Tujikumbushe tungo za Dr. Remmy Ongala- Open post

Kizimkazimkuu

JF-Expert Member
Nov 8, 2007
337
234
Mi nazikumbuka hizi

Mariam

Nakonda kama mnazi kwa mapenzi niliyonayo,
Jina lako nakuota mchana kutwa sili ee
Moyo wanichechemea, mwili damu kauka eee

...na hiki kipande, katika Mola nalilia mtoto

Nakulilia mola wangu eee
Nakuwaza mola wangu eee eh
Yaliyonikuta ni makubwa naona haya
Mbona nateseka,

Wenzangu wana watoto mimi sina hata wa dawa eee
Yailah mtoto si nguo ningenunua
Mtoto ni mtoto kwa mama hakui iiih
hata angelikua ni kilema au mbaya kama remmy, n mtoto tu uuuh

Karibuni mnaozikumbuka tungo za nguli huyu aliyetutoka 2010.....
 
MUZIKI ASILI YAKE WAPI

Muziki asili yake wapi eeee
Muziki ni wa nani eee

Muziki hauna mwenyewe,
Muziki ni wito,
Muziki ni fundisho,
Muziki ni maombolezo, kilioooooo
Usinione nikiimba ukadhani ninayo furaha
Kumbe ninayo huzuni moyoniiiiiiii

WIMBO NISEME NINI
Niseme nini?
Niseme nini?

Sina la kusemaaaaa

......
....
Wengi hutishika na sura yangu mbaya lakini roho yangu ni nyeupe,
Nitahakikisha sifanyi mabaya hapa ulimwenguni,
ili siku ya mwisho nionane na Muumba

SIKU YA KIFO

Wandugu wapenzi,
Hii nyimbo ni nyimbo ya ukumbusho,
wa siku ya kuzaliwa na siku ya kufa,
Ulikuja kwa udongo utarudi kwa udongo,

Mawazo mawazo ya mtu mziiiiiima,
Kama akikwambia neno usibishe,
Neno ya muzee, ukabisha,
mwisho utapata shida.....

NAPENDA pia KAROLA, MREMA, NARUDI NYUMBANI, SAUTI YA MNYONGE, HARUSI YA MWANZA
 
Mi nazikumbuka hizi

Mariam

Nakonda kama mnazi kwa mapenzi niliyonayo,
Jina lako nakuota mchana kutwa sili ee
Moyo wanichechemea, mwili damu kauka eee

...na hiki kipande, katika Mola nalilia mtoto

Nakulilia mola wangu eee
Nakuwaza mola wangu eee eh
Yaliyonikuta ni makubwa naona haya
Mbona nateseka,

Karibuni mnaozikumbuka tungo za nguli huyu aliyetutoka 2010.....




 
Last edited by a moderator:
MUZIKI ASILI YAKE WAPI


WIMBO NISEME NINI

SIKU YA KIFO

NAPENDA pia KAROLA, MREMA, NARUDI NYUMBANI, SAUTI YA MNYONGE, HARUSI YA MWANZA

SIKU YA KUFA by DR. REMMY



MUZIKI ASILI YAKE WAPI



KIFO HAKINA HURUMA

 
Last edited by a moderator:
Binafsi naukumbuka wimbo wa MABMO KWA SOKSI. Wakti wimbo huu unaimba mie nlikuwa primary. Nakumbuka jinsi wimbo huu ulivyopigwa marufuku na serikali kisa eti ulikiuka maadili ya mtanzania. Kiukweli remmy alikuwa akiwaasa watanzania waache kufanya ngono bila kondom.
Kila nikisika matangazo yanayohusu kondom mie naukumbuka huu wimbo, nafikiria jinsi serikari yetu isivyoweza kufanya mambo yake hadi itakiwe na wahisani. remmy alikuwa ni mtanzania wa kwanza kushtukia ishu ya ukimwi na hivyo kuwaasa vijana wavae kondom, mwenyee remmy aliziita soksi. Na kweli vijana tulihasika, tulikuwa na kauli mbiu ya MAMBO KWA SOKSI. Kama remmy angeungwa mkono na serikali basi vijana wengi wasingeteketea na ukimwi. Tunakumbuka shuka wakati kumeshakucha!!!!
Hebu usikilize wimbo wenyewe.




 
Last edited by a moderator:
[I want To Go Home - Matimila(Dr. Remmy Ongala)]

[Remmy]
Narudi nyumbani yooo
Narudi nyumbani
Eeeee nyumbani.....
Nilipoamua nirudi nyumbani
Nyumbani ni nyumbani hata kukiwa kubaya au kuzuri
Nyumbani kwako ni nyumbani eee...nyumbani

Narudi Songea ooo
Narudi Matimila
Narudi Narimo
Ooooooo narudi nyumbani
Narudi Pilamio ooooo eee
Narudi Ungonini
Wangani wote mjiunge walongo vangu(Kikabila sikipati vizuri hapa)

Eeee nyumbani.....

[Wote]
I want to go home
I need to go back ho
I need to go back home
The place that is our home
Good or bad still home
(repeat x 3)

[Remmy tena]
Narudi nyumbani yooo
Narudi nyumbani
Eeeee narudi Majimaji
Narudi Afrika eee( x 2)
Narudi Nigeria
Eee narudi Ghana
Yooho narudi Kenya eee
Yoo narudi Uganda
Eeee narudi Gabon
Yooho narudi Congo
Eeee narudi Zaire eee
Yooho narudi Burundi
Narudi Rwanda
Narudi Majimaji
Nakwenda kula likono na la nyungu
Eee narudi Zambia
Narudi Zimbabwe
Narudi Botswana
Narudi Afrika ya Kusini
Mandela narudi nyumbani eee
Mwinyi weee narudi Tanzania
Eee narudi Tz ooo
Maricela ooo narudi nyumbani
Maricela ooo narudi nyumbani ooo
Murema narudi nyumbani
Baba Murema narudi nyumbani
Kawawa narudi nyumbani.........Salamwela eee
Kamwenye ee narudi nyumbani
Nyerere narudi nyumbani oooo x2
(kinaendele kiloingala hapa sikipati)

[Wote]
I want to go home
I need to go back home
I need to go back home
The place that is our home
Good or bad still home
(repeat x 3) .........
 
[NALILIA MTOTO - Matimila]

Nakulilia Mola wangu weee,
Nakuwaza Mola wangu wee,
Yalonipata makubwa naona balaa,
Wala hamu sina x2

Wenzangu wana watoto,
Mimi sina hata wa dawa eeeh,
Niwatumapo wana wa wenzangu,
Mama zao hunisimanga x2

Nalia nasikitika bahati sina,
Kwa waganga wa kila namna nimefika ni bure tuuuu,
Hospitali za kila namna nimekenda ni bure tuuuu,
Mola nimemuomba na sadaka nimetoa ni bure tuuuu,

Mola, Mola, Molaaa eeeh,
Mola eeeh nataka mtoto,

Mola Mola, Molaa eeh,
Mola eeh, nalilia mtoto

Mtoto angelikuwa ni nguo ningenunua,
Mtoto ni mtoto kwa mama hakui,
Hata angelikuwa kilema au mbaya kama Remmy ni mtoto tu!

Mola Mola, Mola eeeh....
 
[Mariamu - Matimila]
(Remmy)
ataka yote akosa yote
apita ahangaika asijue la kufanya ... asijue la kufanya
mshika mawili yote yamponyoka
apita akebakeba asijiue la kujitetea
mmmhhh mapenzi yawaka moto
naitika nilikukosea sasa nihurumie
si ninafikiri zaidi kuliko wewe
nakonda kama mnazi kwa mapenzi nilionayo
nilalapo nakuota mchana kutwa sili
moyo wanichechemea mwili damu hukauka
penzii eh ..... mmmh penzi eh x 2

nasumbuka kwako unionavyo moyo wangu
wewe ndio dawa yangu
Maraimu wangu
Tanga mbali
waja leo wondoka leoo
waja leo warudi leo

