Tulimcheka Kikwete kumbe wengine wapo!

Angalia hapo kwenye rangi nyekundu au rudi usome tundiko la kwanza......

Mkubwa, hata hao waandishi nao hawana clue, angalia hapa chini kwenye blue
Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) imetoa sh. 4, 875,000 kwa timu ya soka ya Waandishi wa Habari za Michezo Nchini (TASWA FC) kwa ajili ya kushiriki katika bonanza la waandishi wa habari wa Mkoa wa Arusha.
 
IMG_0605.JPG



Meneja Uhusiano wa TBL,Edith Mushi (kushoto) akikabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi milion 4.8 kwa Mwenyekiti wa TASWA FC,Majuto Omary kwa ajili ya mashindao ya Bonanza huko mkoani Arusha.katikati ni Afisa Uhusiano wa TBL,Lilian Erasmus.

Lakini kilichoandikwa kwa numerali (kwenye hundi) ndio hicho hicho kilichoandikwa kwa maneno. Sioni kosa hapo, ilsipokuwa hiyo THOUSANDS ilitakiwa kuandikwa THOUSAND. Sielewi hiyo 4,875,000/= Mwanakijiji ameitoa wapi. Labda kuna ajenda hapa!



Hapana. kilichoandikwa kwa tarakimu sicho kilichoandikwa kwa maneno. Kilichoandikwa kwa maneno ni 'four milion and eighty thousands' yaani 4,080,000.00. Kilichoandikwa kwa tarakimu ni 4,800,000.00 ambacho kwa maneno ya Kiingereza ingekuwa 'four milion and eight hundred thousand'.....

Eight na eighty ni idadi tofauti
 
IMG_0605.JPG



Meneja Uhusiano wa TBL,Edith Mushi (kushoto) akikabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi milion 4.8 kwa Mwenyekiti wa TASWA FC,Majuto Omary kwa ajili ya mashindao ya Bonanza huko mkoani Arusha.katikati ni Afisa Uhusiano wa TBL,Lilian Erasmus.

Lakini kilichoandikwa kwa numerali (kwenye hundi) ndio hicho hicho kilichoandikwa kwa maneno. Sioni kosa hapo, ilsipokuwa hiyo THOUSANDS ilitakiwa kuandikwa THOUSAND. Sielewi hiyo 4,875,000/= Mwanakijiji ameitoa wapi. Labda kuna ajenda hapa!


Duuuuh!...........naona umeamua kuwapa watu kusema zaidi...........kwi kwi kwi kwi
 
mbona haya masomo ya kujua kusoma namba na kuandika namba unajifunza hata college hapa masomo ya mwanzo ya hesabu utadhani hukusoma shuleni.

Unaambiwa andika hii namba kwa maneno: 4,834,868.62

Kwa kiswahili utaiandikaje?

Milioni nne Mia nane thelasini na nne elfu Mia nane sitini na nane na senti sitini na mbili
 
Yah, bongo tambarare. Hapa photo inakuwa haikaliki kwenye makabrasha ya kumbukumbu za mtoaji na mpokeaji. Yaibu(sic) na balaa tupu.
 
Sawa, lakini angalau umejua nilipoitoa, sio?

ulipoipata kuna figures mbili, kwa hiyo na wewe ungeenda benki ukawaambia eti ki caption cha gazeti kimesema natakiwa kupata so and so much wangekuona na wewe Kikwete tu. Not to mention, ungepewa hiyo cheki isingekuja na hicho ki caption cha mwandishi. So, in my book, hapa hatujui kilitakiwa kiandikwe kiasi gani.
 
ulipoipata kuna figures mbili, kwa hiyo na wewe ungeenda benki ukawaambia eti ki caption cha gazeti kimesema natakiwa kupata so and so much wangekuona na wewe Kikwete tu. Not to mention, ungepewa hiyo cheki isingekuja na hicho ki caption cha mwandishi. So, in my book, hapa hatujui kilitakiwa kiandikwe kiasi gani.

Agreed! Zaidi ya hapo labda unataka kucheza ligi ya kombe la mbuzi
 
Kitu chochote unachoweka sahihi hakitaki haraka haraka. Aliyetia sahihi nchi za watu wanaojali kuwajibika hana budi kujieleza au hata kuwajibishwa.

Kama hilo hundi kubwa hivyo anaboronga sijui kama anaweza kufuatilia small print za contracts zinazohitaji sahihi.

Hapo kwenye bluu:
Ndio maana kwa kujua viongozi wetu wengi ni wa-jamii ya JK, na hao wa TBL na TASWA wawekezaji wanaamua kutuita London na kutusainisha mikataba Hotel.
 
Aliyeandika cheque hii alikuwa ni production manager wa TBL na alikuwa ameshabwia kreti kadhaa za bia ku-test ubora wake. Tumsamehe bure.

Shida yetu watanzania wengi hatupendi kusoma kabisa. Yaani aliyesaini cheque wala hakusoma ili ajiridhishe kama ana-sign kitu sahihi (funny signatories!!!!!). Mi nijuavyo unaposign cheque inabidi ujiridhishe kama maandishi na tarakimu ziko sawa. Halafu eti tunashangaa tukilizwa kwenye mikataba mibovu. Wanao-sign huwa wala hawaisomi. Si mmeona hata sheria ya gharama za uchaguzi mkuu ali-sign kichwakichwa tu akaingizwa mjini na wajanja.
 
Back
Top Bottom