Yo Yo
JF-Expert Member
- May 31, 2008
- 11,217
- 1,702
Vijeba utawajua tuNa miss Dominic Chilambo wa kanda ya ziwa. Alikuwa akikutajia line up ya wana TP Lindanda Kirumba unajiskia kama umeshafungwa vile. Halafu kuna Uncle J Nyaisanga, simwoni kwenye list. Kile kipindi chake cha muziki usiku (Disco Show?). Anakuambia leo nimekuandalia vibao ywa kukutoa soksi na na viatu kubakia pale pale. Pia kuna akina Mohamed Kadilu na Bakari Msulwa (mrindimo). Na huyu mama ya Tamwa hujamweka. Pia alikuwepo mwamama mmoja alikuwa anatangaza kipindi cha Kodi na Mapato. Sijui kama hiki kipindi bado kipo.