Tulipokuwa primary,unakumbuka?

nakumbuka shule niliyosoma kaka mkuu na dada mkuu walikuwa na ukaribu, wakati ule kulikuwa hakuna habari za boyfriend na girl friend, tulikuwa tunasema wachumba,....(joke)
 
hahahahaha
sio kma nacheka ila nalia kwa sweet memories za shule.
nakumbuka mara ya kwanza kuvaa chupi ilikuwa nikiwa njuka na chupi maarufu ilikuwa VIP ambayo ukiwa unasukuma soka ikakatika basi itapanda hadi kifuani....

nakumbuka pia ile style ya kuzungusha mkono iliniathiri mno hata mie na ingawa nilikomaa nao nikaingia class kinguvu bila kuandikishwa nilisota darasa la kwanza miaka mitatu (lakini bado naipenda Tanzania).

Kwa wale ambao hatukuwa mamonita najua mnakumbuka matumizi ya upupu na maji ya betri.... ila nilikuwa kiongozi bora sekondari walimu walilia tulipokuwa tunawaaga
 
nimekumbuka mbali sana nilikuwa na safari buti nilizivaa kuanzia darasa la pili hadi la nne haziishi siku moja nikavizia madingi wametoka nikaenda kukitupa kimoja katika shimo la maji machafu ili ninunuliwe chachacha za Burundi.
 
Oyaa mnakakumbuka kamchezo flani kachafu na kakifisadi lakini ka kiufundi kakuweka kioo chini ya akina dada???????? Kuna jamaa alimwekea mwalimu (wale wa mazoezi) siku hiyo ilikuwa kama jehanamu darasa zima tulilambwa fimbo kama mbwa mwizi
 
Kuna chupi zilikuwa na kichuma kwa mbele, sijui kama mnakumbuka. siku moja ilibidi nichukue ya brother wangu baada ya kuchoka kusubiri kununuliwa na mzee. halafu vipi ile miswaki ya miti, kila asubuhi unakwanyua wakati wa kwenda shule, kulikuwa hakuna matumizi ya maji hapo mate yako yalikuwa yanatosha.

Hiyo ya kuwawekea vioo wanasichana ilikuwa kiboko, lakini walikuwa wakikuripoti mzee cha moto unakiona halafu si mnakumbuka wasichana wa enzi zile walikuwa wakubwa sio kama wa sasa. nakumbuka tulikuwa na mmoja darasa la nne alitoa mimba.
 
Hivi nyie wote mnaochangia mjadala huu, nani aliwahi kuwa katika gwaride la "CHIPUKIZI"?
Mie mwenzeni nilikuwa kamanda wa chipukizi miaka hiyo, ukiachiliambali "Ukaka Mkuu". Kwa kweli nilipeta sana enzi zangu.
 
mnakumbuka somo la siasa?? darasa la tano
vipi kuhusu darasa la tatu wakati ndo kwanza tunaanza kukikamata king'eng'e baada ya kusoma nursery halafu ukakiacha miaka miwili tena unakikuta darasa la tatu
vipi wale ambao mwandiko tulianzia ardhini kabla ya kuzawadiwa ubao wa kundikia?? ah nazimiss sana zile chaki na ubao wangu wa mwandiko
 
Idimi umenikumbusha mbali sana kuhusu chipukizi. Mzee si unakumbuka ile kiapoooo! mnaitikia kiapooooo!!! Wewe ni nani????? Mimi ni chipukizi wa chma cha mapinduzi, ntakitumikia chama changu saa yoyote wakati wowote na mali popote ntakapoamriwa- Mungu nisaidie. Kweli tumetoka mbali yaani cahama hiki kilituinfilitrate na kuanza kutuapisha at such a tender age!!!!!! fwantastic Idfimi pliz nikumbushe hivi zile yunifom tuikuwa tunanunua au tunapewa- pamoja na zile raba nyeusi????
 
ooooh what sweet memories.

msanii umenichekesha sana i almost broke my ribs.


sitasahau darasa la 3 tulipoanza kujifunza ngeli kutamka example mi napiga kelele "eksample" taabu zaidi kwenye comparisons ikiandikwa good namalizia good,gooder gooodest


na darasa la i hadi la 2 vidole vyetu vilichapwa sana kwa kunyoosha mwandiko duh yule mwalimu hadi leo sijamsahau.

vipi kuhusu kuweka mayai viza hadi tukimaliza mtihani wa la saba halafu tunamtupia mwalimu aliyekuwa mnoko ile mbaya.

ila tabia ya walimu kulazimisha wanafunzi kununua karanga na ubuyu wao ilikuwa inakera. hata kama huna hela utaandikishwa mkopo, Basi madeni kibao upe, deni la karanga la mwalimu wa kiswahili, deni la mwl wa siasa n.k
 
nimekumbuka mbali sana nilikuwa na safari buti nilizivaa kuanzia darasa la pili hadi la nne haziishi siku moja nikavizia madingi wametoka nikaenda kukitupa kimoja katika shimo la maji machafu ili ninunuliwe chachacha za Burundi.


