Si vibaya mtu ukikumbuka ulipotoka.
Nakumbuka siku ya kwanza kukanyaga Pugu ilikuwa tarehe 5 mwezi februari. ilikuwa ni siku ya mapumziko (public holiday), siku ya kuzaliwa CCM(Kwa miaka hiyo tarehe ya kuzaliwa CCM ilikuwa inaadhimishwa kitaifa na inakuwa ni mapumziko).
Nilipangiwa bweni la Maendeleo 2 na baada ya muda nilichaguliwa kuwa dom monitor. Kipindi kile pale Pugu mbele kidogo ya jiko kulikuwa na mradi wa nguruwe ambapo wanafunzi walikuwa wanawahudumia bila kujali wewe ni wa dini gani, mimi na wenzangu tulisimama kidete kupinga mradi ule hadi ukafutwa.
Nakumbuka shida ya maji ya kunywa pale shuleni na ilikuwa inatupasa twende pondi ya mzee wa shamba kuchota maji na kuja kuyafungia katika makabati yetu maarufu kama lockers.
Maisha ya bweni yalikuwa ni mazuri sana, ratiba ya chakula ilikuwa ni kama ifuatavyo: Tulikuwa tunakunywa uji saa 4, saa nane ugali maharage na usiku pia isipokuwa siku ya jumatano usiku ilikuwa ni siku ya wali maharage na alhamisi mchana tunapewa matunda(ndizi) na usiku wa alhamisi ni ugali kwa nyama(kipindi kile nyama tulikuwa tunaita kishoka).
Vyoo vya Pugu maarufu kwa jina la bettle vilikuwa vina harufu kali sana na ilikuwa inatupasa tuvue mashati kabla ya kuingia vinginevyo utanuka mpaka bwenini/darasani kwa harufu.
Pugu!!!!!!! nakumbuka mengi, walimu wangu akina Cobra "hilo ni jina la utani, jina lake halisi silikumbuki", mwl Charwe(huyu aliwahi kuninyang'anya viatu vyangu vya ngozi nilivyokuwa nimepewa na mzee wangu ambaye alikuwa ni afisa wa jeshi), mwl Juma Wasiwasi, Mwl Maliki, Mwl Shangwe, Mwl mukuru, marehemu mwl Swai, mabagala(sijui yupo wapi siku hizi), Mwl Mamilo, huyu alinikamata na "feki" la Physics NECTA na hatimae nikafutiwa matokeo yangu ya NECTA. Nimekumbuka sana shule yangu, ambayo imesaidia kujenga historia yangu.
WANA PUGU, MNAKUMBUKA NINI PUGU!!!! LET'S SHARE
Nakumbuka siku ya kwanza kukanyaga Pugu ilikuwa tarehe 5 mwezi februari. ilikuwa ni siku ya mapumziko (public holiday), siku ya kuzaliwa CCM(Kwa miaka hiyo tarehe ya kuzaliwa CCM ilikuwa inaadhimishwa kitaifa na inakuwa ni mapumziko).
Nilipangiwa bweni la Maendeleo 2 na baada ya muda nilichaguliwa kuwa dom monitor. Kipindi kile pale Pugu mbele kidogo ya jiko kulikuwa na mradi wa nguruwe ambapo wanafunzi walikuwa wanawahudumia bila kujali wewe ni wa dini gani, mimi na wenzangu tulisimama kidete kupinga mradi ule hadi ukafutwa.
Nakumbuka shida ya maji ya kunywa pale shuleni na ilikuwa inatupasa twende pondi ya mzee wa shamba kuchota maji na kuja kuyafungia katika makabati yetu maarufu kama lockers.
Maisha ya bweni yalikuwa ni mazuri sana, ratiba ya chakula ilikuwa ni kama ifuatavyo: Tulikuwa tunakunywa uji saa 4, saa nane ugali maharage na usiku pia isipokuwa siku ya jumatano usiku ilikuwa ni siku ya wali maharage na alhamisi mchana tunapewa matunda(ndizi) na usiku wa alhamisi ni ugali kwa nyama(kipindi kile nyama tulikuwa tunaita kishoka).
Vyoo vya Pugu maarufu kwa jina la bettle vilikuwa vina harufu kali sana na ilikuwa inatupasa tuvue mashati kabla ya kuingia vinginevyo utanuka mpaka bwenini/darasani kwa harufu.
Pugu!!!!!!! nakumbuka mengi, walimu wangu akina Cobra "hilo ni jina la utani, jina lake halisi silikumbuki", mwl Charwe(huyu aliwahi kuninyang'anya viatu vyangu vya ngozi nilivyokuwa nimepewa na mzee wangu ambaye alikuwa ni afisa wa jeshi), mwl Juma Wasiwasi, Mwl Maliki, Mwl Shangwe, Mwl mukuru, marehemu mwl Swai, mabagala(sijui yupo wapi siku hizi), Mwl Mamilo, huyu alinikamata na "feki" la Physics NECTA na hatimae nikafutiwa matokeo yangu ya NECTA. Nimekumbuka sana shule yangu, ambayo imesaidia kujenga historia yangu.
WANA PUGU, MNAKUMBUKA NINI PUGU!!!! LET'S SHARE