FiQ
JF-Expert Member
- Feb 11, 2011
- 477
- 76
Pamoja na John Samwel Malecela kuwa mwanasiasa mwenye nguvu ndani ya chama cha Mapinduzi CCM na Serikalini lakini juhudi zake za kutafuta kuteuliwa kuwa mgombea urais ziligonga mwamba kwa vipindi vyote viwili vya 1995 na 2005.
Sababu gani zilizofanya ashindwe:
Mbio za Malecela 1995
Ingawa Malecela alikuwa ni mgombea aliyekubalika kati ya wagombea wengine wa CCM lakini Baba wa Taifa JK Nyerere hakufurahishwa na kitendo cha Waziri Mkuu wakati huo Mh. Malecela kuruhusu hoja ya Serikali tatu iletwe bungeni, vile vile hakufurahishwa na kitendo cha yeye kujihusisha na Zanzibar kujiunga na OIC. Kwa hiyo kitendo hicho kilimkera sana Mwalimu hadi akafikia kumtaja Malecela kuwa ni muhuni na mroho wa madaraka. Nanukuu mwandishi mmoja,
"Nyerere saw him as someone who was driven by personal ambition in his quest for the presidency and warned CCM leadership that he would not even attend the party congress if Malecela was on the short list of possible candidates".
Vile vile kulikuwa na hear say kwamba Malecela alikuwa groomed na nchi moja ya kiarabu ili kufanikisha mbio zake za urais na ilisemekana kuwa ilibidi abadili jina(dini) na kujiita Jumanne Samwel Malecela. Kutokana na msimamo wa Mwalimu jina lake halikupendekezwa na Mkapa akaibuka kidedea.
Mbio za Malecela 2005
Baada ya kutofanikiwa lengo lake 1995 Malecela hakukata tamaa alionekana kutokuwa karibu sana na Mwalimu Nyerere na hasira hizo zilienda mbali na kusababisha hadi kwa familia yake imchukie Mwalimu na baadhi ya viongozi wa juu wa CCM, kiasi kwamba katika kinyang'anyiro cha mwaka 2005 jina lake halikuvuka hata raundi ya kwanza wakati Mh. Kikwete alipoibuka kidedea. Inasemekana kinyongo cha Malecela kukosa urais kwa safari mbili kiliendelea hadi kusababisha makundi ndani ya chama.
Kwa vile wakati ule alikuwa bado na cheo cha Makamu Mwenyekiti rais Kikwete kwa kuona hali ilivyo ndani ya chama ikabidi atafute mbinu ya kumtoa pale, akasema anataka asaidiwe kwenye kiti kile cha M/M/kiti na damu changa lakini matokeo yake mwaka 2007 akateuliwa Pius Msekwa kiasi kwamba watu wakajiuliza damu changa iko wapi. Kwa vile ilionekana Malecela bado ana nguvu ndani ya chama uongozi wa juu wa chama katika kumpunguza nguvu zaidi ukafanya juu chini ili Malecela asishinde kwenye kura za maoni za ubunge jimbo la Mtera.
Mimi binafsi ingawa sikuwa kwenye michakato hii toka 1995 enzi za Mwalimu hadi 2005 enzi za Mkapa/Kikwete lakini nafarijika kwamba huyu Mzee hakupata kutuongoza kwenye nafasi ya urais kwa vile kama alivyosema Mwalimu ni Mbinafsi,Muhuni, roho isiyo na utu'You Can Go to Hell' alitaka kutuingiza OIC, kama si Nyerere kuliona hilo mapema tungejuta.
I say again thank God he is/was not a President of Tanzania.
Mkuu umenena then it simz chuki na kwa Mwl imesharithishwa kwa kizaz chote cha Malecela man hata mkewe willie yupo humu kwa Id ya Field Marshal Es, anamponda sana mwl na kudai mwl alikua anagombea na kivuli,Anamtetea sana mkwewe kwa hasira zao ya kukosa Urais. We ngoja utamuona humu muda si mrefu maadamu thread imemgusa mkwewe so lazima bibie ataingia tu.