Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,474
- 39,987
Na. M. M. Mwanakijiji (Tanzania Daima Jumatano Machi 18, 2009)
WAKAKAA katika kikao chao wakakubaliana; Tuwaambie kuhusu majenereta.
Huku wakiwa wametulia mahali wanapojua wao na Mungu wao wakasemezana; tuhakikishe mjadala unahusu majenereta na siyo mmiliki. Wakahimizana wakijua ya kwamba dili lao limeshtukiwa na Watanzania.
Ndiyo. Wakagongesheana gilasi wakijua kabisa ya kuwa wakibadili mkakati majenereta yatanunuliwa tu.
Tusisitize kuwa ni mapya, mmoja wao ambaye ni kinara kati yao akawaambia. Ndiyo! Mwingine akakubali. Tuwaambie majenereta tayari yako Tanzania na ni mapya kuna ubaya gani kuyanunua, wakapanga hoja zao. Tuhakikishe hawazungumzii Dowans. Wasizungumzie umiliki, wasizungumzie tuliingiaje; wasizungumzie tulitokea wapi. Wakakumbushana.
Ndiyo, sasa tuwaambie mmiliki wake basi. Likatolewa wazo.
Si we bwana jina lako tayari linaonekana, kubali tu na tutawapiga maneno yatakwisha. Mjadala wa mmiliki tutaufunga na turudi kuzungumzia majenereta, akasema mmoja wao kisha wakacheka. Wakakubaliana, wakatawanyika kama walivyokutana.
Mmiliki wa Dowans hatimaye akajitokeza na kukubali. Mara ya kwanza nilipozungumza naye alikataa kuijua Dowans; alikataa kabisa kusema amewahi hata kusikia; alikataa akisema kuwa kampuni hiyo haipo Uarabuni. Ndiyo! Alikiri kuwa na urafiki na Rostam lakini alikataa kabisa kuwa Rostam hakuhusika na ujio wa Dowans. Kwa sauti thabiti ya Brigedia Jenerali Suleiman Al-Adawi alikataa kuitambua Dowans! Nikakubali. Sikuridhika.
Nikapata fomu za BRELA (Wakala wa Usajili wa Makampuni na Utoaji wa Leseni). Nikaziangalia. Nikakuta jina lake, anuani yake, na sahihi yake. Nikasema alinidanganya. Nikasema mheshimiwa huyu aliniuzia kanyaboya. Nikatambua kuwa kama hakusema ukweli, kama hakutaka watu wajue ukweli, kuna kitu alikuwa anaficha. Kitu ambacho hakutaka watu wajue; nikakumbuka.
Nilipozungumza naye Jumamosi ile tulizungumza vizuri mpaka aliponiniuliza kama mimi ni Mtanzania. Nikamwambia ndiyo. Akaniuliza; unaandika mambo ya systems ya Tanzania? Nikamjibu ndiyo mkuu. Akasema; Oh. Haikuwa Oh ya nakuelewa; ilikuwa ni Oh ya kukata tamaa, ya kukutwa ukifanya usichotakiwa. Ni hapo nikakumbuka alipoanza kukataa kujibu maswali yangu; ambayo naamini ni ya Watanzania wengi.
Dowans ni kampuni ya nani? Je, anajua Kampuni ya Dowans Holdings ya Uarabuni? Vipi ile Dowans ya Costa Rica; ziko Dowans ngapi? Imeandikishwa wapi na nani? Mbunge wa Igunga Mhe. Rostam Aziz anahusika vipi? Hakutaka kujibu. Akabakia kunipiga mkwara; Usiandike jina la mtu ambaye huna uhakika naye. Nitakutumia wanasheria wangu waje wazungumze nawe. Nikakumbuka amenidanganya.
Jumamosi iliyofuata nikarudi tena nikiwa na ushahidi mkononi. Nikitambua kuwa kati ya Jumamosi ile na Jumamosi hii walifanya kikao chao cha makubaliano. Kikao cha kuhakikisha kuwa lolote liwalo majenereta ya Dowans yatanunuliwa na Jenerali lazima alipwe hela yake kwani ahadi ni deni. Walimuahidi kuwa mwisho wa mkataba serikali itanunua majenereta; walimpa moyo kuwa hata wakisitisha msaada kabla afungue kesi Paris ambayo hatutajiandaa kushinda ili hata kama tukikataa kununua bado tumlipe! Ndiyo! Nikarudi tena kumuuliza.
