Tujikumbushe enzi za madaladala maarufu

Dar mpaka Moro - Moody Punk, Chisu Papino enzi hizo stendi iko pale magomeni mapipa karibu ya hoteli moja maarufu sana michuzi mikali...
 
songea-dar kulikuwa na kiswele --hakuna basi lingine lililotia mguu njia ile miak nenda miaka rudi
 
Back to tose days 1980's - mwanza

Mjini to pansiansi express ina itwa UPENDO ilikuwa ya blue na
Nyingine ilikuwa y Kijani toka mjini kwenda Mwaloni(Kirumba)

INGEMBESAMBO hiyo naikumbuka mpaka
 
Kuna ile UDA flani ilikuw anapiga ruti ya Mbagala posta, ilikuwa na muziki mkubwa utazani mko Bilicanaz.. siku za week end huikosi kule Ndege Beach..
 
Dar - Mbinga lilikuwepo "Supu ya Mawe- Iga Ufe" walipeleka ushindani sana kwa zile injini nyuma za kiswele!

kule Iringa enzi hizo ulikuwa na SONY mini bus za kwanza kwanza Isuzu na kuna wakati ilikuwa inakwenda Tosamaganga

Njombe - Lupembe alikuwepo FIKIRI Kwanza ....Tena Fikiri Sana. milango miwili na amigo! tih tih

Na pia Njombe Kifanya - ndio ilikuwa ruti ya Babu yangu; Masikini Jeuri!

Ilembula - Makambako kulikuwa na Kijombe!

Iringa - Mbeya : Victoria Tours

Iringa Mjini kulikuwa na zile Isuzu za kuchongwa bodi: LOVE IN TOKYO za mzee Mmasi (RIP) Bilakuwa sahau wahindi wale wa JIHANGRI na kina Huwel na ile BALUCHISTAN na almaarufu Mzee SHARJI (cjui yupo hai?)

Buguruni Posta : BEACH BOYZ

Vingunguti Posta: FITINA zile scania za kulala upande mmoja; mpaka raha ikianza kuondoka posta ya zamani!

Mwananyamala Stesheni; kulikuwa na basi la Mtumba WIFI NAE; du watu tulikuwa tunakacha kupanda daladal nyingine mpa WIFI lije! teh teh

Kurasini Shimo la Udongo/Kariakoo KITMEER ENTERPRISES zilikuwa kama uniform za hiyo njia

Chai Maharage maarufu Posta Gongola Mboto; Aunt K na Ndaga Kyala! teh teh zilikuwa na mziki mnene we acha tu a kuibiwa ilikuwa ni lazima; niliibiwa saa yangu ya DISCO (unaifahamu?)

Kudos mtoa mada umeturudisha mbali sana
 
songea-dar kulikuwa na kiswele --hakuna basi lingine lililotia mguu njia ile miak nenda miaka rudi

baba umenitoa machozi, ile kiswele haitatokea tena, kule nyuma imeandikwa iga ufe supu ya mawe, halafu umkute dereva mwenyewe marehemu wiligisi, haha wanatoka songea saa kumi na mbili asubuhi wanafika dar saa kumi na moja jioni wakati mabasi mengine yanafika saa mbili usiku, mbaya zaidi wakitoka dar saa kumi na mbili nilishudia mwenyewe saa kumi basi linafika bombambili wanasimama pale saa nzima wanaogopa kukamatwa na trafiki. Ile ilikuwa mashine kubwa
 
baba umenitoa machozi, ile kiswele haitatokea tena, kule nyuma imeandikwa iga ufe supu ya mawe, halafu umkute dereva mwenyewe marehemu wiligisi, haha wanatoka songea saa kumi na mbili asubuhi wanafika dar saa kumi na moja jioni wakati mabasi mengine yanafika saa mbili usiku, mbaya zaidi wakitoka dar saa kumi na mbili nilishudia mwenyewe saa kumi basi linafika bombambili wanasimama pale saa nzima wanaogopa kukamatwa na trafiki. Ile ilikuwa mashine kubwa

Supu ya mawe haikuwa Basi ya Kiswele; ilkuwa ni kampuni nyingine rivals wa Kiswele; hawa walikuwa wanfika mpaka Mbinga actualy it is the only bus nafikiri mpaka sasa ambalo lilifanya ruti ya Dar-Mbinga; Jamaa alikuwa na basi moja tu lakini ilimchanganya Kiswele mpaka akadhani ziko basi 2 kwa jinsi ya 2 kwa 1 alizokuwa akipigwa!
 
