Tujikumbushe UMBWE

Martina Nkulu yupo dar anafanya kazi Voda ofisi zao zipo pale PPF tower,spyter ni mhasibu wa miradi ya jeshi dodoma kuna kipindi alikuwa anasoma CBE na dogo mmoja tulikuwa nae anaitwa sango kasera alikuwa matata kinoma campus ya dodoma,ommy namuona mara kwa mara kuna kipindi alikuwa anafanya kazi tume ya haki za binadamu,
 
mimi nilimaliza 1999 nakumbuka mambo mengi ila kati ya yote sita msahau braza karua alinipokea mwaka 1996 na kuwa kaka yangu.zaidi ya yote sitaisahau tarehe 28/1/1996 kwani siku hiyo ndio form two walifungua shule na kutukuta form one nakumbuka ilikuwa ni pata shika nguo kuchanika kwanza ilikuwa form one (njuka)huruhusiwi kulala bwenini nakumbuka siku hiyo mida ya saa nne usiku nilikutwa na braza mmja wa form two akaniomba shilingi 100 nikamuambia sina nilipigwa vibao viwili nikapewa kiatu kinacho nuka sana nikaambiwa nipige simu nyumbani niwaeleze wazazi wangu kuwa sina hela kile kiatu kilikuwa kinanuka sana kweli kwa form one ilikuwa ni mateso

nakumbuka wakati tukiwa njuka tulikuwa tunaambiwa tudeki madom bila kuwasha taa ili tusiwasumbue kaka zetu hio ilikuwa mwaka 1996
msele alikuja mwaka 1996 katikati akataka kubadili utaratibu uliozoeleka
form one(njuka) kudeki madom
form two kudeki vyoo
form three kufeka viwanja
form four sikumbumbuki walikuwa wanafanya nini
form wani tikasema tutadeki tumalizie mwaka akatukubalia tulipofika form two akataka akachange akasema wote tudeki na form two ndio mgomo ulipo tokea mnaukumbuka mgomo wa umbwe mwaaka 1997 ulianza ijumaa siku ya general clean wakina kinabo wakiwa vinara namkumbuka kichalechale john,ayubu marehemu shida
 
Pale Mti safi kuna HP mmoja kwa Jina akiitwa Kisare Makori. Huyu jamaa alifanikiwa kuchaguliwa kuwa HP baada ya kumkoromea Mwalimu Lobz alipomkuta akifua nyakati za prep ya adhuhuri. Lakini baada ya kuchaguliwa akageuka na kuwa mnoko kwa wanafunzi. Kwa staff wa Umbwe yule jamaa alikuwa na hadhi ya baada ya Savimbi. Kuona hivyo wapigakura wakaamua kumwonyesha kazi. Wadau wa Mti safi naamini mnazikumbuka chemba. HP kisare Makori alivyokuwa mtanashati, akitembea mkononi ameshikilia rundo la funguo (ingekuwa siku hizi tungesema ana gari) huku mkono huo ukizungushwa kwa mbali usiguse shati; jamaa alikuwa anajipenda bwana wala usipime. Siku ya siku makomandoo wa wapigakura wake wakaenda kuchota maji taka kwenye ndoo, afu wakaenda kwenye chemba yake; kama mnakumbuka vizuri wenye chemba zao walikuwa wakijisomea mumokwamumo. Basi wale makomando wakamwita kwa dirishani, naye Kisare Makori hakusita kujongea karibu na dirisha. Nao Makomandoo wakayatuma majitakwa kwa kuyamwaga kwenda kwenye chemba yake kupitia dirisha. HP Makore akakutana na kusema nayo nao Makomandoo wakaingia mitini. Hayo yalifanyika usiku

Kesho yake HP Kisare Makori akaenda kushtaki kwa Baba yake Savimbi, naye Savimbi hakusita kutufanyia kweli, na hivi ndivyo alivyotuambia, nanukuu ".....sasa nasema kweli kwa jina la Mungu, kwa vile nyinyi mmeamua kummwagia kinyesi HP Kisare, hakika na nyinyi mtalazimika kukigusa kinyesi hicho. kwa hiyo kila darasa litachagua mwakilishi ambaye atakwenda kukigusa (kudeki) kinyesi hicho kwenye chumba cha HP" mwisho wa kunukuu. Shughuli ilikuwa kwenye kuchagua nani wa kwenda kuwakilisha kugusa hicho kinyesi, sikumbuki kwenye Jimbo la Ei wani ni nani ambaye alidondokewa na kura hiyo.

Kitendo hiki hakikuwa cha kiungwana lakini kwa Mtu kama Kisare Makori ililazimu kufanya hivyo. Sijui siku hizi huyu jamaa yuko wapi, maana nakumbuka mwaka 1999 alitaka kugombea Urais wa DARUSU, tukalazimika kumchimba mkwara kwamba yatamtokea kama ya Mti safi. Huyu jamaa alikuwa hafai kabisa kwani mwishoni mwa mwaka 1991 wakati tukiwa kwenye mgomo pale Umbwe, yeye alighairi kuendelea na mgomo na kwenda kumweleza Savimbi mikakati yetu ya kuandamana hadi kwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimakyaro (wakati ule alikuwa Samwel Sitta) kwenye kuhoji kwanini alikuwa amekaa na fedha zetu (kama walivyosema walimu) wakati akijua kuwa tulikuwa karibu kufunga shule na tulizihitaji fedha hizo. Baada ya jamaa kutangaza kujitoa kwenye mgomo na kwenda kumweleza Savimbi juu ya mpango wetu wa kuandamana, kesho yake tukaanza kulipwa fedha. Na baada ya hapo tukafukuzwa shule; nakumbuka tukio hili lilienda sambamba na lile la Matusi ya nguoni aliyoyapata Mheshimiwa Rais Ally Hasan Mwinyi toka kwa wanafunzi wa UDSM; kwani yalitangazwa kwa pamoja kwenye taarifa ya habari.
 
Wana wa Mti safi hapa nawaletea squard nzima ya kidato kilichojulikana kwa jina la Jimbo la Ei Wani (A One) mwaka 2001. Ninataarifa za kufariki kwa jamaa mmoja aliyekuwa akiitwa Michael Ambali. Huyu jamaa alifia kule Bondeni alikokwenda kusaka vijisenti. Mungu amlaze mahali pema.

Nakumbuka tulipoingia Umbwe Five 2001, kulikuwa na mabadiliko tuliyoanza nayo. Mkondo wa ECA (ukijulikana almaarufu kama Mafuta) uliongezwa toka mmoja na kuwa miwili kukawa na Five A One (Ilikuwa ya Wagumu mwaka 2001) na Five A Two (ilikuwa ya Macheckbob). HGL au wenyewe tukiiita Mfupa, mkondo ukabakizwa mmoja. Nakumbuka liliandaliwa disco la welcome Form Five kwaajili yetu, lakini kutokana na kiingilio kuwa juu, wana jimbo la Ei Wani tukazira. Wengi tulitokea shule za DSM na Pwani ambapo kiingilio cha disko hakikuwa kikubwa kama tulivyokikuta Umbwe. Basi wenyeji wetu wakaendelea na disko la kutukaribisha wageni fomu Vii ambao tulibakia nje. Kwa vile darasa letu lilikuwa pua na mdomo na Bwalo ambako ndiko disko lilikuwa likirukwa, tukawa hatuwezi tena kupiga ucheche. Badala yake tukaamua kuchezesha disko letu. Kuna Mtaalam mmoja aitwaye Ninga akawa anaporomosha mziki kwa kupiga dawati huku akifloo ule wimbo nimeusahau kidogo, afu mkali wa kuruka majaoka aitwa Goda Sanga (huyu Bishoo flani lakini Mgumu ambaye alikuwa Ei Two) akawa anayaruka mangoma hayo kwa ustadi wa hali ya juu; wanajimbo wengine tukawa tunayanyuka makofi na kumwaga hemwahemwa kwa midomo yetu. Unajuwa kilichotokea, vijana wa Olevel wakajazana kwenye madirisha kushuhudia umahiri wa Goda Sanga katika kuyaruka mangoma. Ndani ya ukumbi wa disko lenyewe kukawa hakunogi na vijana waliolipa kuingia baadhi yao wakawa hawaoni ladha ya kuingia ndani ya Bwalo. Kamati ya staree kuona hivyo wakaamu kuja kututaka tusitishe disko letu. Sisi hatukuafikiana nao na kuwaeleza kuwa tulikuwa na haki ya kufanya hilo kwavile tulikuwa ndani ya darasa letu. Mvuto ukaendelea kuwa mkubwa kwenye disko letu, kwani vijana toka Tambaza (Goda na Ninga) walikuwa wanafanya mambo ambayo kwa vijana wa Olevel walikuwa hawajawahi kuyaona. Jamaa wa Kamati ya starehe wakaamua kuukata mzizi wa Fitina kwa kumwingiza Goda Sanga bure kwenye Disko la Bwaloni na hivyo kuliua disko la Jimbo la Ei Wani
 
