Ndugu yangu ambaye ni polisi aliyeshiriki kulinda mkutano wa CHADEMA Ndago- Singida amelalamikia sana lawama zinazorushwa kwao kuwa hawakuchukua hatua zozote za kuwalinda CHADEMA.
Kwa mujibu wake anasema kazi waliyoifanya ni kubwa kuliko inavyofikiriwa kwani ni kweli walishapata taarifa kuwa CDM wanakwenda kumtukana Mwigulu na vijana wa CCM walikuwa wamejiandaa kwamba matusi yakirushwa tu wangejibu mapigo. Ilivyokuwa ni kweli vijana wa CCM walikuwepo mkutanoni na ilipotokea Mwikabe kuanza kurusha matusi wengi wakachukia sana na kuanza kulalama Kinyiramba "mukue, "mukue", "mukue", "mukue", wakimaanisha "apigwe" "apigwe", "apigwe", "apigwe".
Hivyo polisi walijitahidi sana kuzuia wale vijana wa CCM wasiwadhuru viongozi wa CHADEMA waliokuwepo pale akiwepo Mnyiramba mwenzao Mayu Dr Kitila Mkumbo. Ndugu yangu alishangaa sana baadaye kuona kundi la vijana wa CHADEMA waliokwenda kuwalinda ndiyo wanafanya fujo kwa kuwakimbiza wenzao na kwenda kumwuua mmoja nyumba ya jirani na wengine wawili kujeruhiwa vibaya sana.
Ila sasa kibao kinawarudia wao polisi eti walishindwa kulinda mkutano wa CHADEMA, ukweli anasema wasingefanya kazi yao wale viongozi wa CHADEMA wangedhurika sana. Kwake yeye hatakuwa tayari kulinda mkutano wa CHADEMA tena.
Source: Mawasiliano yangu na askari ndugu yangu aliyekuwepo kulinda mkutano wa CHADEMA Ndago - Singida.
Kwa mujibu wake anasema kazi waliyoifanya ni kubwa kuliko inavyofikiriwa kwani ni kweli walishapata taarifa kuwa CDM wanakwenda kumtukana Mwigulu na vijana wa CCM walikuwa wamejiandaa kwamba matusi yakirushwa tu wangejibu mapigo. Ilivyokuwa ni kweli vijana wa CCM walikuwepo mkutanoni na ilipotokea Mwikabe kuanza kurusha matusi wengi wakachukia sana na kuanza kulalama Kinyiramba "mukue, "mukue", "mukue", "mukue", wakimaanisha "apigwe" "apigwe", "apigwe", "apigwe".
Hivyo polisi walijitahidi sana kuzuia wale vijana wa CCM wasiwadhuru viongozi wa CHADEMA waliokuwepo pale akiwepo Mnyiramba mwenzao Mayu Dr Kitila Mkumbo. Ndugu yangu alishangaa sana baadaye kuona kundi la vijana wa CHADEMA waliokwenda kuwalinda ndiyo wanafanya fujo kwa kuwakimbiza wenzao na kwenda kumwuua mmoja nyumba ya jirani na wengine wawili kujeruhiwa vibaya sana.
Ila sasa kibao kinawarudia wao polisi eti walishindwa kulinda mkutano wa CHADEMA, ukweli anasema wasingefanya kazi yao wale viongozi wa CHADEMA wangedhurika sana. Kwake yeye hatakuwa tayari kulinda mkutano wa CHADEMA tena.
Source: Mawasiliano yangu na askari ndugu yangu aliyekuwepo kulinda mkutano wa CHADEMA Ndago - Singida.