Tulikosea kumchagua JK 2005, tungemchagua nani?

Kama Idd simba alivyosema juzi - watanzania tumedumaa/tumedumazwa kiakili! Je ni kweli?
JK kashindwa, na hili liko wazi na shahidi ni yeye mwenyewe alipoikana ilani iliyomuweka madarakani - live wote tukiona na kusikia. Sasa anakuja mtu anasema kafanya mengi! Kama yangekuwepo mengi asingeikana ilani yake!
Hoja kwamba tumgemchagua nani mwaka 2005 - jibu ni rahisi - wote walioruhusiwa kugombea urais walikuwa na uwezo wa kuwa marais, Hivyo kwa kuwa mlimchagua JK sasa amevurunda basi kumbe kati ya wale waliobaki mmojawapo angekuwa rais.

Watanzania tunajidumaza kiakili kufikiria eti rais lazima atoke CCM! CCM imekuwa kichaka cha kila aina ya ufisadi, mimi ningekuwa mwanaccm ningekuwa najificha nikisikia mtu anataja CCM ili nisije nikaitwa fisadi.

WaTZ tunaacha kuwachagua watu toka kambi ya upinzani kwa hisia tu - eti hawatafanya vizuri. OK mtasema Mbowe hana rekodi mnayoijua - je Mrema? Mtu aliyepata kushika uwaziri na unaibu waziri mkuu! hamumjui? Si mnajua mafisadi wangepewa siku saba kurudisha pesa zetu; si mrema alianza kunusa ufisadi wa akina patel katika kashfa ya mashamba ya mkonge?

Wengine wanasema eti tukiwachagua wapinzani nao wataenda kula tu! Huo ni udumavu wa akili - kwa nini wawahukumu kwa hisia zako tu? OK hata kama wataenda nao kula, je nchi imeumbwa iliwe na CCM tu?

La msingi, na ndiyo uzuri wa demokrasia halisi, unamchagua mtu akivurunda unamtoa unamuweka mwingine, akivurunda naye unamtoa unamuweka mwingine, naye akivurunda labda yule wa kwanza atakuwa amepata fundisho - unamrudisha, akivurunda tena unamuacha..... and so on .....!
WaTZ tunag'ang'ania CCM tuuuuuuuu ingawa tunakiri inafanya vibaya! UDUMAVU WA AKILI HUO
 
Mwaka 2005 ni mwaka pekee ambao Watanzania tulimchagua Rais bila shinikizo kutoka kwa Mwalimu JK Nyerere.

Ni rais pekee ambaye katika utawala wke hakuna confrotation iliyojitokeza hadi sasa kusababisha matumizi ya nguvu kwa raia.

Ni Rais pekee ambaye ameweza kuanzisha mpango wa shule za sekondari kwa kila kata.
Ni Rais pekee aliyeamua kuunganisha mikoa ya kufungua Mikoa iliyoko nyuma kama Kigoma na Rukwa na kuiunganisha na barabara kuu,ikiwa ni pamoja na ile ya Kagera hadi Mwanza ili ku stimulate biashara na uchumi katika nchi pamoja na kwamba dunia imo katika hali mbaya kiuchumi.
Ni rais pekee ambaye katika utawala wake ameweza kuwapeleka mahakamani watuhumiwa wa ufisadi wakubwa ili wapambane na sheria.
ni katika utawala huu ambao Kilimo kinapewa kipaumbele ili wakulima wetu walime kwa kutumia zana za kisasa kwa vitendo siyo blah blah.
Bila kusahau University ya Dodoma,vivuko vipya Kigamboni,Mv Misungwi na vinginevyo.
Amefanya mageuzi makubwa kwa vyombo vya habari kuwa huru na midomo ya watu kuzungumza bila vitisho.Sasa ati tulikosea! Ili kujua kuwa hatujakosea subiri muone 2010.JK atachaguliwa tena kwa kura zaidi na ataanza ngwe ya pili kwa mipango madhubuti ya maendeleo ya kweli na uhakika!


Kwa mawazo kama haya!! No wonder CCM watatesa mpaka karne ijayo.

Kwa mtaji huu nitakufa bado naililia TZ yangu masikini isiyojua nini maana ya maendeleo.

In fact tatizo letu wa-Bongo hatujui nini maana ya maendeleo ndiyo sababu tukiona kakitu kampya kameletwa sisi tunafikiria hayo ndiyo maendeleo. JK sasa ajitahidi ajenge ka-fly over kamoja bongo then katatosha kumpa urais maisha!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom