George Jinasa
JF-Expert Member
- Sep 14, 2010
- 399
- 52
Kwa wale mliokuwa Luhira miaka ya mwanzo ya tisini mtamkumbuka mwalimu mmoja maalufu wa sayansi naomba nisimtaje jina lake mtamjua tu. Yeye alikuwa mwnafunzi wa arts ukikosea anakataa kukupiga. Utamsikia anasema; ' Sikuchapi. Nimekustukia unataka sifa. Nikikuchapa utajisifu kuwa umepigwa na mwalimu mwenye Bachellors of Science with Honour"
Je Mnamkumbuka mwalimu mwingine mwenye kupenda kufuga nywele ndefu. Yeye alikuwa ananunua dagaa duka la jirani na shule anawatafuna wanaisha kabla hajafika nyumbani.
Maharage ya mbinga mnayakumbuka.
Wale mliokuwa mnatoboa usiku kama mimi mliwahi kukutana na vibwengo?
Choo cha milango saba mnakikumbuka. Sharti moja wapo la kuingia ni kwamba unavua nguo zote hadi za ndani na ukitoka unatoka mbio. Hekima yake ni kwamba ukibaki na nguo ile harufu utaishi nayo wingi nzima.
Weekly Reports mnazikumbuka. Sisi ndio zilikuwa zinatusaidia mitaani kuthibitisha kama ni wasomi. Ukiulizwa unajua kingereza unasema ndio. Ukiambuwa useme unaanza " Ministry of Education, Songea Boys Secondary School, the Weekly Report".
Tuanzisheni mtandao wetu wa box mbili
Je Mnamkumbuka mwalimu mwingine mwenye kupenda kufuga nywele ndefu. Yeye alikuwa ananunua dagaa duka la jirani na shule anawatafuna wanaisha kabla hajafika nyumbani.
Maharage ya mbinga mnayakumbuka.
Wale mliokuwa mnatoboa usiku kama mimi mliwahi kukutana na vibwengo?
Choo cha milango saba mnakikumbuka. Sharti moja wapo la kuingia ni kwamba unavua nguo zote hadi za ndani na ukitoka unatoka mbio. Hekima yake ni kwamba ukibaki na nguo ile harufu utaishi nayo wingi nzima.
Weekly Reports mnazikumbuka. Sisi ndio zilikuwa zinatusaidia mitaani kuthibitisha kama ni wasomi. Ukiulizwa unajua kingereza unasema ndio. Ukiambuwa useme unaanza " Ministry of Education, Songea Boys Secondary School, the Weekly Report".
Tuanzisheni mtandao wetu wa box mbili