Eeka Mangi
JF-Expert Member
- Jul 27, 2008
- 3,173
- 481
Hatukuwa watoto kihivyo ingawa tulistahili kuwa watoto. Niko f2 mwenyewe yuko F1. Wakaja shuleni kwetu kwenye zile inter school social. Jamaa tulikuwa mabreak dancers acha utani! Basi katika lile kundi la wale mabinti akatikea mmoja kuvutiwa na kijana mmoja EM. Haikuchukua mda jitihada zikawa zimewafanya wawe pamoja kwa miaka takribani 2 na nusu. Kwa kusema ukweli binti huyu alinipenda! Mtoto wa kinyamwezi kapanda juu hivi! weusi ule wa kuzaliwa mrembo si haba. Yaani alikamilika. Akitoka kwao anapitia pale Moshi mjini anaacha pocket money kwa kijana anachukua nauli anaishia shule. Weekend anakuja kidume napanga budget.
Natamani sana nimwone leo sijui yuko wapi. Natamani nimwone leo sio kurudia yale tuliyokuwa tunafanya! La hasha!
Nataka nimwombe radhi ka ajili ya siku ile niliyomwambia bila haya eti SIKUTAKI! Kweli alihangaika kucha kunitafuta! Hakuniona usiku huo na wala haikutokea kukutana tena. Bado namwona natamani nimwone tena. Sijui yukoje saa hii.
Anna weeeeeeeeee wapi mdada!
Natamani sana nimwone leo sijui yuko wapi. Natamani nimwone leo sio kurudia yale tuliyokuwa tunafanya! La hasha!
Nataka nimwombe radhi ka ajili ya siku ile niliyomwambia bila haya eti SIKUTAKI! Kweli alihangaika kucha kunitafuta! Hakuniona usiku huo na wala haikutokea kukutana tena. Bado namwona natamani nimwone tena. Sijui yukoje saa hii.
Anna weeeeeeeeee wapi mdada!