Wewe Ally,acha utani...
Mie nilianza shule nilinununliwa viatu laba fulani ziliandikwa DH nilikua nataniwa "Dingi Hana uwezo"
Enzi hizo nasoma Zanaki Primary school nakaa Sinza,zile laba chini ni plastic.
Saa sita natoka shule nishakula hela yote ya nauli au ninayo ya kupandia pale manzese Msufini tu inabidi nifanye yellow page mpaka Msufini au mpaka nyumabini.
Sasa laba zile na jua hazipatani unaweka mfukoni unaanza kutembea peku.
 
Kiapo cha chipukizi kilikuwa hivi:
Ki: Kiapo cha chipukizi kiapo!
Wo: Kiapoooooooooooo!
Ki: We ninani!
Wo: Mi nichipukizi
Ki: Kiongozi wako ni nani?
Wo: Nyerere na Mwinyi
Wo: Nitakitumikia chama changu kitukufu cha CCM, saa yeyote,wakati wowotena mahali popote. MUNGU nisaidie.

Zile uniform tulikuwa tunapewa bure na raba wakati mwingine nakumbuka tulikuwa tunapewa sabuni za kwenda kufulia.Kati yenu kuna aliyecheza halaiki? Mimi nilicheza halaiki mwaka 1986,sherehe za kuzima mwenge kitaifa mwanza.

Nani anakumbuka Kombolela?
Jamani nie acheni tu,tumeanzia mabali
 
hahahahaha
sio kma nacheka ila nalia kwa sweet memories za shule.
nakumbuka mara ya kwanza kuvaa chupi ilikuwa nikiwa njuka na chupi maarufu ilikuwa VIP ambayo ukiwa unasukuma soka ikakatika basi itapanda hadi kifuani....

nakumbuka pia ile style ya kuzungusha mkono iliniathiri mno hata mie na ingawa nilikomaa nao nikaingia class kinguvu bila kuandikishwa nilisota darasa la kwanza miaka mitatu (lakini bado naipenda Tanzania).

Kwa wale ambao hatukuwa mamonita najua mnakumbuka matumizi ya upupu na maji ya betri.... ila nilikuwa kiongozi bora sekondari walimu walilia tulipokuwa tunawaaga

Nimeamini kwamba kweli wewe ni Msanii!
Kumbe na wewe ni Veteran kama mimi siyo? Siwezi kusahau ubao pamoja na kuandika ardhini. Nakumbuka nilikuwa na mwalimu fulani Mngoni, alitupenda sana vijana wake. Tulianza kuandika chini kwa wiki kadha, then tukapewa mbao (wingi wa ubao) na chaki. Baada ya hapo tukawa tunapewa madaftari.
Nakumbuka enzi hizi tulikuwa tunapewa bure madaftari, ila yalikuwa na chata ya Halmashauri ya wilaya husika, noma kweli kweli.
Nakumbuka pia, daftari likiisha unakwenda nalo hadi kwa mwalimu mkuu msaidizi, anakupa jipya na unainganisha na hilo, mwendo mdundo.

Nyambala, wewe madaftari yako yalikuwa na chata gani?
Cheka!
 
leo mmenikumbusha mbali,nilicheza chipukizi sana,wakati huo nilikuwa nasoma stadium shule ya msingi pale lindi,nilikuwa kiongozi tukachaguliwa kwenda dar kwenye sherehe za mashujaa siku hiyo ndipo ile ndege ilianguka pale uwanjani,
basi tulikuwa na jamaa mmoja aliulizwa swali na mwalimu aeleze kuhusu chakula bora basi yeye akasema ni kula mpaka shingoni basi darasa lote lilianguka kucheka.
zile chupi zenye kichuma pale mbele zilikuwa zinaitwa 007.,nakumbuka nilinunuliwa mbili mwanangu hazi hiishi zile manake zilikuwa imara sana.
 