Nilipompata mara ya pili alikuwa mnyenyekevu zaidi, lakini safari hii alikubali. Hakuzungusha maneno. Ndiyo mimi, ndiyo namiliki Dowans, alisema. Nikamuuliza mbona ulinifunga kamba bosi? Akasema; sikujua nani anazungumza na mimi. Nikacheka. Nilikumbuka nilijitambulisha kwake kuwa naandika kwenye gazeti moja la Tanzania na ninaandika kuhusu suala la ufisadi linalohusisha Kampuni ya Dowans.
Akajibu maswali yangu mengi; mengine alishindwa kujibu kwa sababu tayari nilikuwa na majibu.
Dowans haikuingia kwa bahati mbaya. Ilialikwa. Ilialikwa na wakubwa wa nchi hii na wenye nguvu. Sijui nia yao ilikuwa nini, lakini kutatuta tatizo la nishati haikuwa mojawapo. Ulikuwa ni uamuzi wa kibiashara. Uamuzi wa nikune nami nikukune. Wakawaalika baada ya Richmond kushindwa; hawakuwa na kampuni ya nishati kwani Al-Adawi mwenye utajiri mkubwa tu anahusika zaidi na mambo ya ujenzi kama rafikiye Rostam.
Vyanzo vyangu vya uhakika vikanidokeza kuwa ni Rostam aliyemfuata kumpa mwaliko huo ambao naye aliupata kama ombi kutoka juu. Akaambiwa walete wala jamaa zako najua wana uwezo wa kuweza kufanya hivyo. Jamaa akashawishiwa alipohakikishiwa kuwa baada ya mkataba serikali itanunua. Hakuna mnunuzi mwingine, asiwadanganye mtu. Serikali isiponunua jenerali amekula hasara.
Hivyo wanajitahidi. Fungeni mjadala wa Dowans, na tuiache TANESCO ifanye maamuzi yake, akasema waziri mhusika. Kwa maneno mengine, acheni kuhoji-hoji. Tumeambiwa tunyamaze; tumeambiwa tusizungumzie Dowans tena, tuiache serikali ifanye maamuzi.
Tutakuwa tumelogwa tukifanya hivyo; tutakuwa tumelaaniwa tukikubali serikali ifanye mambo sirini; tutakuwa tuna kaugonjwa fulani tukiwaacha watawale wapendavyo. Nikasema kwa nini mtu wa porini na mvi hizi nahangaika na mambo ya Dowans? Kwa nini kujihangaisha kupambana na Goliathi na ka kombeo kangu ka kalamu? Kwa nini namimi nisikubali tu yaishe? Nikasema nitakuwa msaliti wa ndugu zangu! Nitakuwa ni msaliti wa nchi yangu, nitakuwa msaliti wa dhamira yangu!
Lakini pia nikajiuliza; hivi kuna ubaya gani wakiyanunua hayo majenereta na kuleta umeme unaohitajika sana? Kuna ubaya gani kutokujali mmiliki au jinsi gani alivyoingia nchini? Kama jamaa anakuja na dawa naye ni jambazi si tuchukue tu (rafiki yangu mmoja alinipa mfano huo). Nikakumbuka msemo wa kiswahili baniani mbaya kiatu chake ni dawa. Nikasikiliza hoja za watetezi wa tununue mitambo hii kwani itatupa umeme sasa na tayari iko nchini. Nikakumbuka kikao chao.
Lakini nikakumbuka kisa cha utotoni. Nilipokuwa mtoto kulikuwa na jamaa mmoja mwizi. Jamaa huyo alipita usiku akaiba jogoo letu moja kubwa na lililonona. Tulipoamka asubuhi tukatafuta jogoo wetu. Hayupo. Majira ya mchana, kuna mtu akapita akiita nauza jogoo, nauza jogoo. Tulipofungua mlango tulimuona huyo njemba mwizi mwizi na jogoo lake mkononi. Tukakimbia! Aliyekuwa mkubwa nyumbani ikabidi anunue jogoo huyo! Alikuwa ni yule yule jogoo wetu! Jamaa alirudia mara mbili, mwisho ikabidi tuwaambie wazazi!
Ndiyo, tukinunua mitambo ya Dowans itatusaidia kuwa na jogoo wetu; lakini mbona tulishamnunua na kuwa naye bandani? Nikakumbuka. Watanzania hawajali jogoo katoka wapi hata kama alikuwa ni wa kwao alimradi wakiambiwa anatotolesha vizuri! Tuko tayari kumnunua kwa gharama yoyote ile!
Ndipo nikakumbuka walipobadili sheria iliyotengenezwa kuidhoofisha TANESCO. Yaani wale wale waliotunga sheria ya kuidhoofisha TANESCO leo wanasimama kutuambia ati wanaitetea TANESCO! Nimebakia kucheka tu. Kama kweli wanataka kuisadia TANESCO wabadilishe sheria na kuruhusu kampuni yoyote inayotaka kuzalisha nishati ifanye hivyo na isambaze nishati hiyo yenyewe. Wakitaka kutumia nyaya za TANESCO au miundombinu, TANESCO ndiyo iwachaji. Mtashangaa!
Leo wametengeneza sheria ambayo wao wenyewe wamejihakikishia ndiyo wanaleta makampuni ya nishati na kuiuzia TANESCO! Nikasema tumelogwa!
Niseme nini basi? Naweza kusema mengi. Lakini hapa nitasema machache tu. Tuna uamuzi wa kufanya. Kumnunua jogoo tuliyeibiwa au kumwambia mwizi wetu huyo jogoo ni wetu! Tunaweza kununua mitambo ya Dowans na suala hili likaisha. Lakini nawahakikishia mapema kabisa; tukinunua mitambo hiyo haina maana kesi yao kule Paris itafutwa! Tunaweza kununua na jamaa wakashinda kesi! Tukawalipa dola milioni 100 wanazotudai kule, na hizi milioni 60 za kununulia mitambo! Halafu tunawapigia magoti kina Brown ati tunaomba msaada tumelogwa sisi au tumejiloga wenyewe kwa wenyewe!
Vinginevyo tunaweza kuwakatalia. Tukawaambia Hapana Dowans. Zungumzeni na watengenezaji; tangazeni tenda mpya na wapeni jamaa miezi minane ya kuleta na kufunga mitambo mipya kwa bei nafuu ya hiyo; tuone makampuni mangapi yatajitokeza! Tusikae pembeni tuwaambie watawala wetu hivyo. Tuwaambie kina Rostam na wenzake inatosha kutuburuza.
Nakupa namba za simu, tuma sms au piga waambie: Tunahitaji Umeme, siyo wa Dowans, zungumzeni na watengenezaji. Namba ya Rais Kikwete 754 777 775, namba ya Dk. Idris Rashid 754 280 442, ya Rostam 754-555 555 na ya Mhe. William Ngeleja ni 754 710 070. Tuwaheshimu lakini tusiwaogope. Ni ndugu zetu hawa, ni Watanzania wenzetu hawa ninaamini kwa wingi wetu tukiwashawishi kwa hoja hatimaye watatusikiliza.
Kama Al-Adawi ataingia hasara msiwe na wasiwasi. Yeye mwenyewe aliniambia kuwa kwenye biashara kuna hasara na kuna faida. Kasema yuko tayari hata wakiamua kuitaifisha mitambo hiyo (itakuwa hasara kwake).
Lakini niwahakikishie sijui kama sikio la kufa linaweza kusikia dawa. Kwa kadiri mipango ilivyo, Dowans lazima alipwe tu! Aidha kwa kununua mitambo hiyo au kwa kushindwa kesi! Wako tayari kuliachilia moja; yote mawili kuna mtu akili zitamruka.
Lakini wakiamua kununua kama walivyodhamiria tangu miaka miwili iliyopita, mjue taifa zima sisi tumelogwa! Tukubali tu yaishe tuanze mijadala mingine hii ya ufisadi tutakuwa tumeipoteza rasmi.
