Pima mwenyewe
JF-Expert Member
- Nov 20, 2012
- 891
- 236
Jamani tusameheane 7?70.
Bado mapema sana,labda msituibie kura.mkiiba tutachukiana mpaka 2020
Jamani kuna wengi tumekwazana sana kupitia Itikadi, Majibu, Sera, Kuhusu wagombea wetu, kuna wengine najua mmetishana kupitia hata SMS.
Sasa naomba umtaje uliomkosea na umuombe Msamaha.
Yale matusi na kashfa zote ndiyo misingi tuliyoijenga kwa ajili ya maisha mapya baada ya uchaguzi. Amini nakuambia tumeishaharabu nchi uetu wenyewe kwa kujifanya hatuna akili timamu.
Kama nchi Hatujawahi kuwa na kampeni za kiwenda wazimu kama hizi, zanzibar walikua hawazikani wala kushirikiana kwa miaka mingi lakini hawakuwahi kufanya kampeni za kijuha hivi na bahati mbaya huku kwetu aina hizo za kampeni zilikua zikichochewa na viongozi wa vyama na wengine ni ma amiri wakuu.
hatukutofautiana kwa sababu ya uchaguzi tu , bali tofauti zetu ziko kwenye haki na dhuluma , binafsi siwezi kuisamehe ccm hadi siku ya kufa , ianze ccm au mimi .Jamani kuna wengi tumekwazana sana kupitia Itikadi, Majibu, Sera, Kuhusu wagombea wetu, kuna wengine najua mmetishana kupitia hata SMS.
Sasa naomba umtaje uliomkosea na umuombe Msamaha.