Tulichosema kuhusu Kigamboni kimetimia: Tukimbilie wapi?

Dark City,

Kweli kabisa maneno yako lakini pamoja na kuwa na viongozi wabaya huoni kwamba kuna umuhimu wa sehemu hiyo kutojengwa vibanda na kuanzisha biashara haramu za viwanja wakati tuna matatizo mengi..

Mkuu Hata nyumba za Msajili na NHC zinauzwa leo hii kwa mabillioni wakati serikali inapokea vijisenti..Binafsi kama kuna kiongozi ataingilia kati na kusimamisha uuzaji wa nyumba hizi ama ubadilishaji wa mikono ktk nyumba hizi na kutazama upya mpango wa upangishaji na pengine uuzwaji wa nyumba hizi nitapongeza hatua hiyo pamoja na kwamba kuna watu wamekwisha piga mahesabu yao.

Kesho tunaweza kabisa kumweka mtu kiti moto na kumuulizia KULIKONI badala ya kuacha swala zima kila mtu anaingiza mkono wake. Mama Mkapa amekuwa na nguvuna nyumba za serikali kuliko hata Msajili wenyewe.
Kundi dogo la watu ambao hawana hata madaraka serikalini ndio vinara wa uuzaji wa nyumba hizi wakati hawana hata mchango wa senti ktk ujenzi ama sheria andamizi ya Utaifishaji..

Hadi sasa hivi mkuu, viwanja vya Kigamboni vimetolewa kiholela, mimi binafsi niliambiwa nitume dollar 3,000 nipatiwe kiwanja beach nikashtuka kwa sababu sikuamini kabisa kwamba serikali inaweza kutoa viwanja vya beach bila kuona mjengo ama dhumuni la maombi ya kiwanja hicho..Mji haujengwi kwa kutoa vibali na hati bila kufuata ramani iliyopo mezani..Na sidhani kama tunayo ramani ya mji wetu kwa miaka 10 au 20 ijayo!.. hivyo, nilijua kuna namna pamoja na kwamba ningepewa kibali na pengine kuchukua hata Hati ya kumiliki lakini kisheria utaratibu ulotumika unanifungia kanyaboya..

Kweli kabisa toka mwinyi, Mkapa hadi leo Kikwete kumekuwa na utapeli mkubwa toka kwa viongozi wetu lakini kuwepo kwa viwanja hivyo chini ya serikali kunatupa muda na wasaa wa kuwaondoa CCM madarakani na serikali mpya ikaweza kutumia haki hii kuijenga tanzania tunayoitaka badala ya kurudi tena ktk sheria za Utaifishaji baada ya ujenzi mbaya.

Mkuu Mkandara hatutofautiani kitu kuhusu haja ya kuwa na míji iliyotengezwa kwa mpango badala ya kuwa na miji ambayo inakua kama ni ajali ajali vile(unplanned). Ila hatuna watu wakutufanyia kazi hiyo kwa sasa. Kwa sababu hatuna serikali yenye bongo inayoona mbele. Na maadamu hatuna kitu kama hicho (serikali) ambacho ni muhimu katika kubuni mipango na kuisimamia kikiwa na baraka na imani ya wananchi basi tuiache ardhi ikae kama pori. Kwani itaoza?? Mbona Mwalimu JKN aliacha madini yetu kwa sababu kama hizo. Kama isingekuwa hii mibaka uchumi si wangekuja kufaidi wajukuu zetu?? Hata miji itajengwa tu, ama na kizazi chetu au kijacho.

Jambo ambalo sitaki ni kuibiana kimacho macho kama ambavyo wizara ya ardhi (na serikali kwa ujumla) inafanya sasa.
 
Dark City,
Nimekusikia mkuu lakini Nyerere aliacha madini yetu ardhini yakiwa chini ya nani? sio serikali au?..
Maana ya maneno yangu inaonyesha kuwa ardhi hiyo tayari ilikwisha chukuliwa na watu fulani viwanja kugawiwa ndio maana serikali imechukua kuzirudisha mikononi mwake..
Kama isingekuwa hivyo hakuna haja ya serikali kuichukua kwani siku zote ardhi ni ya serikali unless wameigawa tayari kwa mpango wa lease sijui miaka 99.. Na tusingesikia malalamiko ya watu kuhusu hati za kulimiki kama hawakugawiwa viwanja hivyo...
Kitakacho fuata baada ya hapo ndio mapendekezo kama yako..ardhi iachwe bila kupitisha utapeli wowote..
 
Dark City,
Nimekusikia mkuu lakini Nyerere aliacha madini yetu ardhini yakiwa chini ya nani? sio serikali au?..
Maana ya maneno yangu inaonyesha kuwa ardhi hiyo tayari ilikwisha chukuliwa na watu fulani viwanja kugawiwa ndio maana serikali imechukua kuzirudisha mikononi mwake..
Kama isingekuwa hivyo hakuna haja ya serikali kuichukua kwani siku zote ardhi ni ya serikali unless wameigawa tayari kwa mpango wa lease sijui miaka 99.. Na tusingesikia malalamiko ya watu kuhusu hati za kulimiki kama hawakugawiwa viwanja hivyo...
Kitakacho fuata baada ya hapo ndio mapendekezo kama yako..ardhi iachwe bila kupitisha utapeli wowote..

Ndugu Mkandara, serikali ya wakati huo ilikuwa chini ya mwalimu ambaye ama yeye mwenyewe, mke wake au watoto wake hawakuwa wajasiriamali. Kwa hizi serikali zilizofuata ndo maana walishindwa kuvumilia wakaamua heri wagawe madini yetu ili wapate mapaja mawili ya kuku badala ya kuendelea kuyantunza ili siku moja wote tufanye sherehe (party) kwa pamoja na kujipongeza. Mimi nadhani kama wakiwapa walala hoi hata kwa hati za miaka 99 si neno. Shida ni hapo ambapo wanapima viwanja na zaidi ya 80% wanachukua wao na wake zao na nyumba zao ndogo. Mbaya zaidi vingine wanagawawia hao wapuuzi wanaoitwa wawekezaji kwa bei ya kutupa. Ukihitaji ushahidi zaidi nitakupa hadithi ya kilichotokea Bunjua!!
 
Dark City,
Shida ni hapo ambapo wanapima viwanja na zaidi ya 80% wanachukua wao na wake zao na nyumba zao ndogo. Mbaya zaidi vingine wanagawawia hao wapuuzi wanaoitwa wawekezaji kwa bei ya kutupa. Ukihitaji ushahidi zaidi nitakupa hadithi ya kilichotokea Bunjua!!
Nimekusikia mkuu kusema kwenda hata mimi nimepumbazika na kauli ya serikali nikitegemea wanafikiria kama akili yangu kuhusiana na jiji la Dar, kumbe akilini mwa JK na viongozi matapeli ni hiyo hiyo win win situation!
Waswahili wanasema Ujinga ni kutoweza kufahamu maana na Upumbavu ni kupumbazwa na kauli tata ukashindwa kuchukua hatua zenye manufaa!..
Kwa hali hiyo kusema kweli najiona mtupu na serikali yetu wala sijui zuri ni lipi linatakiwa kufanywa!.....
Shukran, umenitoa kizani.
 
Hayo ndiyo mauzo kamili ya nchi, hilo linaitwa Azimio la Kigamboni

Siku zote viongozi hawa wanafanya maamuzi yaliyojaa ubinafsi na uroho waliokuwa nao wa utajiri wa haraka haraka. Halafu tukiwakosoa wanakuja juu eti tusiwakosoe kwa sababu hatuijui Tanzania!!!! Watasema lolote lile ili kukidhi ufisadi wao.
 
Nimeona niibue hii mada kutoka huko kwenye makarabrasha ya zamani kutokana na nilichokisikia leo Radio Cloud's, ishu imekuwa serious, kwani kuna mzee mmoja alikuwa analalamika kwamba kanyimwa mkopo Bank kwa sababu ya huo mradi unaotakiwa kuanzishwa huko Kigamboni. Kwa maana hiyo hizo barua hata Bank zimepelekwa ili wakazi wa kigamboni wasipewe mkopo kwa kutumia hati zao za kigamboni.

Inasikitisha.
 
Nimeona niibue hii mada kutoka huko kwenye makarabrasha ya zamani kutokana na nilichokisikia leo Radio Cloud's, ishu imekuwa serious, kwani kuna mzee mmoja alikuwa analalamika kwamba kanyimwa mkopo Bank kwa sababu ya huo mradi unaotakiwa kuanzishwa huko Kigamboni. Kwa maana hiyo hizo barua hata Bank zimepelekwa ili wakazi wa kigamboni wasipewe mkopo kwa kutumia hati zao za kigamboni.