Sasa naona wengi mmesahau suala la kuvaa vijinsi chini ya sare, ama suala la kuvaa kaptura mbili mbili ili kuzuia fimbo kwenye makalio! Mie nilikuwa hodari sana wa kuvaa nguo za namna hiyo ili kupunguza makali ya fimbo za mwalimu "WALKING". Alipewa jina hili na wanafunzi wa darasa la tatu akiwa anafundisha somo la Kiingereza.
Sasa kioja ni kwamba kuna mwalimu alikuwa akijulikana kama "Twinkle" huyu yeye alikuwa anachapa nyuma ya ugoko ama mikononi. Hapa ikwa vijinsi chini ya sare havina deal tena. Huyu yeye alipewa jina hili la Twinkle kufuatia ule wimbo wa

Twinkle Twinkle Little Star
How I wonder what you are
Up above the World is so High
Like a Diamond in the Sky

Nakumbuka wimbo huu ulikuwa katika kitabu cha Kiingereza cha darasa la sita.
Tunatoka mbali sana kwa kweli.
 
Nimesoma yoooote na nimefarijika sana kukumbuka enzi hizo. Lakini furaha yangu haitaweza kamilika bila ya kukumbuka kitabu kinachitwa MWANDANI WA MWANAFUNZI. hiki kitabu kilikuwa kiboko. ukiweza ku-solve maswali yake yaaani wewe ni kwenda sekondari tu.
 
Nimesoma yoooote na nimefarijika sana kukumbuka enzi hizo. Lakini furaha yangu haitaweza kamilika bila ya kukumbuka kitabu kinachitwa MWANDANI WA MWANAFUNZI. hiki kitabu kilikuwa kiboko. ukiweza ku-solve maswali yake yaaani wewe ni kwenda sekondari tu.

Ni kweli kabisa mkuu, nilifanya mazoezi mengi sana katika kitabu hiki pamoja na vile vya "Jiandae Kumaliza Elimu ya Msingi" na "Primary English Revison" cha Bw B R Nchimbi. Ilikuwa ukikamua vitabu hivi na kuelewa yaliyomo, basi huna haja ya kuwa na wasiwasi wa kufaulu, njia ni nyeupeeeeeeeeeeeee!
 
Tunakumbuka mno,tena sana.wale wazee wenzangu mpo tuliocheza halaiki jamani!! Miaka ya 10 ya UHURU na Miaka 20 TANU!
kulikuwa na sura kibao,majimaji.gobogobo sura ya TANU nk.Ule
ulikuwa wakati jmn.Sisemi sana mpk nipate wa kukumbuka na mimi
jinsi tulivyokuwa tunajimwaga uwanja wa Taifa.
 
Thank you for the post, the memory is just too sweet...umenikubusha mbali sanaaaaaaaaaaaaaaa..kweli ya kale dhahabu..I miss those days.
 
Wewe Ally,acha utani...
Mie nilianza shule nilinununliwa viatu laba fulani ziliandikwa DH nilikua nataniwa "Dingi Hana uwezo"
Enzi hizo nasoma Zanaki Primary school nakaa Sinza,zile laba chini ni plastic.
Saa sita natoka shule nishakula hela yote ya nauli au ninayo ya kupandia pale manzese Msufini tu inabidi nifanye yellow page mpaka Msufini au mpaka nyumabini.
Sasa laba zile na jua hazipatani unaweka mfukoni unaanza kutembea peku.

Jamani hizi memory nyingine zinanivunja mbavu nacheka mpaka machozi yananitoka...kweli tumetoka mbali...unbelievable
 
Ukija Darasa la Nne ndio unakutana na Kibanga Ampiga Mkoloni, Ndoto ya Kimweri (chifu wa Wasambaa), Mkwawa Shujaa, Barua Kwa Mjomba Mndolwa na Siku ya Gulio Katerero (hadithi ya Kiiza).
Shairi la kitabu hiki linaanza hivi:

KAMA MNATAKA MALI
Karudi baba mmoja, toka safari ya mbali
Kavimba yote mapaja, na kutetemeka mwili
Watoto wake wakaja, ili kumtaka hali
Wakataka na kauli iwafae maishani

Akatamka mgonjwa, ninaumwa kweli kweli
Hata kama nikichanjwa, haitoki homa kali
Roho naona yachinjwa, Kifo kimenikabili
Kama mnataka mali, mtayapata shambani
........................................>
Kamanda leo nimekumbuka mbali....
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom