Kamakabuzi
JF-Expert Member
- Dec 3, 2007
- 2,859
- 1,301
Kama Idd simba alivyosema juzi - watanzania tumedumaa/tumedumazwa kiakili! Je ni kweli?
JK kashindwa, na hili liko wazi na shahidi ni yeye mwenyewe alipoikana ilani iliyomuweka madarakani - live wote tukiona na kusikia. Sasa anakuja mtu anasema kafanya mengi! Kama yangekuwepo mengi asingeikana ilani yake!
Hoja kwamba tumgemchagua nani mwaka 2005 - jibu ni rahisi - wote walioruhusiwa kugombea urais walikuwa na uwezo wa kuwa marais, Hivyo kwa kuwa mlimchagua JK sasa amevurunda basi kumbe kati ya wale waliobaki mmojawapo angekuwa rais.
Watanzania tunajidumaza kiakili kufikiria eti rais lazima atoke CCM! CCM imekuwa kichaka cha kila aina ya ufisadi, mimi ningekuwa mwanaccm ningekuwa najificha nikisikia mtu anataja CCM ili nisije nikaitwa fisadi.
WaTZ tunaacha kuwachagua watu toka kambi ya upinzani kwa hisia tu - eti hawatafanya vizuri. OK mtasema Mbowe hana rekodi mnayoijua - je Mrema? Mtu aliyepata kushika uwaziri na unaibu waziri mkuu! hamumjui? Si mnajua mafisadi wangepewa siku saba kurudisha pesa zetu; si mrema alianza kunusa ufisadi wa akina patel katika kashfa ya mashamba ya mkonge?
Wengine wanasema eti tukiwachagua wapinzani nao wataenda kula tu! Huo ni udumavu wa akili - kwa nini wawahukumu kwa hisia zako tu? OK hata kama wataenda nao kula, je nchi imeumbwa iliwe na CCM tu?
La msingi, na ndiyo uzuri wa demokrasia halisi, unamchagua mtu akivurunda unamtoa unamuweka mwingine, akivurunda naye unamtoa unamuweka mwingine, naye akivurunda labda yule wa kwanza atakuwa amepata fundisho - unamrudisha, akivurunda tena unamuacha..... and so on .....!
WaTZ tunag'ang'ania CCM tuuuuuuuu ingawa tunakiri inafanya vibaya! UDUMAVU WA AKILI HUO
JK kashindwa, na hili liko wazi na shahidi ni yeye mwenyewe alipoikana ilani iliyomuweka madarakani - live wote tukiona na kusikia. Sasa anakuja mtu anasema kafanya mengi! Kama yangekuwepo mengi asingeikana ilani yake!
Hoja kwamba tumgemchagua nani mwaka 2005 - jibu ni rahisi - wote walioruhusiwa kugombea urais walikuwa na uwezo wa kuwa marais, Hivyo kwa kuwa mlimchagua JK sasa amevurunda basi kumbe kati ya wale waliobaki mmojawapo angekuwa rais.
Watanzania tunajidumaza kiakili kufikiria eti rais lazima atoke CCM! CCM imekuwa kichaka cha kila aina ya ufisadi, mimi ningekuwa mwanaccm ningekuwa najificha nikisikia mtu anataja CCM ili nisije nikaitwa fisadi.
WaTZ tunaacha kuwachagua watu toka kambi ya upinzani kwa hisia tu - eti hawatafanya vizuri. OK mtasema Mbowe hana rekodi mnayoijua - je Mrema? Mtu aliyepata kushika uwaziri na unaibu waziri mkuu! hamumjui? Si mnajua mafisadi wangepewa siku saba kurudisha pesa zetu; si mrema alianza kunusa ufisadi wa akina patel katika kashfa ya mashamba ya mkonge?
Wengine wanasema eti tukiwachagua wapinzani nao wataenda kula tu! Huo ni udumavu wa akili - kwa nini wawahukumu kwa hisia zako tu? OK hata kama wataenda nao kula, je nchi imeumbwa iliwe na CCM tu?
La msingi, na ndiyo uzuri wa demokrasia halisi, unamchagua mtu akivurunda unamtoa unamuweka mwingine, akivurunda naye unamtoa unamuweka mwingine, naye akivurunda labda yule wa kwanza atakuwa amepata fundisho - unamrudisha, akivurunda tena unamuacha..... and so on .....!
WaTZ tunag'ang'ania CCM tuuuuuuuu ingawa tunakiri inafanya vibaya! UDUMAVU WA AKILI HUO