Inasikitisha.

Hehehe! Nielezeani jamani hivi hata maeneo ambayo hayajapimwa pale Kigamboni yanahusika na hii STOP? Isije nikanunua tofali na kuzifikisha site then napigwa stop wakati nimeshaingia hasara.

Inabidi serikali kupitia Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi waendeshe vipindi maalumu kwenye vyombo vya habari vya elektroniki (TV na Redio) ili tupate kuelewa kikamilifu na si habari za juu juu ambazo ni vipand vipende.
 
Hehehe! Nielezeani jamani hivi hata maeneo ambayo hayajapimwa pale Kigamboni yanahusika na hii STOP? Isije nikanunua tofali na kuzifikisha site then napigwa stop wakati nimeshaingia hasara.

Inabidi serikali kupitia Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi waendeshe vipindi maalumu kwenye vyombo vya habari vya elektroniki (TV na Redio) ili tupate kuelewa kikamilifu na si habari za juu juu ambazo ni vipand vipende.

Kuna mwenyekiti wa kigamboni pia alikuwa anahojiwa leo subuhi, akasema wao wameshaletewa barua tangu mwezi uliopita yaani mwezi wa 10 kuwa waliojenga sawa na ambao hawajajenga basi wasijenge. Na pia tangazo lilishatolewa kwenye gazeti la mwananchi.
 
Sina matatizo na huo mradi wao.nachotaka kujua ni wapi watanipa kiwanja kingine jamani.nina kiwanja hapo vijibweni na sasa ndio nimeona na yeye ipo huko kwenye mradi wao,nimeweka na kakibanda tena ndio kanakaribia kwisha.mliopo nyumbani jamani tusaidie kutupa hizo barua zilizopo hku kwa wenye viti wa mitaa ili tujue tunaanzia wapi kudai haki wandugu
 
Nimepita siku si nyingi barabara ya kutoka kibada, Kisarawe II,mwasonga,Dar es salaam Zoo,mpaka Tundwi songani. Barabara imejengwa vizuri sana, sio ya lami,ila imejengwa kwa ubora wa juu sana,sehemu kubwa ya barabara hiyo ni pori hakuna nyumba. Nilipouliza kulikoni manispaa ya Temeke kujenga barabara ya nguvu hivi huku ilihali mitaa ya Dovya kuliko na watu wengi barabara mbaya,jibu niliambiwa kuwa kule inaandaliwa Dsm mpya. Cha msingi kununua kiwanja Kigamboni na upande wote wa pwani hiyo ni hatari kwa sasa. Nenda ardhi wakusaidie ramani ya eneo hilo.
 
Nimepita siku si nyingi barabara ya kutoka kibada, Kisarawe II,mwasonga,Dar es salaam Zoo,mpaka Tundwi songani. Barabara imejengwa vizuri sana, sio ya lami,ila imejengwa kwa ubora wa juu sana,sehemu kubwa ya barabara hiyo ni pori hakuna nyumba. Nilipouliza kulikoni manispaa ya Temeke kujenga barabara ya nguvu hivi huku ilihali mitaa ya Dovya kuliko na watu wengi barabara mbaya,jibu niliambiwa kuwa kule inaandaliwa Dsm mpya. Cha msingi kununua kiwanja Kigamboni na upande wote wa pwani hiyo ni hatari kwa sasa. Nenda ardhi wakusaidie ramani ya eneo hilo.

Tatizo kwa sisi ambao tumeshanunua na tumeanza kujenga na tupo katika sehemu nzuri tu kwenye ujenzi, Sijui nini hatma yetu. na hata wakija wakatulipa watatupeleka wapi kama sio kukudidimiza ndani zaidi i mean nnje ya mji??????
 
Tatizo kwa sisi ambao tumeshanunua na tumeanza kujenga na tupo katika sehemu nzuri tu kwenye ujenzi, Sijui nini hatma yetu. na hata wakija wakatulipa watatupeleka wapi kama sio kukudidimiza ndani zaidi i mean nnje ya mji??????


Mkuu,

Pole sana kwa wasiwasi uliokuwa nao. Ila nina imani iwapo umeshajenga basi fidia inaweza kukutosha kuhamia sehemu nzuri iwapo utakuwa mbishi.