Hiki ndicho kikosi cha Jimbo la Ei Wani (A One) 2001-2003 waanzilishi wa Mikondo miwili ya ECA. Pamoja na kuongeza mkondo lakini bado tulikuwa wachache sana enzi hizo tuliokuwa tukisoma ECA Mafuta.

Nakumbuka tulipiga ucheche wa nguvu kiasi kwamba tulianza kukokotoa yumkini (probability) ya kutopata wani na kuona kwamba ilikuwa hakuna. Hivi ndivyo tulivyokuwa tukikokotoa. Kwa vile tulikuwa hatuna mwalimu wa Uchumi kwa muda mrefu tukawa tunaasume kwamba tutapata mswaki wa Uchumi ambayo ni pointi 5; ukija kwenye uhasibu na biashara hakukuwa na dalili za mtu kupata pointi zaidi ya nne yaani A moja na C moja. Ukizingatia kwamba wakati ule bado kanuni ya matokeo ya umbwe ilikuwa inahold; niwakumbushe kanuni yenyewe ilikuwa inasema hivi: Ukichaguliwa tu kujiunga na Umbwe Sekondari tayari una Divisheni IV; ukisafiri na kufika getini Umbwe una Divisheni III; ukiingia darasani una Divisheni II; ukiandika notice una Divisheni I; namna gani utachechelaiz ndiyo ditaminant fakta ya kupata wani ya pointi ngapi. Kanuni hii ilichafuliwa na jamaa mmoja ambaye alimaliza 2004 na kuzungusha. Huyu jamaa aliyekuwa na china la chombo kimojawapo cha kutilia chakula alikuwa mwanasoka mzuri kweli. Laiti angekulia nyakati hizi za udhamini wa NMB na Senge angeshakuwa juu sana.

Nakumbuka tulitembelea UDSM FCM tukawa tunaulizia vigezo vya kuingia Mlimani, manake tulikuwa tukihofia BAM na siasa (BAM alianza kutufundisha Savimbi lakini baada ya mgomo wa Novemba 2001, tulivyorudishwa shule akasusa kutufundisha, badala yake tukawa tunafundishwa na Protas Mwalimu wa Olevel. Bw. Protas naye siku moja akatuletea zake tukamkoromea naye akazira, ikabidi tuanze kufundishana wenyewe. Siku moja Mw. Protas akawa anapita nje ya darasa la V ATwo, akaona kwa dirishani intergration inashushwa na jamaa mmoja aliyejulikana kama Martin Chanila-Vijana waliokuwa wamesoma additional Math-. Hapo ndipo alipogundua kuwa hakuwa ametukomoa, na hivyo kuona soo na kuamua kurejea mwenyewe kutufundisha). Yule Lecturer wa UDSM ambaye tulikuwa tunamwuliza mahitaji ya kufaulu ili kuingia UDSM, yeye akatwambia msihangaike kuulizia habari hizo nendeni mkasome kwa bidii kwanza. Tukamwambia hivi pale tulivyokuwa kila mtu alikuwa na uhakika wa kupata wani ila pointi tu ndo tulikuwa hatuzijui. Kwahiyo ndo akatuambia kwamba iwapo utapata mswaki wa BAM au Siasa lakini kwenye kombi umefanya vema, wataangalia Form IV kama ulipata C na kwenda juu basi watakuchukuwa. Ungejuwa tulivyofurahia maelezo hayo huwezi pima, maana tulikuwa ha uhakika kwamba hata kama Vibaraka wa Savimbi wakiamua kutofundisha BAM au Siasa hakuna noma kwani kila mwanafunzi alikuwa na akiba ya form IV
 
Hiki ndicho kikosi cha Jimbo la Ei Wani (A One) 2001-2003 waanzilishi wa Mikondo miwili ya ECA. Pamoja na kuongeza mkondo lakini bado tulikuwa wachache sana enzi hizo tuliokuwa tukisoma ECA Mafuta.

Nakumbuka tulipiga ucheche wa nguvu kiasi kwamba tulianza kukokotoa yumkini (probability) ya kutopata wani na kuona kwamba ilikuwa hakuna. Hivi ndivyo tulivyokuwa tukikokotoa. Kwa vile tulikuwa hatuna mwalimu wa Uchumi kwa muda mrefu tukawa tunaasume kwamba tutapata mswaki wa Uchumi ambayo ni pointi 5; ukija kwenye uhasibu na biashara hakukuwa na dalili za mtu kupata pointi zaidi ya nne yaani A moja na C moja. Ukizingatia kwamba wakati ule bado kanuni ya matokeo ya umbwe ilikuwa inahold; niwakumbushe kanuni yenyewe ilikuwa inasema hivi: Ukichaguliwa tu kujiunga na Umbwe Sekondari tayari una Divisheni IV; ukisafiri na kufika getini Umbwe una Divisheni III; ukiingia darasani una Divisheni II; ukiandika notice una Divisheni I; namna gani utachechelaiz ndiyo ditaminant fakta ya kupata wani ya pointi ngapi. Kanuni hii ilichafuliwa na jamaa mmoja ambaye alimaliza 2004 na kuzungusha. Huyu jamaa aliyekuwa na china la chombo kimojawapo cha kutilia chakula alikuwa mwanasoka mzuri kweli. Laiti angekulia nyakati hizi za udhamini wa NMB na Senge angeshakuwa juu sana.

Nakumbuka tulitembelea UDSM FCM tukawa tunaulizia vigezo vya kuingia Mlimani, manake tulikuwa tukihofia BAM na siasa (BAM alianza kutufundisha Savimbi lakini baada ya mgomo wa Novemba 2001, tulivyorudishwa shule akasusa kutufundisha, badala yake tukawa tunafundishwa na Protas Mwalimu wa Olevel. Bw. Protas naye siku moja akatuletea zake tukamkoromea naye akazira, ikabidi tuanze kufundishana wenyewe. Siku moja Mw. Protas akawa anapita nje ya darasa la V ATwo, akaona kwa dirishani intergration inashushwa na jamaa mmoja aliyejulikana kama Martin Chanila-Vijana waliokuwa wamesoma additional Math-. Hapo ndipo alipogundua kuwa hakuwa ametukomoa, na hivyo kuona soo na kuamua kurejea mwenyewe kutufundisha). Yule Lecturer wa UDSM ambaye tulikuwa tunamwuliza mahitaji ya kufaulu ili kuingia UDSM, yeye akatwambia msihangaike kuulizia habari hizo nendeni mkasome kwa bidii kwanza. Tukamwambia hivi pale tulivyokuwa kila mtu alikuwa na uhakika wa kupata wani ila pointi tu ndo tulikuwa hatuzijui. Kwahiyo ndo akatuambia kwamba iwapo utapata mswaki wa BAM au Siasa lakini kwenye kombi umefanya vema, wataangalia Form IV kama ulipata C na kwenda juu basi watakuchukuwa. Ungejuwa tulivyofurahia maelezo hayo huwezi pima, maana tulikuwa ha uhakika kwamba hata kama Vibaraka wa Savimbi wakiamua kutofundisha BAM au Siasa hakuna noma kwani kila mwanafunzi alikuwa na akiba ya form IV

Kichankuli naona unapotosha ukweli katika post yako. Mikondo miwili ya ECA pale MTI SAFI haikuanza 2001 kama unavyosema. Sie tumemaliza hapo kabla wewe hujaanza na ilikuwa miwili. In fact sidhani kama iliwahi kuwa mkondo mmoja tangu a-LEVEL ya ECA ilipoanzishwa Umbwe, kwenye mid 1980's. Halafu ni vema pia tukarekebishana kimahesabu kuwa Mswaki 'F' ya form 6 ni point 7, na sio point 5, so ili upate Div ONE kama una F ya Economics huna choice zaidi ya kupata A in both Commerce and Accountancy.
 
