Synthesizer
JF-Expert Member
- Feb 15, 2010
- 11,143
- 18,774
Ni jambo ambalo hadi leo linanikera, linaniudhi, na kunisikitisha sana. Tanzania katika miaka ya 1960 hadi 1990 ilikuwa mwanzilishi wa nchi tano zilizo mstari wa mbele katika ukombozi wa kusini mwa Afrika. Tulilaani kwa ngiuvu zote ubaguzi wa rangi. Tulilaani kwa nguvu zote ubabe wa polisi wa makaburu dhidi ya raia wasiokuwa na silaha walipoandamana kudai haki zao. Tulilaani haya yakitokea nje ya mipaka yetu.
La ajabu sana, leo hii tunakubali ubaguzi na ubabe wa polisi ndani ya mipaka yetu wenyewe. Leo hii wazungu wengi wanaokuja katika nchi yetu kwa mlango wa uwekezaji wanawanyanyasa na kuwafanyia ubaguzi wa rangi raia na wazalendo kwa kiasi cha juu sana, na serikali yetu haitaki kusikiliza kilio cha wananchi kwa kuogopa kuwaudhi wawekezaji. Kuna baadhi ya wawekezaji toka South Afrika wanafanya vitendo vya kibaguzi kwa namna ambayo wasingethubutu hata kidogo kuvifanya huko kwao katika Afrika Kusini ya sasa. Viongozi wetu hawaoni shida juu ya hili, hawataki kuwasikiliza wananchi juu ya hili. Leo hii mtanzania mweusi hana haki katika sehemu kama migodi ya dhahabu, ananyanyaswa katika nchi yake mwenyewe, anadharauliwa na bosi wake mzungu na hana kwa kusemea kwa kuwa hakuna anayemsikiliza. Haya yote yanafanyika katika nchi iliyokuwa mstari wa mbele kulaani ubaguzi, na hata Watanzania wakapoteza maisha katika vita dhidi ya ubaguzi kusini mwa Afrika. Hata hao wageni wazungu katika nchi yetu wanatucheka na kutudharau sana, wanatukebehi wakisema kwa jinsi mlipovyopiga kelele juu ya ubaguzi wa rangi, tulidhani hapa Tanzania mtu angehukumiwa kifo kwa kufanya ubaguzi wa rangi, sasa iweje baadhi ya wenzetu wanawafanyia ubaguzi wa rangi na hakuna lolote serikali yenu inachofanya? Huu ni unafiki sana.
Vipi ubabe na mauaji ya polisi ya raia wasio na silaha? Naam, tulilaani Sharpeville, pale polisi walipopiga raia risasi za moto migongoni. Hatukuuliza serikali ya makaburu kama wale raia walikuwa na kibali cha kuandamana, bali tulilaani tu, tukasema walikuwa na haki ya kudai haki zao kwa maandamano.
Tulilaani mauaji ya Soweto polisi walipopiga na kuua wanafunzi wasio na silaha. Hatukuuliza kama wanafunzi waliomba kibali cha kuandamana. Tulisema wanafunzi walikuwa na madai ya msingi na ilaaniwe serikali ya makaburu kwa kuua raia wasio na silaha.
Tuliaani ubagaguzi, ubabe wa polisi nje ya nchi yetu. Tulitoa hotuba kulaani, tulikatisha masomo na kazi na shughuli za shamba ili tuandamane na kulaani, tulitunga miziki kulaani, na hata tulipeleka jeshi letu kupigana - tukisema uhuru wetu hauwezi kuwa safi wakati ndugu zetu wanabaguliwa na kunyanyaswa na ubabe wa polisi. Tuliwaita watu wa Msumbiji, Namibia, Afrika Kusini waje nchini kwetu wafungue kambi za mafunzo ya kijeshi ili wakapigane nchini kwao kuondoa ubaguzi wa rangi na unyanyasaji wa polisi. Tukasema tutapigana nao bega kwa bega hadi tone la mwisho la damu!
Sasa ubaguzi, mauaji ya polisi yanatokea ndani ya mipaka yetu. Tunaona sawa inakubalika. Raia wanapigwa na polisi na tunaambiwa sababu ni kwamba raia waliandamana bila kibali tukawapiga risasi za moto. Tunaona sawa. Tuaangalia picha za polisi wakitumia mabavu dhidi ya wanafunzi chuo kikuu na kwingineko kwa udhalilishaji wa hali ya juu. Tunaona sawa.
Tulilaani raia wazalendo wa Afrika kusini kuhamishwa toka makao yao ili kuwapisha wazungu. Leo mzalendo wa Kitanzania akihamishwa kwa mabavu na polisi ili wawapishe wawekezaji (wazungu) toka nje, na hata akiuwawa katika kuhamishwa huko, tunaona sawa.
Kwa nini isiwe sawa kwetu kwa wananchi kubaguliwa na wazungu kule Msumbiji, Angola, Namibia, Afrika kusini lakini iwe sawa kwa wazalendo Watanzania kubaguliwa ndani ya mipaka ya nchi yao?
Kwa nini isiwe sawa kwa polisi kuwapiga risasi za moto waandamanaji wasio na kibali kule Sharpeville, Soweto na mitaa mingi ya Afrika ya kusini lakini iwe sawa kwa polisi wetu wenyewe kufanya hivyo Mbeya, Arusha, Songea na kwingineko?
Kwa nini tushindwe kuvumilia ubaguzi wa rangi na unyanyasaji wa polisi nje ya mipaka yetu na hata kujitoa muhanga kuwakomboa jirani zetu na baadaye tiyavumilie nmaovu hayo hayo yanapofanywa ndani ya mipaka yetu wenyewe?
