- Thread starter
- #61
Naomba kupima uelewa wako.
Mwiguli nchemba aligawa pikipiki jimboni kawe za nini!!!
Epa gua penaazutyuuswa neelasi ka sika nugunua ne kenaazushanelelia,
munidyoolo nouga "laa uu uluuu uuu"
Uelewa wangu ni mkubwa sana Jogi, just PM me. Kikubwa sikatai kwamba hatakiwi kwenda kule ila kumbuka tayari walishakwaruzana Bungeni na wana kesi tayari sasa ile kwenda kwa Mwigulu kwa wakati huu ni kama kuchochea moto wa ugomvi kwa petroli. Ukweli uliopo ni kweli kabisa polisi walijitahidi sana kuwalinda akina Mnyika, hiyo ni kweli kabisa kwa sababu licha ya kuongea na askari aliyekuwepo pale nimeongea hata na mzee mmoja jirani sana na nyumbani kwa mwl ambapo mauaji yalifanyikia. Ukweli CCM watakuwa wameanzisha fujo za SIKU HIYO, lakini sio kwamba hiyo ilianzia hapo. Mnyika hakutumia hekima, na naamini toke ameshinda ile kesi ya ubunge Mnyika amekuwa na mambo ya juu juu tu, mimi nina marafiki waliompigia kura na wanampenda sana lakini wanakubali kwa sasa anaokesea.