Kichankuli naona unapotosha ukweli katika post yako. Mikondo miwili ya ECA pale MTI SAFI haikuanza 2001 kama unavyosema. Sie tumemaliza hapo kabla wewe hujaanza na ilikuwa miwili. In fact sidhani kama iliwahi kuwa mkondo mmoja tangu a-LEVEL ya ECA ilipoanzishwa Umbwe, kwenye mid 1980's. Halafu ni vema pia tukarekebishana kimahesabu kuwa Mswaki 'F' ya form 6 ni point 7, na sio point 5, so ili upate Div ONE kama una F ya Economics huna choice zaidi ya kupata A in both Commerce and Accountancy.

Salaam mkulu Shonge,ni kweli huyu bwana ni mpotoshaji hasa,nadhani hata hajui anaongea nini na maana mimi mwenyewe nimesoma mti safi kabla yake na ECA tulikuwa na ECA 1 na 2.Labda aseme kuwa HGL ndo waliongezewa darasa maana kipindi naondoka kulikuwa kuna mpango wa kuongeza mkondo kwa HGL(sina uhakika kama uliongezwa ama la),huyu bwana ni mwongo,kimsingi anawapotosha wana jamii humu JF....Mbarikiwe sana
 
Kesho yake HP Kisare Makori akaenda kushtaki kwa Baba yake Savimbi, naye Savimbi hakusita kutufanyia kweli, na hivi ndivyo alivyotuambia, nanukuu ".....sasa nasema kweli kwa jina la Mungu, kwa vile nyinyi mmeamua kummwagia kinyesi HP Kisare, hakika na nyinyi mtalazimika kukigusa kinyesi hicho. kwa hiyo kila darasa litachagua mwakilishi ambaye atakwenda kukigusa (kudeki) kinyesi hicho kwenye chumba cha HP" mwisho wa kunukuu. Shughuli ilikuwa kwenye kuchagua nani wa kwenda kuwakilisha kugusa hicho kinyesi, sikumbuki kwenye Jimbo la Ei wani ni nani ambaye alidondokewa na kura hiyo.

Kitendo hiki hakikuwa cha kiungwana lakini kwa Mtu kama Kisare Makori ililazimu kufanya hivyo. Sijui siku hizi huyu jamaa yuko wapi, maana nakumbuka mwaka 1999 alitaka kugombea Urais wa DARUSO, tukalazimika kumchimba mkwara kwamba yatamtokea kama ya Mti safi. Huyu jamaa alikuwa hafai kabisa kwani mwishoni mwa mwaka 1991 wakati tukiwa kwenye mgomo pale Umbwe, yeye alighairi kuendelea na mgomo na kwenda kumweleza Savimbi mikakati yetu ya kuandamana hadi kwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimakyaro (wakati ule alikuwa Samwel Sitta) kwenye kuhoji kwanini alikuwa amekaa na fedha zetu (kama walivyosema walimu) wakati akijua kuwa tulikuwa karibu kufunga shule na tulizihitaji fedha hizo. Baada ya jamaa kutangaza kujitoa kwenye mgomo na kwenda kumweleza Savimbi juu ya mpango wetu wa kuandamana, kesho yake tukaanza kulipwa fedha. Na baada ya hapo tukafukuzwa shule; nakumbuka tukio hili lilienda sambamba na lile la Matusi ya nguoni aliyoyapata Mheshimiwa Rais Ally Hasan Mwinyi toka kwa wanafunzi wa UDSM; kwani yalitangazwa kwa pamoja kwenye taarifa ya habari.

