinanifanaya ni discredit chuo hiki:
- Toka mwaka jana October, 2011 nilitakiwa (Tulitakiwa) niwe/tuwe tumepewa award certificates na Zawadi (Fedha) katika fani mbalimbali lakini mpaka dakika hii hakuna aliyepewa hizo awards. Nimefanya michakato ya hapa na pale kufuatilia hii kitu kwa wahusika, imeshindikana. Haya ni kati ya majawabu nilopewa (i) Njoo wiki ijayo nilijibiwa more than twice (ii) Aliyekuwa anashughulikia mwanzo kabadilishiwa ofisi (Kitengo) (iii) Anayeprint kasafiri (iv) Printer inamatatizo (iv) Vyeti vilikosewa so vinaprintiwa upya (v) Nipe No yako vikiwa tayari ntakujulisha. Niliargue nao sana na kuwapa live on how the University suppose to be called Shule ya Kata na wala siyo Chuo kikiuu (Cause vyuo kikuuu hakuna upuuzi kama huo).
- Mda wa kuchukua transcripts ulipofika nilijongea nikiwa na vitu vyote vinavyohitajika. Majibu yalikuwa kama yale yale ya juu. Nikamface DPAA ni kaargue naye kwa mbali akaelewa hasa nilipomwambia (Haya mnayotufanyia ndo tunawasaidia kuwatangazia chuo chenu kwamba ndo huduma zenu ziko hivyo). Akaimove Issue siku hiyohiyo nikapata transcript lakini ikiwa na mapungufu yafuatayo (i) Kuna kozi ilikuwa imekosewa kabisa kuandikwa jina lake, jina la programme pia likiwa limekosewa. Pamoja na hayo yote transcript ikawa imesainiwa na DPAA pamoja na Provost..They assented the tracscipt. Mimi niliona hayo makosa mara tu nilipoishika mkononi. Nikajaribu kufanya mpango namna ya kurekebisha makosa yale, ikarekebishwa lakini ikatoka ikiwa na kosa jingine jipya kabisa. Nilichoka kabisa alafu nikajilaamu sana kwa nini nimesoma chuo cha ubabaishaji namna hii especially at administrative level? Watu tunaamua kusoma kwa malengo, nakupata matokea mapema ni kitu cha msingi sana kwa mwanafunzi yeyote. I am not proud to be amongst the Tumaini University Graduates, because toka nigraduate bado sijapata nilichointend. Kwa sababu pamoja na mambo mengine qualifications zangu Tumaini pia ni sehemu kubwa ya CV yangu kukamilisha mambo mengine ikiwemo kuendlea na masomo anywhere in this World.
- Baada ya kufanya clearance chuo kinatakiwa kukulipe TZS 50,000 kupita CRB or NBC account ya mwanafunzu husika. Mpaka ninapoandika hakuna kitu. Ubabaishaji wa kutisha. Mambo kama haya ni lazima yakome kwenye vyuo vyetu.
Nilijaribu kufuatilia kujua utaratibu na namna wanavyofanya kazi pale Tumaini; haya yalijitokeza:
- Ajira zinapewa kindugu na efficiency ya mtu katika kazi haingaliwi kabisa (mfano, ofisi inayoshughulikia transcripts na certificates, makosa kila wakati? Siyo ishara njema kwa chuo. Ukiwa mhehe no problem you have an employment at Tumaini University – Iringa College. Angalizo, kwenye fani kama mathematics na Computer might not be the case.
- Accountability ya ufanyaji kazi haipo kabisa kwa sababu ya ndugu kushindwa kunyosheena mikono. Kila mtu anajifanyia mambo yake tu, ukienda kwa huyu ukitegemea ni mkubwa atamuwajibisha huyu...wapi,ndo kwanza anafurahi na danadana zinaendlea.
Naomba kuwasilisha, mwenye hoja tofauti kuhusu chuo hiki, na vyuo vingine vya namna hii Tanzania huu ndo wakati wake, jimwage hapa jamvini.
Naomba ujikite kwenye hoja za msingi, siyo umbea na utani!!!!!.