Mariamu bibi
mwenzenu sina pumuzi kujizuwia siwezi ohhh
mwanaume barabara kazi ya mume kwa mke
neno ya mke chumvi kwa mumewe
neno ya muke kachumbari kwa mumewe
penzi oh penzi likamung'uma he heh heh

likamung'uma hen heh heh .... mmhhhh
mdundiko, mdundiko ........ waaaaaa
mdundiko ...... waaaa
 
[MWANAIDI - Matimila]

(Kibao MWANAIDI kilipigwa na wana Matimila enzi hizo.
Sauti ni za Skassy Kasambula, Kyanga Songa, Fan fan na solo
ni la Batii Osenga bila kumsahau Mbwana Cox katika rythim)

nimetokea kumpenda binti Mwanaidi
nimeridhishwa na tabia yake
nikaamua tufunge nae pingu za maisha
urithi ulioacha baba niliutumia
ili kuneemesha ukoo wake
nilianza kuuza mifugo
hatimaye shamba
ili kumtosholeza mahitaji yake ehhh

baada ya miezi michache nikapata barua kutoka kwa Mwanaidi
..... .. kuwa yeye hanitaki tena
tena hawezi kuolewa na mimi

(wote)
mimi najuta eh najuta mama
gharama nilizogharamia
ameona bure
sijui la kufanya .. nasikitika oh
sababu yako ....... Mwanaidi x 3
 
[Mwanza - Matimila]

Mwanza oooh Mwanza eeeh,
Mwanza mji mzuri eeh,
Mwanza nitarudi Mwanza,
Mwanza nitakuja tena! x2

Mji wa Mwanza umezungukwa na milima ya mawe,
Milima ya alimasi,
Milima ya dhahabu,


Mji wa Mwanza umezungukwa na Lake Victoria,
Lenye maji bariiiidi,
Na samaki watamu wazuri,
Mwanza ooh,

Nalia Mwanza,
Wakazi wa Mwanza ni Wasukuma ooh,
Kabila Wasukuma,
Sukuma waaa!
Sukuma waaa!


Kutoka Mwanza tulielekea Bukoba,
Bukoba tulipokewa vizuri eeh,
Matoke kwa wingi,

Wakazi wa Bukoba wanasema Kihaya,
Mwabonaki waitu,
Mmmmh waitu eeeh


Mwanza oooh Mwanza eeeh

 
[NALILIA MTOTO - Matimila]


Nakulilia Mola wangu weee,
Nakuwaza Mola wangu wee,
Yalonipata makubwa naona balaa,
Wala hamu sina x2

Wenzangu wana watoto,
Mimi sina hata wa dawa eeeh,
Niwatumapo wana wa wenzangu,
Mama zao hunisimanga x2

Nalia nasikitika bahati sina,
Kwa waganga wa kila namna nimefika ni bure tuuuu,
Hospitali za kila namna nimekenda ni bure tuuuu,
Mola nimemuomba na sadaka nimetoa ni bure tuuuu,

Mola, Mola, Molaaa eeeh,
Mola eeeh nataka mtoto,

Mola Mola, Molaa eeh,
Mola eeh, nalilia mtoto

Mtoto angelikuwa ni nguo ningenunua,
Mtoto ni mtoto kwa mama hakui,
Hata angelikuwa kilema au mbaya kama Remmy ni mtoto tu!


Mola Mola, Mola eeeh....

KAKURUVI thanks a lot ....U have made my day. Hizi nyimbo za huyu jamaa zilikuwa na maneno na ujumbe mtamu uliowasilishwa kwa lugha nyepesi sana na ya kila siku.....asante kwa kuchangia!
 
Nawashukuru wote (nimewaachia thanks kwenye posts zenu)..baba Mtu, 3D na Kakuruvi kwa kuchangia. Tumepoteza msanii mahiri ambaye aliipenda Tanzania na watanzania wengi , hasa walahahoi walimpenda!
 