WAKAKAA katika kikao chao wakakubaliana; Tuwaambie kuhusu majenereta.
Huku wakiwa wametulia mahali wanapojua wao na Mungu wao wakasemezana; tuhakikishe mjadala unahusu majenereta na siyo mmiliki. Wakahimizana wakijua ya kwamba dili lao limeshtukiwa na Watanzania.
Ndiyo. Wakagongesheana gilasi wakijua kabisa ya kuwa wakibadili mkakati majenereta yatanunuliwa tu.
Tusisitize kuwa ni mapya, mmoja wao ambaye ni kinara kati yao akawaambia. Ndiyo! Mwingine akakubali. Tuwaambie majenereta tayari yako Tanzania na ni mapya kuna ubaya gani kuyanunua, wakapanga hoja zao. Tuhakikishe hawazungumzii Dowans. Wasizungumzie umiliki, wasizungumzie tuliingiaje; wasizungumzie tulitokea wapi. Wakakumbushana.
Ndiyo, sasa tuwaambie mmiliki wake basi. Likatolewa wazo.
Si we bwana jina lako tayari linaonekana, kubali tu na tutawapiga maneno yatakwisha. Mjadala wa mmiliki tutaufunga na turudi kuzungumzia majenereta, akasema mmoja wao kisha wakacheka. Wakakubaliana, wakatawanyika kama walivyokutana.
Mmiliki wa Dowans hatimaye akajitokeza na kukubali. Mara ya kwanza nilipozungumza naye alikataa kuijua Dowans; alikataa kabisa kusema amewahi hata kusikia; alikataa akisema kuwa kampuni hiyo haipo Uarabuni. Ndiyo! Alikiri kuwa na urafiki na Rostam lakini alikataa kabisa kuwa Rostam hakuhusika na ujio wa Dowans. Kwa sauti thabiti ya Brigedia Jenerali Suleiman Al-Adawi alikataa kuitambua Dowans! Nikakubali. Sikuridhika.
Nikapata fomu za BRELA (Wakala wa Usajili wa Makampuni na Utoaji wa Leseni). Nikaziangalia. Nikakuta jina lake, anuani yake, na sahihi yake. Nikasema alinidanganya. Nikasema mheshimiwa huyu aliniuzia kanyaboya. Nikatambua kuwa kama hakusema ukweli, kama hakutaka watu wajue ukweli, kuna kitu alikuwa anaficha. Kitu ambacho hakutaka watu wajue; nikakumbuka.
Nilipozungumza naye Jumamosi ile tulizungumza vizuri mpaka aliponiniuliza kama mimi ni Mtanzania. Nikamwambia ndiyo. Akaniuliza; unaandika mambo ya systems ya Tanzania? Nikamjibu ndiyo mkuu. Akasema; Oh. Haikuwa Oh ya nakuelewa; ilikuwa ni Oh ya kukata tamaa, ya kukutwa ukifanya usichotakiwa. Ni hapo nikakumbuka alipoanza kukataa kujibu maswali yangu; ambayo naamini ni ya Watanzania wengi.
Dowans ni kampuni ya nani? Je, anajua Kampuni ya Dowans Holdings ya Uarabuni? Vipi ile Dowans ya Costa Rica; ziko Dowans ngapi? Imeandikishwa wapi na nani? Mbunge wa Igunga Mhe. Rostam Aziz anahusika vipi? Hakutaka kujibu. Akabakia kunipiga mkwara; Usiandike jina la mtu ambaye huna uhakika naye. Nitakutumia wanasheria wangu waje wazungumze nawe. Nikakumbuka amenidanganya.
Jumamosi iliyofuata nikarudi tena nikiwa na ushahidi mkononi. Nikitambua kuwa kati ya Jumamosi ile na Jumamosi hii walifanya kikao chao cha makubaliano. Kikao cha kuhakikisha kuwa lolote liwalo majenereta ya Dowans yatanunuliwa na Jenerali lazima alipwe hela yake kwani ahadi ni deni. Walimuahidi kuwa mwisho wa mkataba serikali itanunua majenereta; walimpa moyo kuwa hata wakisitisha msaada kabla afungue kesi Paris ambayo hatutajiandaa kushinda ili hata kama tukikataa kununua bado tumlipe! Ndiyo! Nikarudi tena kumuuliza.
