mpayukaji
JF-Expert Member
- Oct 31, 2010
- 940
- 349
Taarifa zinazozidi kukoroga vichwa vya wabunge na wananchi za wabunge kuongezewa mshiko ni ushahidi kuwa hatuna wabunge bali wasasi ngawira. Tumeambiwa kuwa mapato ya mbunge kwa mwezi ni sawa na mshahara wa mwalimu wa shule ya msingi wa miaka mitatu na mshahara wa mwaka wa daktari. Je kwa uhovyo huu, kwanini tusiachane na dhana ya kuwa na wawakilishi wanaowakilisha matumbo yao na badala yake tuwe na wawakilishi wanaoweza kutimuliwa na waajiri wao yaani wananchi wakati wowote wakijisikia kufanya hivyo badala ya hawa wezi tunaopandikiziwa na vyama vya siasa.