Mcheza Karate
JF-Expert Member
- Jun 30, 2011
- 690
- 350
"mh. Spika hatukupokea senti tano ya mtu wala baiskeli yake. Mwenye ushahidi tofauti, basi alithibitishie bunge hili tukufu.(Dr.H.Mwakyembe, Dodoma, 6. Feb.2008)". "Mh. Spika nimesimama hapa kuelezea masikitiko yangu ofisi ya bunge hadi ofisini kwangu hata kama wangeniita ningekwenda kwa miguu kama hamna gari na nilikuwa tayari kufanya hivyo, nimeonewa sana ktk hili"(Edward N. Lowassa, Dodoma, Feb,7,2008). "Mh.Spika napenda nitumie nafasi hii pia kumshukuru kwa moyo wa dhati kabisa mh. Edward Lowassa aliyeamua kujiuzulu kutokana na kuipenda nchi yake"(Mizengo Pinda Dodoma Feb,9,2008). Mwana JF umewahi kutafakari kauli hizi namna zinavyokanganya? Kumbe EL anaipenda sana nchi yake?(nadhani TANZANIA). Kumbe mratibu na mtekelezaji wa shughuli za serikali anamjua EL jinsi anavyoipenda nchi yake kumbe!!!!!!!!!! Hebu tafakari kabla ya kutoa jibu.