Mkuu naona unachanganya mambo kwa kiasi fulani....
  1. Mwaka 1999 Kisare hakuwepo UDSM, hivyo hawezi kuwa alitaka kugombea urais wa Daruso.
  2. Mwishoni wa mwaka 1991 (wakati wa mgomo wa kudai kurudishiwa fedha za nauli wakati wa likizo), head prefect alikua sio Kisare Makori.
  3. Hiyo nukuu yako toka kwa Shayo (Savimbi) inatia mashaka sana....siikumbuki. Unakumbuka baada ya tukio lile, pia alitishiwa kuchomwa kwa petroli? Hadi ikabidi aje mkuu wa wilaya?
  4. Kisare kwa sasa ni mwajiriwa wa Ikulu (nilishawahi kumwona akiongea kama kaimu mkurugenzi wa mawasiliano wa Ikulu - ile nafasi ya Salva).
  5. Mbona unaongelea matukio ya 2001 na 1991 kwa wakati mmoja, sidhani kama unaweza kuwa ulisoma mti safi miaka yote hiyo.
 
Mkuu naona unachanganya mambo kwa kiasi fulani....
  1. Mwaka 1999 Kisare hakuwepo UDSM, hivyo hawezi kuwa alitaka kugombea urais wa Daruso.
  2. Mwishoni wa mwaka 1991 (wakati wa mgomo wa kudai kurudishiwa fedha za nauli wakati wa likizo), head prefect alikua sio Kisare Makori.
  3. Hiyo nukuu yako toka kwa Shayo (Savimbi) inatia mashaka sana....siikumbuki. Unakumbuka baada ya tukio lile, pia alitishiwa kuchomwa kwa petroli? Hadi ikabidi aje mkuu wa wilaya?
  4. Kisare kwa sasa ni mwajiriwa wa Ikulu (nilishawahi kumwona akiongea kama kaimu mkurugenzi wa mawasiliano wa Ikulu - ile nafasi ya Salva).
  5. Mbona unaongelea matukio ya 2001 na 1991 kwa wakati mmoja, sidhani kama unaweza kuwa ulisoma mti safi miaka yote hiyo.

Mdau ni kweli kuna kosa la kiuandishi kwenye mwaka wa Kisare kutaka kugombea Urais wa DARUSO ilikuwa 1996 na siyo 1999. Kuhusu mgomo wa kudai nauli niko sahihi kwa maana ya 1991 kama ulikuwepo nyakati hizo mwalimu wa commerce A leve alikuwa Ludwick toka ujerumani. Wakati wa mgomo huo tayari Kisare alishaachia uHP na kuchukuliwa na Jamaa mmoja aliyetokea Mawenzi na ndiye aliyeongoza mapambano hayo hadi yakafanikiwa japokuwa yeye yalimgharimu kwa kufukuzwa shule moja kwa moja. Kama unakumbuka vizuri kuna yule jamaa ambaye alikuwa Brazameni na mtu wa kinywaji sana na ambaye walikuwa darasa moja na kisare. Naye ilikuwa amefukuzwa shule moja kwa moja, lakini akafaiti (yaonyesha alikuwa na magodfaza wa nguvu kwenye sistimu) na kurejeshwa. Siku hiyo amerudi shuleni tulikuwa Bwaloni tukamshangilia sana.

Lakini kitu kingine ninachokumbuka ni kwamba alikuja Samwel Sita baada ya Mgomo na katika kutuunga mkono madai yetu, alirejea njisi alivyotoa shilingi bungeni kwa kutoridhishwa na sababu zilizotolewa kkwaajili ya chanzo cha moto wa BOT. Na pia alitangaza kufutwa somo la siasa
 
Kichankuli naona unapotosha ukweli katika post yako. Mikondo miwili ya ECA pale MTI SAFI haikuanza 2001 kama unavyosema. Sie tumemaliza hapo kabla wewe hujaanza na ilikuwa miwili. In fact sidhani kama iliwahi kuwa mkondo mmoja tangu a-LEVEL ya ECA ilipoanzishwa Umbwe, kwenye mid 1980's. Halafu ni vema pia tukarekebishana kimahesabu kuwa Mswaki 'F' ya form 6 ni point 7, na sio point 5, so ili upate Div ONE kama una F ya Economics huna choice zaidi ya kupata A in both Commerce and Accountancy.