Nilipompata mara ya pili alikuwa mnyenyekevu zaidi, lakini safari hii alikubali. Hakuzungusha maneno. Ndiyo mimi, ndiyo namiliki Dowans, alisema. Nikamuuliza mbona ulinifunga kamba bosi? Akasema; sikujua nani anazungumza na mimi. Nikacheka. Nilikumbuka nilijitambulisha kwake kuwa naandika kwenye gazeti moja la Tanzania na ninaandika kuhusu suala la ufisadi linalohusisha Kampuni ya Dowans.
Akajibu maswali yangu mengi; mengine alishindwa kujibu kwa sababu tayari nilikuwa na majibu.
Dowans haikuingia kwa bahati mbaya. Ilialikwa. Ilialikwa na wakubwa wa nchi hii na wenye nguvu. Sijui nia yao ilikuwa nini, lakini kutatuta tatizo la nishati haikuwa mojawapo. Ulikuwa ni uamuzi wa kibiashara. Uamuzi wa nikune nami nikukune. Wakawaalika baada ya Richmond kushindwa; hawakuwa na kampuni ya nishati kwani Al-Adawi mwenye utajiri mkubwa tu anahusika zaidi na mambo ya ujenzi kama rafikiye Rostam.
Vyanzo vyangu vya uhakika vikanidokeza kuwa ni Rostam aliyemfuata kumpa mwaliko huo ambao naye aliupata kama ombi kutoka juu. Akaambiwa walete wala jamaa zako najua wana uwezo wa kuweza kufanya hivyo. Jamaa akashawishiwa alipohakikishiwa kuwa baada ya mkataba serikali itanunua. Hakuna mnunuzi mwingine, asiwadanganye mtu. Serikali isiponunua jenerali amekula hasara.
Hivyo wanajitahidi. Fungeni mjadala wa Dowans, na tuiache TANESCO ifanye maamuzi yake, akasema waziri mhusika. Kwa maneno mengine, acheni kuhoji-hoji. Tumeambiwa tunyamaze; tumeambiwa tusizungumzie Dowans tena, tuiache serikali ifanye maamuzi.
Tutakuwa tumelogwa tukifanya hivyo; tutakuwa tumelaaniwa tukikubali serikali ifanye mambo sirini; tutakuwa tuna kaugonjwa fulani tukiwaacha watawale wapendavyo. Nikasema kwa nini mtu wa porini na mvi hizi nahangaika na mambo ya Dowans? Kwa nini kujihangaisha kupambana na Goliathi na ka kombeo kangu ka kalamu? Kwa nini namimi nisikubali tu yaishe? Nikasema nitakuwa msaliti wa ndugu zangu! Nitakuwa ni msaliti wa nchi yangu, nitakuwa msaliti wa dhamira yangu!
Lakini pia nikajiuliza; hivi kuna ubaya gani wakiyanunua hayo majenereta na kuleta umeme unaohitajika sana? Kuna ubaya gani kutokujali mmiliki au jinsi gani alivyoingia nchini? Kama jamaa anakuja na dawa naye ni jambazi si tuchukue tu (rafiki yangu mmoja alinipa mfano huo). Nikakumbuka msemo wa kiswahili baniani mbaya kiatu chake ni dawa. Nikasikiliza hoja za watetezi wa tununue mitambo hii kwani itatupa umeme sasa na tayari iko nchini. Nikakumbuka kikao chao.
Lakini nikakumbuka kisa cha utotoni. Nilipokuwa mtoto kulikuwa na jamaa mmoja mwizi. Jamaa huyo alipita usiku akaiba jogoo letu moja kubwa na lililonona. Tulipoamka asubuhi tukatafuta jogoo wetu. Hayupo. Majira ya mchana, kuna mtu akapita akiita nauza jogoo, nauza jogoo. Tulipofungua mlango tulimuona huyo njemba mwizi mwizi na jogoo lake mkononi. Tukakimbia! Aliyekuwa mkubwa nyumbani ikabidi anunue jogoo huyo! Alikuwa ni yule yule jogoo wetu! Jamaa alirudia mara mbili, mwisho ikabidi tuwaambie wazazi!