[MWANAIDI - Matimila]

(Kibao MWANAIDI kilipigwa na wana Matimila enzi hizo.
Sauti ni za Skassy Kasambula, Kyanga Songa, Fan fan na solo
ni la Batii Osenga bila kumsahau Mbwana Cox katika rythim)

nimetokea kumpenda binti Mwanaidi
nimeridhishwa na tabia yake
nikaamua tufunge nae pingu za maisha
urithi ulioacha baba niliutumia
ili kuneemesha ukoo wake
nilianza kuuza mifugo
hatimaye shamba
ili kumtosholeza mahitaji yake ehhh

baada ya miezi michache nikapata barua kutoka kwa Mwanaidi
..... .. kuwa yeye hanitaki tena
tena hawezi kuolewa na mimi

(wote)
mimi najuta eh najuta mama
gharama nilizogharamia
ameona bure
sijui la kufanya .. nasikitika oh
sababu yako ....... Mwanaidi x 3

Nafikiri hawa walikuwa ni orchestra Toma toma
 
SAUTI YA MNYONGE

Mama yeh yeh yeh yeeeh
Mama ninalia weh
Mama uko wapi
Mama nateseka eh
Mama umejificha wapi
Mama yoh yoh yoh yoh yoh yohoooo...
Mama mi nalia ohooo
Mama mi nalia eheee
Mama mi nalia
Ninalia ohooo
Mama uko wapi
Mama weh
Mama uko wapi ohoo
Remmy analia eheee
Mama uko wapi ohoo
Uko wapi ohoo

Mimi mtoto yatima
Sina baba wala mama
Sina dada wala kaka
Sina ndugu mwenzenu
Sina ndugu mwenzenu ehee
Nikaombe kwa nani ihiii
Niende wapi

Najutia ulimwengu
Nimekosa nini mola
Unyimwa ndugu
Nikazaliwa peke yangu
Mwenzenu sina baba wala mama
Sina shangazi wala mjomba
Sina babu wala bibi
Niende wapi ohoo
Niende wapi eheee
Jamani niende wapi

Masomoni nimefukuzwa
Nalikuwa sina sare
Nalikuwa sina viatu
Nalikuwa sina madaftari
Nimekwenda eh kwa mwalimu mkuu
Mwalimu nihurumie ehee mwalimu
Baba yangu ni kiwete eheee
Mama yangu ni kipofu mwalimu
Madaftari nani ataninunulia mwalimu ehee
Unapinga kunisikiliza oh mwalimu
Amenifukuza kiroho mbaya
Shauri ya unyonge eh
Sababu ya unyonge
Sababu ya unyonge ehee
Niende wapi ohoo

Nimekwenda kuomba kazi nikaambiwa sina kisomo
Nimeuza machungwa nipate kula nikaambiwa sina kibali
Nimeuza big g nikaambiwa mimi mzururaji
Nimeuza sigara nikaambiwa mimi mlanguzi jamani
Sijui nile wapi ohooo
Jamani nile wapi eheee
Nikaombe kwa nani