Shonge nianze kwa kukiri kosa la kiuandishi la mwaka nilimaanisha 1991 badala ya 2001; vivyo hivyo 2001-2003 siyo sahihi bali sahihi ni 1991-1993. Kuna uwezekano basi awali ilikuwa mikondo miwili ya ECA halafu mmoja ukajapunguzwa kwasababu ECA iliyomaliza 1991 na 1992 ilikuwa na mkondo mmoja tu
 
Shonge nianze kwa kukiri kosa la kiuandishi la mwaka nilimaanisha 1991 badala ya 2001; vivyo hivyo 2001-2003 siyo sahihi bali sahihi ni 1991-1993. Kuna uwezekano basi awali ilikuwa mikondo miwili ya ECA halafu mmoja ukajapunguzwa kwasababu ECA iliyomaliza 1991 na 1992 ilikuwa na mkondo mmoja tu

Umesomeka mkulu...be blessed
 
Kwa kweli kumbukumbu ya Umbwe imenifurahisha. Nakumbuka sana sikumoja tulikua tunapiga SEREKA ya fuka nukanusurika kidogo kutumbukizwe uso kwenye dishi la FUKA. Jamani nani anajua aliko TYSONI a.k.a Osmond Shuma?
 
Kuna anaekumbuka ile incidence ya COCA COLA kugeuka DOUBLE COLA? HIVI YULE MWALIMU MOSHA YUKO WAPI SIKU HIZI? KUNA MWENYE TAARIFA YEYOTE?
 
Samahani kuchelewa kujibu mkuu, nimemaliza mwaka 1997, nahisi ulikuwa hujaingia bado, -so mimi mzee kidogo.

Huyu jamaa ALEX MSELLE ALITOKEA Old Moshi, alitukuta pale.

Alikuwa mnoko kishenzi, ila nasikia akirudi home mke wake anamtuliza, ''yaani mama anatawala nyumba''

Aisee jamaa sura yake tu akikuangalia adhabu tosha!

May be mpaka leo bado yeye, una taarifa zozote?
Msele aliondoka nadhani around 2003. He was a nice headmaster
 
mimi nilimaliza 1999 nakumbuka mambo mengi ila kati ya yote sita msahau braza karua alinipokea mwaka 1996 na kuwa kaka yangu.zaidi ya yote sitaisahau tarehe 28/1/1996 kwani siku hiyo ndio form two walifungua shule na kutukuta form one nakumbuka ilikuwa ni pata shika nguo kuchanika kwanza ilikuwa form one (njuka)huruhusiwi kulala bwenini nakumbuka siku hiyo mida ya saa nne usiku nilikutwa na braza mmja wa form two akaniomba shilingi 100 nikamuambia sina nilipigwa vibao viwili nikapewa kiatu kinacho nuka sana nikaambiwa nipige simu nyumbani niwaeleze wazazi wangu kuwa sina hela kile kiatu kilikuwa kinanuka sana kweli kwa form one ilikuwa ni mateso

nakumbuka wakati tukiwa njuka tulikuwa tunaambiwa tudeki madom bila kuwasha taa ili tusiwasumbue kaka zetu hio ilikuwa mwaka 1996
msele alikuja mwaka 1996 katikati akataka kubadili utaratibu uliozoeleka
form one(njuka) kudeki madom
form two kudeki vyoo
form three kufeka viwanja
form four sikumbumbuki walikuwa wanafanya nini
form wani tikasema tutadeki tumalizie mwaka akatukubalia tulipofika form two akataka akachange akasema wote tudeki na form two ndio mgomo ulipo tokea mnaukumbuka mgomo wa umbwe mwaaka 1997 ulianza ijumaa siku ya general clean wakina kinabo wakiwa vinara namkumbuka kichalechale john,ayubu marehemu shida
Huo mgomo ulikuwa 1998 na sio 1997. Ni katika maswala ya kuweka rekodi sawa tu.
 
mhh ni kweli ilikuwa 98 sory vipi na wee ulikuwepo enzi zile unakumbuka kitanda cha HP kilimwagiwa mali kutoka maputo
 
namkumbuka jamaa mmoja tulikuwa naye dorm 9 alikunywa banana wine akavimba mwili mzima kumbe alikuwa na aleji...
 
Back
Top Bottom