Safari masters sikumbuki ilikwenda wapi

Mnakumbuka enzi hizo barabara ya Tanzania - Zambia ilkuwa na basi zina kula mzigo wa kufa mtu kwenye zile carrier za juu ya basi; Ikitoka dar ilikuwa inakula boksi mpaka inakata nyaya za simu njiani; na ikitoka Mkoani inakula gunia za viazi zinasimamishwa wima ; ama tenga za nyanya; mfumajia alikuwa ni lazima awe mtu wa futi sita na anaufuma mzigo huko juu kwa kipimo chake!Ilikuwa ni mchezo wa wafanyabiashara ulipoanzia kuwahonga madereva kuwahisha mizigo dar au mkoani.

Nakumbuka Zainab's na Scandanavia walikamatwa (of coz kizushi nadhani hawakuwa wamefika dau) wakaletwa Mahakamani pale Iringa mjini; wanokumbuka enzi hizo Iringa ina mahakama moja tu pale kwenye yale majengo yaliyoachwa na Mjerumani! Haya mabasi yalishindwa kupaki pale na ikalazimu yabaki barabarani kuelekea hospitali ya Mkoa.
Ilkuwa hatari tupu!
 
Kwa daladala tu, Tanga wameniacha hoi manake kila daladala lazima liwe limepigwa chata ya jina la msanii au winbo unaotamba na zote miziki ni minene na iko juu yaani kama daladala haina mziki basi watu hawapandi. Southern Highlands-IGESA LINE
 
Ubungo-Posta (Jai Shanka), Manzese Kariakoo (Tilikia), M'nyamala-k'koo (Ushora Ndago).
Nakumbuka Dunia hadaa ilikuwa ya mzee mmoja wa kiarabu pale Tandika-Chihota, pia alikuwa na mashine ya kusaga nafaka.
 
Dah.. mimi nilikuona tuu naona hizo daladala nikenda shule nikiwa ndani ya Cidiz la baba !.. haswa hasa Mbibi, kabibi - Posta - Masaki.
 
Leo nimekumbuka sana zile enzi za madalada zenye majina maarufu ....wakati tukiwa madenti yaani ujanja ni kuwa 'staff' kwenye daladala maana yake haulipi nauli sababu makonda au dereva ni washkaji..ilikuwa raha kwelikweli.....kama konda hakujui akikuomba nauli unamwambia mi staff...muulize dereva..dah ...
Temeke Posta - Dunia Hadaa( hizi zilikuwa za mwanzo kabisa-Temeke/Tandika Posta),Riziki kwa mungu ,Golo, Kainkwa,Kita Ngoma nk.....Kwa upande wa Ubungo posta kulikuwa na yakle marefu makubwa ..nakumbuka Matema Beach....tukumbushane wadau......

Old Korogwe-Manundu ilikuwepo Kaizibe kama waijua!
 
Gongolamboto - Kariakoo Kulikuwa na Mfugale, NDL, ROSA, FAMAGUSTA nk
Tandika - Kariakoo kulikuwa na Black Power
 
mbeya kulikua na mwailubi,urassa,sokolo,mbembela,double coaster ya kwanza mbeya nzima el_kibo,karanja ilikua inapiga tripu tukuyu-mbeya mjini,wengine wataongezea.

Kyela-mbeya ilikuwepo LEA WATOTO, HUDUMA (la mwenye lift valey hotel), NTAHENA, UPENDO, KARANJA. humo ni kupakia mikungu ya ndizi na mafuta ya mawese. Teh, teh,
 
Bakukijana, kumbuka Ile maneno inaitwa MBOGO'ULENJE pale Mbeya, kipiga ruti za Igoma Tunduma. Ile kitu ilikuwa haina mfano wake, Leyland Albion, ikipiga ile kinanda yake inasikika umbali wa kilometa kadhaa! Gia yake ndefu kama fimbo ya kuchezea pool!
Maisha haya bana!
na kuna goma lilikuja lilikua linaitwa MGANGALUMA mnalikumbuka?
Kyela-mbeya ilikuwepo LEA WATOTO, HUDUMA (la mwenye lift valey hotel), NTAHENA, UPENDO, KARANJA. humo ni kupakia mikungu ya ndizi na mafuta ya mawese. Tehlikumbuka?, teh,
ndio halafu kuna scania moja nimesahau kidogo jina ila ni southern cross au????
 
Back
Top Bottom