Tutafika
JF-Expert Member
- Nov 4, 2009
- 1,443
- 631
Naomba tukumbushane matukio, hoja na vioja vilivyotokea ambavyo haijulikani hitimisho ilikua ni nini. Hii itatusaidia watanzania kuachana na kasumba ya kwenda na upepo ili tuweze kufikia suluhu katika matatizo yanayotukabili kama nchi.
Kwa kuanzia:
1. HOJA YA UFISADI TANROADS:
Katika hili, aliekuwa anaiongoza hii taasisi ndugu Mrema alisemwa sana, alitukanwa sana, alidharirishwa sana na alifedheheshwa sana (kasoro tu hakuachia ngazi). Baada ya huyu jamaa kumaliza mkataba wake simsikii tena kana kwamba hakuna baya alilo lifanya. Sasa je, alisingiziwa au ni kweli?,
2. HOJA YA UFISADI WA MNADHIMU JWTZ:
Huyu nae ilianza kushuka mvua ya tuhuma kwamba kachukua hela nyingi sana za taifa hili na kwenda kuzificha Afrika ya kusini. Hii hoja iliahirishwa (invisible anahusika), je imefikia wapi?
3. TUKIO LA MAUAJI YA NDUGU MWAIKUSA (Mhadhili wa chuo kikuu cha dar es salaam)
Mengi yalisemwa hapa kwamba Rais Kagame anahusika, na polis waliahidi kufanyia kazi haraka. Hili tukio kwa mara ya mwisho taarifa nilio nayo ni kwamba wauaji walikamatwa lakini hakuna aliekuwa tayari kusema ni kina nani hao. Je mahakamani watafikishwa lini na kwa sasa wapo gereza gani?
4. TUKIO LA KULETWA ALSHABAB KUMUUA MWAKYEMBE
Hili ni kati ya mambo ambayo yalitolewa ushahidi wa kina na mwakyembe mwenyewe polisi, wamefikia wapi?, achilia mbali hili la sasa la kupewa sumu ambalo wanasema hawawezi kuchunguza kwa sababu hawana ushahidi
5. TUHUMA ZA UFISADI KWA BWANA ROSTAM
Hivi tuhuma juu ya huyu bwana ni wivu unasumbua maskini wa tanzania au ni kweli? Naona baada ya kuwaachia ubunge wenu mambo sasa ni shwari kabisa!
6. MADAWA YA KULEVYA
Hili nadhani ni sugu na halisemeki vizuri tangia enzi hizo. Ngoja mi niongelee mawili tu, kwanza ni tukio la kubambikiwa kesi bwana Reginard Mengi na mtoto wake. Hili aliweka wazi wahusika tena kwa majina na vyeo, sijui liliishaje. Pili ni madawa yaliyokamatwa kule mbeya halafu baadae polisi wakayaiba, imekuwaje hapo? na je madawa ambaya yanakamatwa kila mara yanaenda wapi? na watuhumiwa mbona hatuwaoni mahakamani?. yaani hata kesi moja ya madawa ya lulevya siisikii kabisa!
7.......................,
Kwa kuanzia:
1. HOJA YA UFISADI TANROADS:
Katika hili, aliekuwa anaiongoza hii taasisi ndugu Mrema alisemwa sana, alitukanwa sana, alidharirishwa sana na alifedheheshwa sana (kasoro tu hakuachia ngazi). Baada ya huyu jamaa kumaliza mkataba wake simsikii tena kana kwamba hakuna baya alilo lifanya. Sasa je, alisingiziwa au ni kweli?,
2. HOJA YA UFISADI WA MNADHIMU JWTZ:
Huyu nae ilianza kushuka mvua ya tuhuma kwamba kachukua hela nyingi sana za taifa hili na kwenda kuzificha Afrika ya kusini. Hii hoja iliahirishwa (invisible anahusika), je imefikia wapi?
3. TUKIO LA MAUAJI YA NDUGU MWAIKUSA (Mhadhili wa chuo kikuu cha dar es salaam)
Mengi yalisemwa hapa kwamba Rais Kagame anahusika, na polis waliahidi kufanyia kazi haraka. Hili tukio kwa mara ya mwisho taarifa nilio nayo ni kwamba wauaji walikamatwa lakini hakuna aliekuwa tayari kusema ni kina nani hao. Je mahakamani watafikishwa lini na kwa sasa wapo gereza gani?
4. TUKIO LA KULETWA ALSHABAB KUMUUA MWAKYEMBE
Hili ni kati ya mambo ambayo yalitolewa ushahidi wa kina na mwakyembe mwenyewe polisi, wamefikia wapi?, achilia mbali hili la sasa la kupewa sumu ambalo wanasema hawawezi kuchunguza kwa sababu hawana ushahidi
5. TUHUMA ZA UFISADI KWA BWANA ROSTAM
Hivi tuhuma juu ya huyu bwana ni wivu unasumbua maskini wa tanzania au ni kweli? Naona baada ya kuwaachia ubunge wenu mambo sasa ni shwari kabisa!
6. MADAWA YA KULEVYA
Hili nadhani ni sugu na halisemeki vizuri tangia enzi hizo. Ngoja mi niongelee mawili tu, kwanza ni tukio la kubambikiwa kesi bwana Reginard Mengi na mtoto wake. Hili aliweka wazi wahusika tena kwa majina na vyeo, sijui liliishaje. Pili ni madawa yaliyokamatwa kule mbeya halafu baadae polisi wakayaiba, imekuwaje hapo? na je madawa ambaya yanakamatwa kila mara yanaenda wapi? na watuhumiwa mbona hatuwaoni mahakamani?. yaani hata kesi moja ya madawa ya lulevya siisikii kabisa!
7.......................,