Ndiyo, tukinunua mitambo ya Dowans itatusaidia kuwa na jogoo wetu; lakini mbona tulishamnunua na kuwa naye bandani? Nikakumbuka. Watanzania hawajali jogoo katoka wapi hata kama alikuwa ni wa kwao alimradi wakiambiwa anatotolesha vizuri! Tuko tayari kumnunua kwa gharama yoyote ile!
Ndipo nikakumbuka walipobadili sheria iliyotengenezwa kuidhoofisha TANESCO. Yaani wale wale waliotunga sheria ya kuidhoofisha TANESCO leo wanasimama kutuambia ati wanaitetea TANESCO! Nimebakia kucheka tu. Kama kweli wanataka kuisadia TANESCO wabadilishe sheria na kuruhusu kampuni yoyote inayotaka kuzalisha nishati ifanye hivyo na isambaze nishati hiyo yenyewe. Wakitaka kutumia nyaya za TANESCO au miundombinu, TANESCO ndiyo iwachaji. Mtashangaa!
Leo wametengeneza sheria ambayo wao wenyewe wamejihakikishia ndiyo wanaleta makampuni ya nishati na kuiuzia TANESCO! Nikasema tumelogwa!
Niseme nini basi? Naweza kusema mengi. Lakini hapa nitasema machache tu. Tuna uamuzi wa kufanya. Kumnunua jogoo tuliyeibiwa au kumwambia mwizi wetu huyo jogoo ni wetu! Tunaweza kununua mitambo ya Dowans na suala hili likaisha. Lakini nawahakikishia mapema kabisa; tukinunua mitambo hiyo haina maana kesi yao kule Paris itafutwa! Tunaweza kununua na jamaa wakashinda kesi! Tukawalipa dola milioni 100 wanazotudai kule, na hizi milioni 60 za kununulia mitambo! Halafu tunawapigia magoti kina Brown ati tunaomba msaada tumelogwa sisi au tumejiloga wenyewe kwa wenyewe!
Vinginevyo tunaweza kuwakatalia. Tukawaambia Hapana Dowans. Zungumzeni na watengenezaji; tangazeni tenda mpya na wapeni jamaa miezi minane ya kuleta na kufunga mitambo mipya kwa bei nafuu ya hiyo; tuone makampuni mangapi yatajitokeza! Tusikae pembeni tuwaambie watawala wetu hivyo. Tuwaambie kina Rostam na wenzake inatosha kutuburuza.
Nakupa namba za simu, tuma sms au piga waambie: Tunahitaji Umeme, siyo wa Dowans, zungumzeni na watengenezaji. Namba ya Rais Kikwete 754 777 775, namba ya Dk. Idris Rashid 754 280 442, ya Rostam 754-555 555 na ya Mhe. William Ngeleja ni 754 710 070. Tuwaheshimu lakini tusiwaogope. Ni ndugu zetu hawa, ni Watanzania wenzetu hawa ninaamini kwa wingi wetu tukiwashawishi kwa hoja hatimaye watatusikiliza.
Kama Al-Adawi ataingia hasara msiwe na wasiwasi. Yeye mwenyewe aliniambia kuwa kwenye biashara kuna hasara na kuna faida. Kasema yuko tayari hata wakiamua kuitaifisha mitambo hiyo (itakuwa hasara kwake).
Lakini niwahakikishie sijui kama sikio la kufa linaweza kusikia dawa. Kwa kadiri mipango ilivyo, Dowans lazima alipwe tu! Aidha kwa kununua mitambo hiyo au kwa kushindwa kesi! Wako tayari kuliachilia moja; yote mawili kuna mtu akili zitamruka.
Lakini wakiamua kununua kama walivyodhamiria tangu miaka miwili iliyopita, mjue taifa zima sisi tumelogwa! Tukubali tu yaishe tuanze mijadala mingine hii ya ufisadi tutakuwa tumeipoteza rasmi.