Mwanajamii
JF-Expert Member
- Mar 5, 2008
- 7,063
- 68
Wanaharakati wa haki za kibinadamu wa Dar es Salaam pengine kwa kusukumwa na uzalendo , ushabiki wa kisiasa au vyote wanaandaa maandamano ya kupinga kulipwa kwa tozo ya zaidi ya Ths. Bilioni 110 kwa Kampuni ya Dowans. Wapo wanasiasa wa chama tawala na wa vyama vya upinzani ambao wanaunga mkono harakati za taasisi hiyo kupinga malipo ya tozo hiyo.
Wakati tunaangalia hayo tukubali kwamba nchi hii inaongozwa na utawala wa sheria na bila kuangalia kama DOWANS ni ya nani tukubali kwamba Mahakama ya Kimataifa ya Biashara ICC ndiyo iliyotoza tozo hiyo kwa Kampuni hiyo.
Watanzania wengi ambao wanataka tozo hiyo isilipwe hawazingatii kwamba kama ICC ikiombwa na DOWANS inaweza kukaza hukumu na kuitangaza Tanzania kwenye vyombo vingine vya Kimataifa, hatua ambayo inaweza kusababisha mali za Tanzania zikakamatwa mpaka pale tozo hiyo itakapolipwa.
Suala lingine la msingi la kuzingatia ni kwamba kadri tunavyoendelea kubishana na kuendelea kukataa kulipa deni ndivyo riba itakavyozidi kukua na deni kuongezeka. Deni halisi lilikuwa bilioni 94 na sasa ni zaidi ya bilioni 110.
Tunachotakiwa kufanya ni kile ambacho serikali inafanya sasa cha kutafuta njia rahisi ya kukaa na Dowans na kupata ufumbuzi unaoweza kuipa nchi ahueni. Maandamano na kelele za majukwaani au kwenye vyombo vya habari hazina tija kwa sasa.
Naomba kutoa hoja.
Wakati tunaangalia hayo tukubali kwamba nchi hii inaongozwa na utawala wa sheria na bila kuangalia kama DOWANS ni ya nani tukubali kwamba Mahakama ya Kimataifa ya Biashara ICC ndiyo iliyotoza tozo hiyo kwa Kampuni hiyo.
Watanzania wengi ambao wanataka tozo hiyo isilipwe hawazingatii kwamba kama ICC ikiombwa na DOWANS inaweza kukaza hukumu na kuitangaza Tanzania kwenye vyombo vingine vya Kimataifa, hatua ambayo inaweza kusababisha mali za Tanzania zikakamatwa mpaka pale tozo hiyo itakapolipwa.
Suala lingine la msingi la kuzingatia ni kwamba kadri tunavyoendelea kubishana na kuendelea kukataa kulipa deni ndivyo riba itakavyozidi kukua na deni kuongezeka. Deni halisi lilikuwa bilioni 94 na sasa ni zaidi ya bilioni 110.
Tunachotakiwa kufanya ni kile ambacho serikali inafanya sasa cha kutafuta njia rahisi ya kukaa na Dowans na kupata ufumbuzi unaoweza kuipa nchi ahueni. Maandamano na kelele za majukwaani au kwenye vyombo vya habari hazina tija kwa sasa.
Naomba kutoa hoja.