'Tulimkamata Osama Bin Laden Lakini Marekani Walimuachia Huru'

MwanaFalsafa1

JF-Expert Member
Feb 26, 2008
5,565
836
Baada ya awali kusema kwamba Taliban iliundwa na shirika la ujasusi la Marekani la CIA kwaajili ya faida ya Marekani, rais wa Pakistan ameendelea kutoa vijembe kwa serikali ya Marekani.

Akiongea na televisheni ya NBC ya Marekani, Zardari alisema kwamba Osama bin Laden alikamatwa na majeshi ya Pakistani mwaka 2001 lakini Marekani walimuachia huru.

Zardari alisema kwamba majeshi ya Pakistan kwa kushirikiana na majeshi ya Marekani walishirikiana katika operesheni ya kumsaka Osama bin Laden kwenye milima ya Tora Bora.

Zardari aliendelea kusema kuwa wakati wa operesheni hiyo majeshi ya Pakistan yalimkamata Osama bin Laden na kumkabidhi kwa majeshi ya Marekani lakini majeshi hayo ya Marekani yalimuachia huru.

Zardari alisema pia kwamba haamini kama Osama bin Laden ambaye alikamatwa miezi mitatu baada ya mashambulizi ya septemba 11 yuko hai hadi sasa.

Ni miaka minane sasa CIA haijapata habari zozote kuhusiana na Osama bin Laden na hata hivyo Marekani ilishatupilia mbali mipango yake ya kuishawishi dunia iamini kwamba Osama bin Laden amejificha kwenye milima ya Tora bora.

Pakistan imekuwa kwenye shinikizo kubwa toka kwa Marekani ambayo imeitaka Pakistan itokomeze majeshi ya Taliban ambayo yanajiunga upya kwenye miji iliyopo kwenye mpaka wa Pakistan na Afghanistan.

Source:http://www.nifahamishe.com/NewsDetails.aspx?NewsId=2033078&&Cat=2
 
Huyu Zardari utawala wake nao uko hatarini na Congress wanaanza kuhisi hela zinazotolewa kwa ajili ya kusaidia jeshi zinakwenda kwenye Nuclear Arsenal Expansion.ASFC inakua kila siku, missile battalions zinaongezeka lakini hakuna anayejua wanakwenda wapi. Ila siku moja Nuclear za Pkistan zitaslip into wrong hands and find its way to India na kuua millions...
 
Hilo Shirika hata siku moja(hivi karibuni) haliwezi kukubali moja kwa moja au kwa namna nyingine kwamba hili limewahi kutokea-Lakini kama huyo Zardari ana uhakika-basi amejichimbia kaburi la kisiasa na uhusiano na Marekani!
 
CIA wana conspiracies nyingi. Wanaserve interests za taifa lao kwa hiyo hata kama ni kweli wata tafyta njia za kuficha. Claims za huyu jamaa siwezi kuzi dismiss moja kwa moja,ina wezekana.
 
Mambo ni Tete mno huko Pakistani hata huyu Bwana Asif Zardari yupo kwenye angle mbaya......inaonekana mambo yanamwendea vibaya na hao Taliban wamepata kasi ya ajabu...Kikubwa ambacho USA wanakiangalia ni kwamba General Ashfaq Kayani haonekani kum-support Rais wake,nae kwa sasa ndiye mtu mwenye nguvu na ushawishi mkubwa kwa siasa za ndani...Kuna baadhi ya wanadiplomasia wanatabiri si muda mrefu Jeshi litachukua madaraka!
 
Mambo ni Tete mno huko Pakistani hata huyu Bwana Asif Zardari yupo kwenye angle mbaya......inaonekana mambo yanamwendea vibaya na hao Taliban wamepata kasi ya ajabu...Kikubwa ambacho USA wanakiangalia ni kwamba General Ashfaq Kayani haonekani kum-support Rais wake,nae kwa sasa ndiye mtu mwenye nguvu na ushawishi mkubwa kwa siasa za ndani...Kuna baadhi ya wanadiplomasia wanatabiri si muda mrefu Jeshi litachukua madaraka!

Uko sawa kabisa, Kayani ni kipenzi cha US isitoshe amesomea Marekani vile vile. Zardari maji yameshafika shingoni its a matter of time kabla hawajamtoa madarakani, na inasemekana silaha zinazotolewa na US zinaishia mikononi mwa Taliban na hakuna anayejua zinafikaje uko.
 
Mmarekani, especially CIA, kila anachofanya anafanya kwa motive na ambition fulani.

Motive yao ilikuwa ni nini katika kumuachia Osama? Ambition yao ilikuwa ni nini? Je Bush asingefurahi kujionyesha mshindi kwa kuionyesha dunia kwamba ameweza kumkamata Osama?

Hii haiingii akilini, most likely Zardari ni mfa maji anayetoa dramatics za kutapatapa au hiyo source si credible.
 
Back
Top Bottom