Kwa wengine ambao wanatarajia kujenga huko Kigamboni na maeneo mengine; zama za kujenga kwenye kiwanja kisicho na Hati au Barua ya Ofa zimepita kitambo. Ni hatari sasa hivi kujenga kabla ya kupima na kuomba kibali cha kujenga, hata huko Manispaa hawana tena huruma.
 
Mkuu,

Pole sana kwa wasiwasi uliokuwa nao. Ila nina imani iwapo umeshajenga basi fidia inaweza kukutosha kuhamia sehemu nzuri iwapo utakuwa mbishi.

Kwa wengine ambao wanatarajia kujenga huko Kigamboni na maeneo mengine; zama za kujenga kwenye kiwanja kisicho na Hati au Barua ya Ofa zimepita kitambo. Ni hatari sasa hivi kujenga kabla ya kupima na kuomba kibali cha kujenga, hata huko Manispaa hawana tena huruma.

Ofa ipo, ila Hati ndio ipo kwa commissioner (Ardhi) inangoja signature. ila bulding permit ndio sina.
 
Jamani hii habari ya Kigamboni kweli na ni serious kuliko mnavyodhani. Mradi utaanzia feri navy yote, vijibweni, huko beach yote mpaka kibugumo. Watakaopona ni wale wa mradi wa viwanja 20000, Mzee Jumbe, Shule, Hospitali na vituo vya jamii basi. Wengine wote watalipwa fidia na kuhamishwa.

Kinachonishangaza mimi ni kuwa mpaka sasa serikali bado inatafuta mwekezaji wa ku invest ktk mradi huo,nia ni kuifanya Kigamboni iwe ni satelite town.

Tusali na tuombe hizo fidia wajanja wasizi EPALISE
 
Ofa ipo, ila Hati ndio ipo kwa commissioner (Ardhi) inangoja signature. ila bulding permit ndio sina.

Kama Ofa yako ipo ktk Mradi wa viwanja 20,000 dont worry!!!..

na Kwa wale wenye Hati au wapo ktk process za Hati, ktk Plot za Serikali za 20,000 za Kigamboni.....Lazima u-submit Map manispaa waipitishe kabla hujaanza kujenga, ukijenga bila Ramani nyumba yako Itavunjwa!!!...Usije ukalalamika...Muda wa Kujenga Kiholela UKOME...

Tunawashauri Serikali kuwa Wenye Mashamba yao na Nyumba zao Kigamboni MSIWADHULUMU kama Mlivyofanya kule Kurasini.
 
Kama Ofa yako ipo ktk Mradi wa viwanja 20,000 dont worry!!!..

na Kwa wale wenye Hati au wapo ktk process za Hati, ktk Plot za Serikali za 20,000 za Kigamboni.....Lazima u-submit Map manispaa waipitishe kabla hujaanza kujenga, ukijenga bila Ramani nyumba yako Itavunjwa!!!...Usije ukalalamika...Muda wa Kujenga Kiholela UKOME...

Tunawashauri Serikali kuwa Wenye Mashamba yao na Nyumba zao Kigamboni MSIWADHULUMU kama Mlivyofanya kule Kurasini.

Mimi nadhani kuzungumza na kufikwa na hili jambo nia mambo mawili tofauti,hapa kunawatu wana zungumza tu bila ya kutoa suluhisho ya issue nzima.
Kuna mchangiaji mmoja alisema na ndio ilivyo kwamba hivyo vilivyo ndani ya mradi(KISOTA,KIBADA) haviguswi na zoezi zima la la NEW CITY,ingawa vimo kwenye eneo zima la mradi huu wa NEW CITY (sababu vilipimwa na kuuzwa na serikali yenyewe)
Sasa kazi ipo kwa sisi tulio ndani ya eneo hilo amabalo ni karibu kilometa 10 kutoka Ferry hadi shamba la NAFCO(shamba la MANJI) wengi wetu tulishapima na kupata hati za maeneo yetu ila kwa mujibu wa barua hizo ambazo Ndg.DOMO KAYA anasema zimetoka mwezi wa 10,zinatoa katazo kwamba tusiendeleze ikiwa ya maana ya kujenga ama kupima kwa wale ambao hawajafanya hivyo bado.