Kijijini nimefika nikaambiwa mimi ni mwizi
Ngedere kala mahindi nikaambiwa ni mimi
Nguruwe kala mihogo nikasingiziwa ni mimi
Jirani akiibiwa naambiwa ni mimi jamani
Sijui niishi wapi ohooo
Jamani niishi wapi eheee
Uko kijijini nakoishi hakuna bia
Uko kijijjini nakolima hakuna stoo ya soda
Sasa uniambie ninywe nini ehee
Jamani naomba kinywaji ninywe gongo
Gongo pombe ya wanyonge ehe
Gongo pombe ya wakulima
Nikinywa gongo nalima kama punda
Nikinywa gongo nalima kama farasi
Hiyo nyanya unanunua kariakoo unajua inatoka wapi
Kwa sisi walevi wa gongo uko kijijini
Sisi ndio tunanguvu ya kulima
Jamani nasikitika ehee
Niende wapi ohooo
Jamani niende wapi ohooo
Mimi sikusoma
Hata ulaya wazungu wengine hawakusoma
Sisi wote tukisoma
Nani atamsomesha mwenzie
Jamani nanyanyaswa ohoo
Niende wapi ehee
Jamani niende wapi ohoo
Sikupendelea nizaliwe kilema
Sikutaka kabisa nizaliwe kipofu
Nikiomba msininyime ehee
Nikipita msinicheke ehee
Mimi mtoto yatima
Pia ni mukulima
Nyumba nalijenga ya makuti
Nalalia ngozi la mbuzi
Chini kuna viroboto ohooo
Pia kuna kunguni ihiii
Jamani sina umeme ehee
Naishi kwa kibatari
Sina chandaruha
Hata kidonge ya klorokwini nyumbani kwangu sina
Naishi kimungu mungu
Naogopa ukimwi
Niende wapi ohooo
Wenye nguvu mnawajua vizuri
Matembezi yao ni kwa gari
Starehe zao kilimanjaro
Ukienda kilimanjaro sasa hivi utawakuta
Wake zao wamepaka lipstiki wazuri kama malaika
Watoto zao wote wanasoma ulaya
Niambie mimi mkulima jamani
Mwanangu shuleni amefukuzwa
Mke wangu anavyaa midabwada
Mimi mwenyewe sina pesa jamani
Niende wapi ohooo
Jamani niende wapi eheee
Nikaombe kwa nani
Mama yoh yoh yoh yoh
Mama ninalia weh
Mama uko wapi
Mama nateseka ohooo....

Mama yeh yeh yeh yeeeh
Baba ninalia weh
Baba uko wapi
Baba nateseka eh
Baba umejificha wapi
Mama yoh yoh yoh yoh yoh yohoooo...
Mama mi nalia eheee
Remmy analia ohooo
Masikini remmy analia ohooo remmy weh
Remmy ni mnyonge ehe
 
SAUTI YA MNYONGE

Mama yeh yeh yeh yeeeh
Mama ninalia weh
Mama uko wapi
Mama nateseka eh
Mama umejificha wapi
Mama yoh yoh yoh yoh yoh yohoooo...
Mama mi nalia ohooo
Mama mi nalia eheee
Mama mi nalia
Ninalia ohooo
Mama uko wapi
Mama weh
Mama uko wapi ohoo
Remmy analia eheee
Mama uko wapi ohoo
Uko wapi ohoo

Mimi mtoto yatima
Sina baba wala mama
Sina dada wala kaka
Sina ndugu mwenzenu
Sina ndugu mwenzenu ehee
Nikaombe kwa nani ihiii
Niende wapi

Najutia ulimwengu
Nimekosa nini mola
Unyimwa ndugu
Nikazaliwa peke yangu
Mwenzenu sina baba wala mama
Sina shangazi wala mjomba
Sina babu wala bibi
Niende wapi ohoo
Niende wapi eheee
Jamani niende wapi

Masomoni nimefukuzwa
Nalikuwa sina sare
Nalikuwa sina viatu
Nalikuwa sina madaftari
Nimekwenda eh kwa mwalimu mkuu
Mwalimu nihurumie ehee mwalimu
Baba yangu ni kiwete eheee
Mama yangu ni kipofu mwalimu
Madaftari nani ataninunulia mwalimu ehee
Unapinga kunisikiliza oh mwalimu
Amenifukuza kiroho mbaya
Shauri ya unyonge eh
Sababu ya unyonge
Sababu ya unyonge ehee
Niende wapi ohoo

Nimekwenda kuomba kazi nikaambiwa sina kisomo
Nimeuza machungwa nipate kula nikaambiwa sina kibali
Nimeuza big g nikaambiwa mimi mzururaji
Nimeuza sigara nikaambiwa mimi mlanguzi jamani
Sijui nile wapi ohooo
Jamani nile wapi eheee
Nikaombe kwa nani