Lazima tuwaulize viongozi wetu watupe majibu.
Lazima tuwaeleze wananchi kwamba haya yote hayakuwa sawa nje ya mipaka yetu, na si sawa ndani ya mipaka yetu
Lazima tueneze ujumbe huu ili kuonyesha kwamba tuna viongozi ambao ni viongozi kwa maslahi yao wao binafsi.
La ajabu sana, leo hii tunakubali ubaguzi na ubabe wa polisi ndani ya mipaka yetu wenyewe. Leo hii wazungu wengi wanaokuja katika nchi yetu kwa mlango wa uwekezaji wanawanyanyasa na kuwafanyia ubaguzi wa rangi raia na wazalendo kwa kiasi cha juu sana, na serikali yetu haitaki kusikiliza kilio cha wananchi kwa kuogopa kuwaudhi wawekezaji. Kuna baadhi ya wawekezaji toka South Afrika wanafanya vitendo vya kibaguzi kwa namna ambayo wasingethubutu hata kidogo kuvifanya huko kwao katika Afrika Kusini ya sasa. Viongozi wetu hawaoni shida juu ya hili, hawataki kuwasikiliza wananchi juu ya hili. Leo hii mtanzania mweusi hana haki katika sehemu kama migodi ya dhahabu, ananyanyaswa katika nchi yake mwenyewe, anadharauliwa na bosi wake mzungu na hana kwa kusemea kwa kuwa hakuna anayemsikiliza. Haya yote yanafanyika katika nchi iliyokuwa mstari wa mbele kulaani ubaguzi, na hata Watanzania wakapoteza maisha katika vita dhidi ya ubaguzi kusini mwa Afrika. Hata hao wageni wazungu katika nchi yetu wanatucheka na kutudharau sana, wanatukebehi wakisema kwa jinsi mlipovyopiga kelele juu ya ubaguzi wa rangi, tulidhani hapa Tanzania mtu angehukumiwa kifo kwa kufanya ubaguzi wa rangi, sasa iweje baadhi ya wenzetu wanawafanyia ubaguzi wa rangi na hakuna lolote serikali yenu inachofanya? Huu ni unafiki sana.
Vipi ubabe na mauaji ya polisi ya raia wasio na silaha? Naam, tulilaani Sharpeville, pale polisi walipopiga raia risasi za moto migongoni. Hatukuuliza serikali ya makaburu kama wale raia walikuwa na kibali cha kuandamana, bali tulilaani tu, tukasema walikuwa na haki ya kudai haki zao kwa maandamano.
Tulilaani mauaji ya Soweto polisi walipopiga na kuua wanafunzi wasio na silaha. Hatukuuliza kama wanafunzi waliomba kibali cha kuandamana. Tulisema wanafunzi walikuwa na madai ya msingi na ilaaniwe serikali ya makaburu kwa kuua raia wasio na silaha.
Tuliaani ubagaguzi, ubabe wa polisi nje ya nchi yetu. Tulitoa hotuba kulaani, tulikatisha masomo na kazi na shughuli za shamba ili tuandamane na kulaani, tulitunga miziki kulaani, na hata tulipeleka jeshi letu kupigana - tukisema uhuru wetu hauwezi kuwa safi wakati ndugu zetu wanabaguliwa na kunyanyaswa na ubabe wa polisi. Tuliwaita watu wa Msumbiji, Namibia, Afrika Kusini waje nchini kwetu wafungue kambi za mafunzo ya kijeshi ili wakapigane nchini kwao kuondoa ubaguzi wa rangi na unyanyasaji wa polisi. Tukasema tutapigana nao bega kwa bega hadi tone la mwisho la damu!
Sasa ubaguzi, mauaji ya polisi yanatokea ndani ya mipaka yetu. Tunaona sawa inakubalika. Raia wanapigwa na polisi na tunaambiwa sababu ni kwamba raia waliandamana bila kibali tukawapiga risasi za moto. Tunaona sawa. Tuaangalia picha za polisi wakitumia mabavu dhidi ya wanafunzi chuo kikuu na kwingineko kwa udhalilishaji wa hali ya juu. Tunaona sawa.
Tulilaani raia wazalendo wa Afrika kusini kuhamishwa toka makao yao ili kuwapisha wazungu. Leo mzalendo wa Kitanzania akihamishwa kwa mabavu na polisi ili wawapishe wawekezaji (wazungu) toka nje, na hata akiuwawa katika kuhamishwa huko, tunaona sawa.
Kwa nini isiwe sawa kwetu kwa wananchi kubaguliwa na wazungu kule Msumbiji, Angola, Namibia, Afrika kusini lakini iwe sawa kwa wazalendo Watanzania kubaguliwa ndani ya mipaka ya nchi yao?
Kwa nini isiwe sawa kwa polisi kuwapiga risasi za moto waandamanaji wasio na kibali kule Sharpeville, Soweto na mitaa mingi ya Afrika ya kusini lakini iwe sawa kwa polisi wetu wenyewe kufanya hivyo Mbeya, Arusha, Songea na kwingineko?
Kwa nini tushindwe kuvumilia ubaguzi wa rangi na unyanyasaji wa polisi nje ya mipaka yetu na hata kujitoa muhanga kuwakomboa jirani zetu na baadaye tiyavumilie nmaovu hayo hayo yanapofanywa ndani ya mipaka yetu wenyewe?
Lazima tuwaulize viongozi wetu watupe majibu.
Lazima tuwaeleze wananchi kwamba haya yote hayakuwa sawa nje ya mipaka yetu, na si sawa ndani ya mipaka yetu
Lazima tueneze ujumbe huu ili kuonyesha kwamba tuna viongozi ambao ni viongozi kwa maslahi yao wao binafsi.