Sasa mimi nauliza hivi, tulipo kua tukipima hizi sehemu tulionyeshwa ramani za mipango miji ambazo tayari maeneo haya tuliyonunua na kupima yalitoa ruhusa kwa ajiri ya makazi na OFFER na HATI zilitolewa kwa minajiri hayo,sasa nini kimetokea mpaka mipango hii ya awali kubadilika kwa hii NEW CITY wakati tayari ramani zilikuwapo?
AU ujio wa BUSH (rais wa marekani) ndio chanzo cha haya yote,maana mambo yanazungumzwa?
Hao wahusika,MAAFISA MIPANGOMIJI,WAHANDISI na HATA MAAFISA ARDHI hawajuu nini kimetokea mpaka KATAZO kutolewa tena GHAFLA au MMESHAUZA KIGAMBONI KWA WAMEREKANI????
 
Wakuu JF imetoa mwanga kwa serikali kuhusiana na mji wetu wa Dar hivyo kuna dalili kubwa kuwa mchoro wa Mji wa Dar unafikiria kupanuka kwa mji... Ukitazama mji wetu utaona kuwa sehemu (viwanja) nyingi za maofisi ya services mbalimbali na biashara zimepungua zaidi ya mitaa michache ya mjini wakati residential areas zinazidi kupanuka zaidi na viwanja bado vipo..

Kwa hiyo, yawezekana kabisa wakuu zangu kuwa huo mji mpya upo ktk kufikiria matanuzi, lakini binafsi kama nilivyosema huko nyuma lile sehemu la Bandari yetu ndilo lingetumika zaidi kupanuliwa kwa mji kuliko Kivukoni..
Huko Kivukoni ilitakiwa uwe mji wa Utalii tu.. Mahotel, viwanja vya Golf, Yatch Clubs na kadhalika kuvuta watalii nchini kwani maswala ya mbuga za Wanyama na kupanda milima ni Utalii uliopitwa na wakati.. Siku hizi wataliii wanakuja nchi zetu kutanua, kujipumzisha beach, sehemu peaceful, stressfree! baada ya kazi ngumu za mwaka mzima nchi za baridi...Maswala ya kufukuzana na Simba yamepitwa, siku hizi Simba wanakata viuno ktk Ma Zoo!

Sasa kama kweli mnaliweka Taifa mbele ya maisha yenu wenyewe nadhani swala hili halitawapeni taabu sana kufikiria, unless kama nilivyoambiwa kuwa upo uwezekano viwanja vyenu vinatakiwa na wakubwa!
 
Wakuu JF imetoa mwanga kwa serikali kuhusiana na mji wetu wa Dar hivyo kuna dalili kubwa kuwa mchoro wa Mji wa Dar unafikiria kupanuka kwa mji... Ukitazama mji wetu utaona kuwa sehemu (viwanja) nyingi za maofisi ya services mbalimbali na biashara zimepungua zaidi ya mitaa michache ya mjini wakati residential areas zinazidi kupanuka zaidi na viwanja bado vipo..

Kwa hiyo, yawezekana kabisa wakuu zangu kuwa huo mji mpya upo ktk kufikiria matanuzi, lakini binafsi kama nilivyosema huko nyuma lile sehemu la Bandari yetu ndilo lingetumika zaidi kupanuliwa kwa mji kuliko Kivukoni..
Huko Kivukoni ilitakiwa uwe mji wa Utalii tu.. Mahotel, viwanja vya Golf, Yatch Clubs na kadhalika kuvuta watalii nchini kwani maswala ya mbuga za Wanyama na kupanda milima ni Utalii uliopitwa na wakati.. Siku hizi wataliii wanakuja nchi zetu kutanua, kujipumzisha beach, sehemu peaceful, stressfree! baada ya kazi ngumu za mwaka mzima nchi za baridi...Maswala ya kufukuzana na Simba yamepitwa, siku hizi Simba wanakata viuno ktk Ma Zoo!

Sasa kama kweli mnaliweka Taifa mbele ya maisha yenu wenyewe nadhani swala hili halitawapeni taabu sana kufikiria, unless kama nilivyoambiwa kuwa upo uwezekano viwanja vyenu vinatakiwa na wakubwa!


Taifa kwanza linatakiwa liweke maswahi ya wananchi wake mbele na sio ya wawekezaji uchwala,machifu wazamani ndio walitoa ardhi yao kama personal gift kwa wazungu,na hatuhitaji kwenda huko katika miaka hii.
Walishchola ramani,nakilichobakia kwa wao waseme wanataka watu tuweke majengo ya namna gani,siku hizi hauitaji mzungu ili mji uwe na maghorofa angalia kariakoo?kama tatizo ni maghorofa
 
Back
Top Bottom