Tukumbushane: Hivi kwanini Nyerere alikataa J. S. Malecela asigombee urais kupitia CCM

Jasho la Damu

JF-Expert Member
Mar 10, 2011
956
120
Wasalaam JF,

Tumekuwa tukiamini na kuendelea kuamini na ukweli ndivyo ulivyo kuwa muasisi wa taifa hili la Tanzania, Baba wa Taifa Mwl J. K Nyerere ndiye aliyepata kuwa rais muadilifu na mwenye uchungu na umaskini wa watz wanyonge hivyo alipewa heshima zote ndani ya chama na Serikali.

Nimekuwa nikijiuliza sana kwanini Nyerere alimkataa Malecela asigombee nafasi ya kuwania Urais kupitia chama cha mapinduzi,ccm? mpaka alitishia kurudisha kadi yake ya uanachama endapo Malecela asingejitoa.

Anayefahamu atujuze
 
Ungetafuta kitabualichoandika kuhusu suala hilokinaitwa,viongozi wetu na hatima ya tanzania....
ok mkuu nitakitafuta ila kama una dondoo zozote juu ya hili tudokezee japo kidogo najua kuna watu wana hamu ya kufahamu na uwezekan wa kukipata hicho kitabu ni vigumu.
 
Moja ya kitu kilichomchukiza nyerere ni ile jama alipruhusu ile G58( Kama sikoesei) Ya kina Njelu Kasaka kuruhusu nyufa a muungano kujadiliwa....... Hilo ni moja tu.

But nadhani mengine Nyerere aliyajua ambyo watu wengi hawayajui ndio maana hata baada Nyerere waliofuata pia walimchomoa mzee kwa style za kidiplomasia. So sio sula la nyerere tu mbona hata nyerere alivyokuwa marehemu walimchomoa?

Alivyokuwa Malechelela kipindi kile bila Nyerere Mwinyi alikuwa mzee wa ruksa tu muda wake uishe. Ndio kama sasa uavyoona Lowasa na JK bila Bunge nadhani Lowasa alishajisimika sawa sawa. Sasa hivi jamaa karudishwa nyuma lakini hajakata tamaa

Mzee wetu malechela nadhani kakubali yaishe kilichbki ni yeye kuamua ataside na upande gani kwa maslahi ya wananchi au maslahi yake binafsi. Anajua yeye
 
Mwalimu alisema mengi kule kitabuni juu ya Malecela na Lowasa pia .So kwa kuwa kuna kitabu tupunguze mjadala soma kitabu then uje .
 
Wasalaam JFTumekuwa tukiamini na kuendelea kuamini na ukweli ndivyo ulivyo kuwa muasisi wa taifa hili la Tanzania, Baba wa Taifa Mwl J. K Nyerere ndiye aliyepata kuwa rais muadilifu na mwenye uchungu na umaskini wa watz wanyonge hivyo alipewa heshima zote ndani ya chama na Serikali. Nimekuwa nikijiuliza sana kwanini Nyerere alimkataa Malecela asigombee nafasi ya kuwania Urais kupitia chama cha mapinduzi,ccm? mpaka alitishia kurudisha kadi yake ya uanachama endapo Malecela asingejitoa.Anayefahamu atujuz
The reson is that he kept calling everbody 'mbuzi' like he did in here.https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/151496-mazungumzo-na-dr-slaa-maswali-na-majibu-7.html
 
Sababu ni nyingi. Nyengine ziko humo kwenye hako kajitabu, nyengine hazipo. Malecela inawezekana asingekua kiongozi muafaka wa Tanzania, lakini amekashifiwa sana mzee wa watu. Ukisoma kitabu cha Mwalimu, hio ni one sided opinion. Unapata opinion ya MTU aliemhukumu Malecela. Kwa bahati mbaya Malecela hana uwakilishi kwenye forum, it would have been better if we heard the other part of the story.

Mie nasema kwamba Mwalimu kama mtu mwengine, hakuwa Malaika. Kuna watu aliwapenda, kuna watu aliwapendelea na vivyo hivyo kuna watu aliwachukia na kuna watu ali wa victimise.

Hivi wana jamii, mnayo habari kwamba wakati tupo katika kilele cha kutekeleza Azimio la Arusha Sir George alipata nafasi ya kuwa Mkurugenzi CDA. Sir George alikuwa akipeleka suti zake laundry Nairobi, na mwalimu alikuwa anafahamu na hakumwambia fyoko. huo ndio utaratibu.

Tumuombee dua hayati Nyerere
 
Namheshimu Mzee huyu kwa jambo moja sijawaikumuona public kujibu tuhuma zake zilizotolewa na mwalimu dhidi yake hivyo kwa waelevu ni kukubali udhaifu wako.

Anamakosa makubwa ambayo kwa mtanzania wa kawaida kujua maamuzi aliyofanya Mheshimiwa huyu yamelikosti Taifa ni mdogo sana.ni mzuri UPSTAIRS na mwanadiplomasia mwenye ushawishi.Kuna maamuzi ya msingi aliyayatenda akuangalia utanzania [Uafrika].Na hili limekua ni tatizo la viongozi wengi wanakutana sana na wazungu wanasahau Uafrika na kuanza kufikilia kizungu na kutenda kizungu kwa mali na mazingira ya waafrika.

Anauzoefu mkubwa wa mshikemshike wa mabo mengi yawahusuyo wakubwa wengi na kiu ama ndoto ya kukaa kwenye kiti ilikatika,kwa asilimia mia naamini ilikuwa sawa kwa kuwa ndani ya moyo wake kiu yake haikumezwa na kuwapa maisha bora na ustawi watanzania wa Afrika hii.

Ni mwasisi wa mambo mengi,mazuri na mengine mabovu ambayo yamewatajarisha wengine mpaka wamekuwa mwiba mchungu kwenye jamii.Bado nafasi hipo na uzima upo ila kwa utu uzima wake huo tunaitaji kitabu akitwambia uzoefu wake wa Mazuri na Mabaya juu ya maamuzi yake.Ikibidi conffesion, na kukili kuwa Mwalimu alimuone na hivyo akmtendea haki,ukizingatia kuwa wananchi walimwamini sana Mwalimu hivyo imani hiyo ya Mwalimu uenda ilitumika vibaya kumuhukumu na hivyo kumnyima haki yake ya kulitumikia Taifa kupitia kiti cha enzi.

Kama kweli ndie aliyesimamia nn...na hivyo kuuzwa kwake,kulimuuzi sana Mwalimu natumaini dhambi ile ndio msingi wa Mwalimu kuona hafai,na ndio maana uenda asiweze kujibu tuhuma hizo kamwe na daima kubaki siri ya wanaojua issue hiyo ya maliasili safi Mungu aliyotupatia watz.

Ila atauondolee kichomi kilichopandia watz kupitia mgongo wake na kuweza kuwa tajiri wa kutupa ndani ya kivuli cha mzee.
 
Wakuu nawasoma sana lkn wengi naona mnanipa dondoo za juu juu tu khs mtifuano ulivyokuwa. Niliwai kusikia Malecela alitaka kuuza nchi kwa waarabu wa OIC na Mkapa akanyaka hizo nyaraka na kuzipeleka kwa Nyerere ndio ikawa shida hv ni kweli? na hicho ndicho kilichompa urais bwana B.Mkapa.
 
Back
Top Bottom