Kijijini nimefika nikaambiwa mimi ni mwizi
Ngedere kala mahindi nikaambiwa ni mimi
Nguruwe kala mihogo nikasingiziwa ni mimi
Jirani akiibiwa naambiwa ni mimi jamani
Sijui niishi wapi ohooo
Jamani niishi wapi eheee
Uko kijijini nakoishi hakuna bia
Uko kijijjini nakolima hakuna stoo ya soda
Sasa uniambie ninywe nini ehee
Jamani naomba kinywaji ninywe gongo
Gongo pombe ya wanyonge ehe
Gongo pombe ya wakulima
Nikinywa gongo nalima kama punda
Nikinywa gongo nalima kama farasi
Hiyo nyanya unanunua kariakoo unajua inatoka wapi
Kwa sisi walevi wa gongo uko kijijini
Sisi ndio tunanguvu ya kulima
Jamani nasikitika ehee
Niende wapi ohooo
Jamani niende wapi ohooo
Mimi sikusoma
Hata ulaya wazungu wengine hawakusoma
Sisi wote tukisoma
Nani atamsomesha mwenzie
Jamani nanyanyaswa ohoo
Niende wapi ehee
Jamani niende wapi ohoo
Sikupendelea nizaliwe kilema
Sikutaka kabisa nizaliwe kipofu
Nikiomba msininyime ehee
Nikipita msinicheke ehee
Mimi mtoto yatima
Pia ni mukulima
Nyumba nalijenga ya makuti
Nalalia ngozi la mbuzi
Chini kuna viroboto ohooo
Pia kuna kunguni ihiii
Jamani sina umeme ehee
Naishi kwa kibatari
Sina chandaruha
Hata kidonge ya klorokwini nyumbani kwangu sina
Naishi kimungu mungu
Naogopa ukimwi
Niende wapi ohooo
Wenye nguvu mnawajua vizuri
Matembezi yao ni kwa gari
Starehe zao kilimanjaro
Ukienda kilimanjaro sasa hivi utawakuta
Wake zao wamepaka lipstiki wazuri kama malaika
Watoto zao wote wanasoma ulaya
Niambie mimi mkulima jamani
Mwanangu shuleni amefukuzwa
Mke wangu anavyaa midabwada
Mimi mwenyewe sina pesa jamani
Niende wapi ohooo
Jamani niende wapi eheee
Nikaombe kwa nani
Mama yoh yoh yoh yoh
Mama ninalia weh
Mama uko wapi
Mama nateseka ohooo....

Mama yeh yeh yeh yeeeh
Baba ninalia weh
Baba uko wapi
Baba nateseka eh
Baba umejificha wapi
Mama yoh yoh yoh yoh yoh yohoooo...
Mama mi nalia eheee
Remmy analia ohooo
Masikini remmy analia ohooo remmy weh
Remmy ni mnyonge ehe
 
SAUTI YA MNYONGE

Mama yeh yeh yeh yeeeh
Mama ninalia weh
Mama uko wapi
Mama nateseka eh
Mama umejificha wapi
Mama yoh yoh yoh yoh yoh yohoooo...
Mama mi nalia ohooo
Mama mi nalia eheee
Mama mi nalia
Ninalia ohooo
Mama uko wapi
Mama weh
Mama uko wapi ohoo
Remmy analia eheee
Mama uko wapi ohoo
Uko wapi ohoo

Mimi mtoto yatima
Sina baba wala mama
Sina dada wala kaka
Sina ndugu mwenzenu
Sina ndugu mwenzenu ehee
Nikaombe kwa nani ihiii
Niende wapi

Najutia ulimwengu
Nimekosa nini mola
Unyimwa ndugu
Nikazaliwa peke yangu
Mwenzenu sina baba wala mama
Sina shangazi wala mjomba
Sina babu wala bibi
Niende wapi ohoo
Niende wapi eheee
Jamani niende wapi

