hasan124
JF-Expert Member
- Jan 2, 2012
- 716
- 128
Katika ule muendelezo wa Kuweweseka na jinamizi la kumfukuza Mhe. HAMAD Rashid Mohamed, Mbunge wa Wawi kupitia CUF, Makamu Mwenyekiti wa chama hicho Mzee Machano ameibuka na kusema kwamba walishinikizwa na Katibu Mkuu akishirikiana na Kaimu wake kumfukuza MHE. HAMAD.
Habari hizi za ndani zimedai kwamba makubaliano hayakuwa kufukuza Bali ni kutoa onyo tu, ila hali ilikuja kubadilika ghafla kabla kikao hicho hakijaanza pale Masons Hotel mjini Zanzibar, ambapo shinikizo Hilo la Katibu na Mpambe wake Jusa kuwazidi wajumbe waliohudhuria kikao hicho cha tar.04-01-2012. Shinikizo ambalo ndilo lililopelekea hata kura za kuwafukuza MHE. HAMAD na wenzake kuwa ni za kunyanyua MKONO juu na kuhesabiwa wakihofu endapo watapiga kura za Siri lengo lisingetimia.
Habari hizi za ndani zimekuja siku chache baada ya Mwenyekiti wa Chama Taifa Prof. I. Lipumba kupokewa kwa gharama Kubwa ambazo zingeiwezesha CCM B kuingia kwenye uchaguzi huko Arumeru, Jambo hili linalotafsiriwa na wajuzi wa mambo kuwa ni moja kati ya Matumizi mabaya ya raslimali watu na fedha kwani mapokezi hayawezi kuipa ushindi hata wa udiwani CUF almaarufu Kama CCM B bali imejikuta ikipata gharama zaidi za kuuguza majeruhi waliopata ajili katika mapokezi HAYO.
Inapotokea chama cha siasa chenye miaka ishirini toka kusajiliwa, ni sehemu ya serikali katika upande mmoja wa Nchi, kinapata ruzuku na michango ya wabunge wake zaidi ya thelathini ambao huchanga zaidi ya shilingi million moja kwa mwezi kila mmoja lakini kinashindwa kushiriki uchaguzi mdogo kwa kisingizio chochote, hapo ni kuonyesha mwisho wa chama chenyewe.
Kwa maoni yangu CUF wanatakiwa watambue kwamba Uhai wa Chama haupimwi kwa Maandamano au Mapokezi Bali Matokeo ya Uchaguzi, na ni vyema watu wajue aliyepokelewa ni Profesa Lipumba sio CUF kwa kuthibitisha hili asafiri kiongozi mwingine halafu waandae HAYO mapokezi tuone.
Source: Rest in peace.
Habari hizi za ndani zimedai kwamba makubaliano hayakuwa kufukuza Bali ni kutoa onyo tu, ila hali ilikuja kubadilika ghafla kabla kikao hicho hakijaanza pale Masons Hotel mjini Zanzibar, ambapo shinikizo Hilo la Katibu na Mpambe wake Jusa kuwazidi wajumbe waliohudhuria kikao hicho cha tar.04-01-2012. Shinikizo ambalo ndilo lililopelekea hata kura za kuwafukuza MHE. HAMAD na wenzake kuwa ni za kunyanyua MKONO juu na kuhesabiwa wakihofu endapo watapiga kura za Siri lengo lisingetimia.
Habari hizi za ndani zimekuja siku chache baada ya Mwenyekiti wa Chama Taifa Prof. I. Lipumba kupokewa kwa gharama Kubwa ambazo zingeiwezesha CCM B kuingia kwenye uchaguzi huko Arumeru, Jambo hili linalotafsiriwa na wajuzi wa mambo kuwa ni moja kati ya Matumizi mabaya ya raslimali watu na fedha kwani mapokezi hayawezi kuipa ushindi hata wa udiwani CUF almaarufu Kama CCM B bali imejikuta ikipata gharama zaidi za kuuguza majeruhi waliopata ajili katika mapokezi HAYO.
Inapotokea chama cha siasa chenye miaka ishirini toka kusajiliwa, ni sehemu ya serikali katika upande mmoja wa Nchi, kinapata ruzuku na michango ya wabunge wake zaidi ya thelathini ambao huchanga zaidi ya shilingi million moja kwa mwezi kila mmoja lakini kinashindwa kushiriki uchaguzi mdogo kwa kisingizio chochote, hapo ni kuonyesha mwisho wa chama chenyewe.
Kwa maoni yangu CUF wanatakiwa watambue kwamba Uhai wa Chama haupimwi kwa Maandamano au Mapokezi Bali Matokeo ya Uchaguzi, na ni vyema watu wajue aliyepokelewa ni Profesa Lipumba sio CUF kwa kuthibitisha hili asafiri kiongozi mwingine halafu waandae HAYO mapokezi tuone.
Source: Rest in peace.