Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,475
- 39,991
Mongella: Sheria ya Gharama za Uchaguzi itekelezwe kwa umakini
Mwandishi Wetu
Mbunge wa Ukerewe, Dk. Getrude Mongella, ametaka busara itumike katika kutekeleza Sheria ya Gharama za Uchaguzi, vinginevyo wagombea watatengwa na jamii.
Mongella alisema hayo baada ya Kamanda wa Tasisi ya Kuzuia na Kupambana Rushwa (Takukuru) Wilaya ya Ukerewe, Leonidas Rugemalila, na Msimamizi wa Uchaguzi wa wilaya hiyo, Dk. Leonard Masale, kuwasilisha mada zao kuhusu sheria hiyo katika kikao cha kawaida cha Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilayani Ukerewe.
Alisema kifungu kinachokataza mgombea kukusanya watu popote na hata nyumbani kwake kitawanyima haki ya wagombea kutembelewa na kutembelea wananchi na hasa majirani kwa hofu ya kuadhibiwa na sheria hiyo.
Akitoa mfano, Dk. Mongella alisema kwa kawaida anapokuwepo nyumbani kwake, watu humtembelea kwa ajili ya kusalimia na kwamba wakati mwingine unaweza kukuta zaidi ya mtu mmoja na kwamba wakati mwingine hula nao chakula hivyo, kwa hali ya sasa kitendo hicho kinaweza kutafsiriwa kuwa kinavunja sheria hiyo.
Mbunge huyo alivitaka vyombo vinavyosimamia sheria hiyo hasa maafisa wa Takukuru kuwa makini na kutumia busara wakati wanatekeleza majukumu yao ili kuepuka kuwachukulia watu waio na makosa na kuongeza kuwa ni vyema elimu hiyo ikatolewa hadi ngazi ya chini ili wananchi waielewe.
Akiwasilisha mada, Rugemalila alisema Takukuru imejiandaa kukabiana na vitendo vya rushwa katika uchaguzi mkuu ujao ikiwa ni pamoja na katika mchakato wa kuwapata wagombea wa CCM na kuwataka wote wenye mipango hiyo kuachana nayo ili kuepuka mkono wa sheria.
Kwa upande wake, Dk. Masale aliwataka wanachama wa vyama vya siasa kuwa makini na watu wanaodaiwa kupita maeneo tofauti nchini wakigawa kadi za vyama vya siasa hasa CCM.
Alisema kamati yake itakuwa na watu wawili kila kata na kuwataka wagombea kusoma sheria hiyo na kuielewa ili kuepuka kufanya makosa na hatimaye kuondolewa katika uchaguzi.
NIPASHE
My Take:
Mmezidi Ubishi, wabunge nyinyi, kulalamika mlalamike nyinyi.. tuliwaimbia na kuwapigia kelele hii sheria mbovu mkaizunguka kwa mbwembwe kama watu wanaomzunguka mganga wa kienyeji.. sasa wacha igeuke iwanyofoe ndio mkome. Inakuwaje mtunga sheria anailalamikia sheria ambayo alikuwa na uwezo wa kuifanyia mabadiliko!
Mwandishi Wetu
Mbunge wa Ukerewe, Dk. Getrude Mongella, ametaka busara itumike katika kutekeleza Sheria ya Gharama za Uchaguzi, vinginevyo wagombea watatengwa na jamii.
Mongella alisema hayo baada ya Kamanda wa Tasisi ya Kuzuia na Kupambana Rushwa (Takukuru) Wilaya ya Ukerewe, Leonidas Rugemalila, na Msimamizi wa Uchaguzi wa wilaya hiyo, Dk. Leonard Masale, kuwasilisha mada zao kuhusu sheria hiyo katika kikao cha kawaida cha Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilayani Ukerewe.
Alisema kifungu kinachokataza mgombea kukusanya watu popote na hata nyumbani kwake kitawanyima haki ya wagombea kutembelewa na kutembelea wananchi na hasa majirani kwa hofu ya kuadhibiwa na sheria hiyo.
Akitoa mfano, Dk. Mongella alisema kwa kawaida anapokuwepo nyumbani kwake, watu humtembelea kwa ajili ya kusalimia na kwamba wakati mwingine unaweza kukuta zaidi ya mtu mmoja na kwamba wakati mwingine hula nao chakula hivyo, kwa hali ya sasa kitendo hicho kinaweza kutafsiriwa kuwa kinavunja sheria hiyo.
Mbunge huyo alivitaka vyombo vinavyosimamia sheria hiyo hasa maafisa wa Takukuru kuwa makini na kutumia busara wakati wanatekeleza majukumu yao ili kuepuka kuwachukulia watu waio na makosa na kuongeza kuwa ni vyema elimu hiyo ikatolewa hadi ngazi ya chini ili wananchi waielewe.
Akiwasilisha mada, Rugemalila alisema Takukuru imejiandaa kukabiana na vitendo vya rushwa katika uchaguzi mkuu ujao ikiwa ni pamoja na katika mchakato wa kuwapata wagombea wa CCM na kuwataka wote wenye mipango hiyo kuachana nayo ili kuepuka mkono wa sheria.
Kwa upande wake, Dk. Masale aliwataka wanachama wa vyama vya siasa kuwa makini na watu wanaodaiwa kupita maeneo tofauti nchini wakigawa kadi za vyama vya siasa hasa CCM.
Alisema kamati yake itakuwa na watu wawili kila kata na kuwataka wagombea kusoma sheria hiyo na kuielewa ili kuepuka kufanya makosa na hatimaye kuondolewa katika uchaguzi.
NIPASHE
My Take:
Mmezidi Ubishi, wabunge nyinyi, kulalamika mlalamike nyinyi.. tuliwaimbia na kuwapigia kelele hii sheria mbovu mkaizunguka kwa mbwembwe kama watu wanaomzunguka mganga wa kienyeji.. sasa wacha igeuke iwanyofoe ndio mkome. Inakuwaje mtunga sheria anailalamikia sheria ambayo alikuwa na uwezo wa kuifanyia mabadiliko!