Masomoni nimefukuzwa
Nalikuwa sina sare
Nalikuwa sina viatu
Nalikuwa sina madaftari
Nimekwenda eh kwa mwalimu mkuu
Mwalimu nihurumie ehee mwalimu
Baba yangu ni kiwete eheee
Mama yangu ni kipofu mwalimu
Madaftari nani ataninunulia mwalimu ehee
Unapinga kunisikiliza oh mwalimu
Amenifukuza kiroho mbaya
Shauri ya unyonge eh
Sababu ya unyonge
Sababu ya unyonge ehee
Niende wapi ohoo

Nimekwenda kuomba kazi nikaambiwa sina kisomo
Nimeuza machungwa nipate kula nikaambiwa sina kibali
Nimeuza big g nikaambiwa mimi mzururaji
Nimeuza sigara nikaambiwa mimi mlanguzi jamani
Sijui nile wapi ohooo
Jamani nile wapi eheee
Nikaombe kwa nani

Kijijini nimefika nikaambiwa mimi ni mwizi
Ngedere kala mahindi nikaambiwa ni mimi
Nguruwe kala mihogo nikasingiziwa ni mimi
Jirani akiibiwa naambiwa ni mimi jamani
Sijui niishi wapi ohooo
Jamani niishi wapi eheee
Uko kijijini nakoishi hakuna bia
Uko kijijjini nakolima hakuna stoo ya soda
Sasa uniambie ninywe nini ehee
Jamani naomba kinywaji ninywe gongo
Gongo pombe ya wanyonge ehe
Gongo pombe ya wakulima
Nikinywa gongo nalima kama punda
Nikinywa gongo nalima kama farasi
Hiyo nyanya unanunua kariakoo unajua inatoka wapi
Kwa sisi walevi wa gongo uko kijijini
Sisi ndio tunanguvu ya kulima
Jamani nasikitika ehee
Niende wapi ohooo
Jamani niende wapi ohooo
Mimi sikusoma
Hata ulaya wazungu wengine hawakusoma
Sisi wote tukisoma
Nani atamsomesha mwenzie
Jamani nanyanyaswa ohoo
Niende wapi ehee
Jamani niende wapi ohoo
Sikupendelea nizaliwe kilema
Sikutaka kabisa nizaliwe kipofu
Nikiomba msininyime ehee
Nikipita msinicheke ehee
Mimi mtoto yatima
Pia ni mukulima
Nyumba nalijenga ya makuti
Nalalia ngozi la mbuzi
Chini kuna viroboto ohooo
Pia kuna kunguni ihiii
Jamani sina umeme ehee
Naishi kwa kibatari
Sina chandaruha
Hata kidonge ya klorokwini nyumbani kwangu sina
Naishi kimungu mungu
Naogopa ukimwi
Niende wapi ohooo
Wenye nguvu mnawajua vizuri
Matembezi yao ni kwa gari
Starehe zao kilimanjaro
Ukienda kilimanjaro sasa hivi utawakuta
Wake zao wamepaka lipstiki wazuri kama malaika
Watoto zao wote wanasoma ulaya
Niambie mimi mkulima jamani
Mwanangu shuleni amefukuzwa
Mke wangu anavyaa midabwada
Mimi mwenyewe sina pesa jamani
Niende wapi ohooo
Jamani niende wapi eheee
Nikaombe kwa nani
Mama yoh yoh yoh yoh
Mama ninalia weh
Mama uko wapi
Mama nateseka ohooo....

Mama yeh yeh yeh yeeeh
Baba ninalia weh
Baba uko wapi
Baba nateseka eh
Baba umejificha wapi
Mama yoh yoh yoh yoh yoh yohoooo...
Mama mi nalia eheee
Remmy analia ohooo
Masikini remmy analia ohooo remmy weh
Remmy ni mnyonge ehe
 
Huyu jamaa nikiwa mdogo nilikua najua ni mngoni kumbe ni mtu wa Congo ila aliipenda sana nchi ya tanzania
 
Back
Top Bottom